WALIMU wa Shule za Sekondari na wazee wa watoto waliofutiwa matokeo ya mitihani ya kidato cha nne Zanzibar, wanakusudia kulishitaki mahakamani Baraza la Mithani la Taifa (Necta) kwa kutoa adhabu ya ujumla kwa wanafunzi ambayo ni kinyume na sheria za nchi.
Wazee hao pamoja na walimu walitoa msimamo huo katika ukumbi wa Baitul-Yamin karibu na Hoteli ya Bwawani, Zanzibar, ambapo palikuwa na mjadala wa wazi kuhusiana na kadhia hiyo ya kufutiwa watoto wao mitihani.
Bila ya kutaja kifungu gani katika sheria za makosa ya jinai, washiriki wa mjadala huo walieleza kuwa kwa mujibu wa sheria hiyo ni kosa kutoa hukumu za jumla.
Walisema Necta hawezi kuwafutia watoto wote kwakosa la mtu mmoja na pia kuwazuia kufanya mitihani kwa muda wa miaka mitatu.
Wanaovujisha mitihani ni wao halafu wanakwenda kuwafutia watoto wetu matokeo na uzembe ni wao, kwa hili hatuwezi kukubali, alisema mzee Ali Hassan ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kati.
Mzee Hassan alifahamisha kuwa mtoto wake yeye alikuwa anashika nafasi za mwanzo katika matokeo ya mitihani darasani lakini Necta wanasema hana uwezo.
Hawezi mtu na akili zake kuandika nyimbo za bongo fleva wakatumia fursa hiyo kuwakandamiza wengine, hiyo ni mipango yao katika kuwafelisha watoto wetu, alieleza mzee Hassan.
Wazee na walimu hao waliitaka Necta kupeleka katika shule zote ushahidi wa karatasi za mitihani zilichafuliwa kwa kuandika mambo ambayo hayahusiani na majibu.
Kwa upande wao, waalimu ambao washiriki katika kusahihisha mitihani walisema walimwambia Katibu wa Necta, Dk Joyce Ndalichako kuwa mitihani imevuja lakini yeye alikataa.
Tulimwambia mithani imevuja ni vyema ikarudiwa kulikoni kuwafutia matokeo kwa baraza halitotenda haki hapo, alifahamisha mwalimu wa shule ya Laurent, Hemmed Soud.
Alisema wanachofanya Necta ni kuua maendeleo ya elimu katika visiwa vya Zanzibar ili ionekane kuwa hukuna wataalamu.
Mwalimu huyo alidai suala la kutembelea katika mikoa tofauti Katibu huyo wa Necta ni kuweka kiini macho tu.
Tangu kutangazwa kwa matokeo ya mitihani hiyo zaidi ya wiki moja sasa, kumekuwa na mijadala mizito kufuatia watoto 3,301 kufutiwa matokeo yao kwa kile kinachodaiwa kwa kufanya udanganyifu
Wazee hao pamoja na walimu walitoa msimamo huo katika ukumbi wa Baitul-Yamin karibu na Hoteli ya Bwawani, Zanzibar, ambapo palikuwa na mjadala wa wazi kuhusiana na kadhia hiyo ya kufutiwa watoto wao mitihani.
Bila ya kutaja kifungu gani katika sheria za makosa ya jinai, washiriki wa mjadala huo walieleza kuwa kwa mujibu wa sheria hiyo ni kosa kutoa hukumu za jumla.
Walisema Necta hawezi kuwafutia watoto wote kwakosa la mtu mmoja na pia kuwazuia kufanya mitihani kwa muda wa miaka mitatu.
Wanaovujisha mitihani ni wao halafu wanakwenda kuwafutia watoto wetu matokeo na uzembe ni wao, kwa hili hatuwezi kukubali, alisema mzee Ali Hassan ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kati.
Mzee Hassan alifahamisha kuwa mtoto wake yeye alikuwa anashika nafasi za mwanzo katika matokeo ya mitihani darasani lakini Necta wanasema hana uwezo.
Hawezi mtu na akili zake kuandika nyimbo za bongo fleva wakatumia fursa hiyo kuwakandamiza wengine, hiyo ni mipango yao katika kuwafelisha watoto wetu, alieleza mzee Hassan.
Wazee na walimu hao waliitaka Necta kupeleka katika shule zote ushahidi wa karatasi za mitihani zilichafuliwa kwa kuandika mambo ambayo hayahusiani na majibu.
Kwa upande wao, waalimu ambao washiriki katika kusahihisha mitihani walisema walimwambia Katibu wa Necta, Dk Joyce Ndalichako kuwa mitihani imevuja lakini yeye alikataa.
Tulimwambia mithani imevuja ni vyema ikarudiwa kulikoni kuwafutia matokeo kwa baraza halitotenda haki hapo, alifahamisha mwalimu wa shule ya Laurent, Hemmed Soud.
Alisema wanachofanya Necta ni kuua maendeleo ya elimu katika visiwa vya Zanzibar ili ionekane kuwa hukuna wataalamu.
Mwalimu huyo alidai suala la kutembelea katika mikoa tofauti Katibu huyo wa Necta ni kuweka kiini macho tu.
Tangu kutangazwa kwa matokeo ya mitihani hiyo zaidi ya wiki moja sasa, kumekuwa na mijadala mizito kufuatia watoto 3,301 kufutiwa matokeo yao kwa kile kinachodaiwa kwa kufanya udanganyifu