Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dk Samuel Gwamaka amesema baada ya kutafakari athari za kiuchumi, wafanyabiashara 20 walioandika barua na kukiri makosa yao wamefunguliwa.
Dk wamaka amesema, wapo waliokiri na kuandika barua, na kulipa faini.
“Ni mara ya kwanza tulilazimika kuwafungia baada ya kutoa elimu kwa miaka mitano, watu walikuwa hawalali licha ya malalamiko yakiongezeka,” amesema Gwamaka.
Amesema walitumia mbinu mbalimbali ikiwemo kuwaita wamiliki wote na kutoa elimu kuanzia ngazi ya mkoa na baadae ngazi ya ya halmashauri.
“Kelele ziliendelea na malalniko yaliendele tukatoa angalizo watakaoendelea kukiu sheria kuanzia Mei Mosi, hatua zitachukuliwa, baada ya kuona tumeanza kuchukua ndio wakashtuka,” amesema na kuongeza:
“Kila mtu ana nafasi yake kuna washehereshaji lakini pia kuna wenye ajira, lakini kuna watu walioathitirika na wengine kufariki,” amesema.
Miongoni mwa baa na kumbi za starehe zilizokuwa zimefungiwa ni Boarddroom, Wavuvi Camp, Warehouse, Avoco, Kitambaa Cheupe. Wengine ni Element, Chako ni Chako, Rainbow, Gentlemen, Liquid na Soweto.
Dk wamaka amesema, wapo waliokiri na kuandika barua, na kulipa faini.
“Ni mara ya kwanza tulilazimika kuwafungia baada ya kutoa elimu kwa miaka mitano, watu walikuwa hawalali licha ya malalamiko yakiongezeka,” amesema Gwamaka.
Amesema walitumia mbinu mbalimbali ikiwemo kuwaita wamiliki wote na kutoa elimu kuanzia ngazi ya mkoa na baadae ngazi ya ya halmashauri.
“Kelele ziliendelea na malalniko yaliendele tukatoa angalizo watakaoendelea kukiu sheria kuanzia Mei Mosi, hatua zitachukuliwa, baada ya kuona tumeanza kuchukua ndio wakashtuka,” amesema na kuongeza:
“Kila mtu ana nafasi yake kuna washehereshaji lakini pia kuna wenye ajira, lakini kuna watu walioathitirika na wengine kufariki,” amesema.
Miongoni mwa baa na kumbi za starehe zilizokuwa zimefungiwa ni Boarddroom, Wavuvi Camp, Warehouse, Avoco, Kitambaa Cheupe. Wengine ni Element, Chako ni Chako, Rainbow, Gentlemen, Liquid na Soweto.