Neno la Asubuhi: Kula nyama za watu

Neno la Asubuhi: Kula nyama za watu

mitale na midimu

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2015
Posts
10,419
Reaction score
17,759
Kupiga majungu, kumuongea mwenzako pembeni mambo ambayo ulipaswa kumwambia moja kwa moja, Kusingiziana ili mmoja akandamizwe na mwingine atumie hiyo kama ngazi, kusambaza umbea, kuchongeana,Kutokusema ukweli kwa maslahi binafsi ili ukimya huo ukunufaishe kwa njia moja au nyingine, kumbomoa mwenzako kwa hila,etc tabia hizi hufananishwa na kula nyama ya watu (Cannibalism).

Lengo la maneno haya, huwa ni kumjeruhi muhusika kihisia,kisaikolojia na kijamii. Asilimia karibu 90 ya magonjwa tunayopata huanzia akilini. Matokeo yake watu wamekuwa na misongo ya mawazo na wengine hata kufariki. na hii ndiyo sababu vitendo hivi kifananishwa na kula nyama ya mtu hadi kuhakikisha umemmaliza na kumuua kabisa.

NINI UFANYE?
1: Usichangie kwa ushabiki kitu ambacho huna uhakika kama ni kweli kumuhusu mwenzako.
Kama hauna uhakika useme,
2:Watu wengi huwasema vibaya wengine ili wao waonekane au wajisikie vizuri. Ni vizuri kujua nia ya unachoongea, na kama unasukumwa na kisasi,chuki,kukomoa Muombe Mungu akupe nia nzuri.
3:Kuza tabia ya kuwa mzito kuongea na mwepesi kusikiliza.
4:Ikiwezekana kwepa kabisa kukaa meza moja na wala watu.

tabia hii ni maarufu sana makazini, mijumuiko ya kiimani na mijumuiko katika mambo ya kijamii.


:: Ndugu Msisingiziane... (Yakobo 4:11)
:: Speak not evil one of another, Bretheren (James 4:11,KJV)
 
Kweli kabisa.
Home ilifikia wakati wakaniita bubu anayeongea.
Marafiki wananiambia kama nisingesoma ningekuwa bonge la mshamba, yote nawaambia siko kama mnavyoniwazia.
Una kipaji,mi kukaa kimya siwezi aisee hasa kwa watu niliowazoea,ila ugenini aaaah wanaweza sema mi mkimya kweli kweli
 
Kweli kabisa.
Home ilifikia wakati wakaniita bubu anayeongea.
Marafiki wananiambia kama nisingesoma ningekuwa bonge la mshamba, yote nawaambia siko kama mnavyoniwazia.
winston spenser Churchill aliwahi kusema nikipewa Dakika 50 kuongea nitatumia dakika 48 kujiandaa na kuongea dakika 2.
usomi haujengwi na wingi wa maneno mkuu, bali ubora na nguvu iloyochangamana na maneno hayo.
ungekuwa mbali sana.
 
Una kipaji,mi kukaa kimya siwezi aisee hasa kwa watu niliowazoea,ila ugenini aaaah wanaweza sema mi mkimya kweli kweli
hahahaa
mimi kama nina kitu cha kusema ntakisema hata kama mbele yangu kuna mtu mmoja au laki.
najifunza kunyamaza siku hizi, hasa baada ya kugundua kuna watu wengine huwa wanakuwa insecure na kudhani natamani nafasi flani walizo nazo.
Pia ukiongea sana, unakoswa fursa ya kujifunza mengi.
 
hahahaa
mimi kama nina kitu cha kusema ntakisema hata kama mbele yangu kuna mtu mmoja au laki.
najifunza kunyamaza siku hizi, hasa baada ya kugundua kuna watu wengine huwa wanakuwa insecure na kudhani natamani nafasi flani walizo nazo.
Pia ukiongea sana, unakoswa fursa ya kujifunza mengi.
Ni kweli kabisa sema kuna kuongea na kuropoka,mi ni muongeaji,msikilizaji pia ila sio mropokaji
 
winston spenser Churchill aliwahi kusema nikipewa Dakika 50 kuongea nitatumia dakika 48 kujiandaa na kuongea dakika 2.
usomi haujengwi na wingi wa maneno mkuu, bali ubora na nguvu iloyochangamana na maneno hayo.
ungekuwa mbali sana.
It's true.
Niliwahi kukwazana na baba mdogo, akaniweka kikao mbele ya wazee ili ijulikane mimi ni mkosaji.
Aliongea mambo mengi sana, wazee wakasema sasa kijana ongea tukusikilize.

Nilitumia muda kidogo kuongea mambo mengi yenye ukweli tupu. Hadi wale wazee wakabaki wanamshangaa.

Ukimya wakati mwingi huniepusha na mambo ambayo yangeniweka pabaya.
 
Una kipaji,mi kukaa kimya siwezi aisee hasa kwa watu niliowazoea,ila ugenini aaaah wanaweza sema mi mkimya kweli kweli
Ni kipaji pale unapokuwa unajua siri nyingi na mambo mengi mazuri na mabaya ya watu lakini husemi lolote kwa mtu yeyote.

Usiri na ukimya wangu umenifanya kujua mengi na kuambiwa mengi na rafiki,ndugu na jamaa toka udogoni na hata sasa ujanani.
 
Back
Top Bottom