Uchaguzi 2020 NEC na ZEC, hadi tupeane makavu?

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,822
35,817
Mabibi na mabwana heshima kwenu na moja kwa moja kwenye mada.

Ninaamini kumekuwapo na kujizuia kwa hali ya juu wanazuoni wanaita subira kutoka kwa wanaoathirika moja kwa moja na maamuzi yenu na kwa muda mrefu tu.

Jamani tusiache subira hizi kufika ukomo.

NEC na ZEC mnayo sababu na uwezo wa kuiepushia shari nchi hii. Kinachoombwa kwenu mbona ni kidogo mno na cha msingi tu?

"Mnaombwa uchaguzi ulio huru na wa haki." Ni hivyo tu basi. Si zaidi wala si pungufu.

Haki huambatana na jitihada za wazi kuielekea kuonekana kuwa kweli zinafanyika. Hapa tulipo ni muhimu sana sasa mkawarejesha wale wagombea wote walioenguliwa na hasa wale wanaolalamika kutokutendewa haki.

Inafahamika kuwa wapo wagombea walionunuliwa ili waenguliwe. Hao kama takukuru kaona ni sawa waacheni takukuru watabeba mzigo wao wenyewe.

Hivi, mtapata hasara gani kwa kuchukua msimamo kama huo wa kuwarejesha wagombea wanaolalamika, ambao mh. Jaffo alipata kuutumia kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa uliopita?

Uchaguzi 2020 - Tume ya Uchaguzi ya uenguaji, somo la Jaffo haliwafai?

Pana vyama wagombea wao wako kwenye media zote muda wote na hata wakitumia lugha za makabila yao kutoa kejeli, vitisho na labda hata matusi. Yaliyotokea kanda ya ziwa na hata yanayoendelea hasa Tarime ni mfano mzuri wa hali ilikofikia.

Pana vyama vinaminywa na kunyimwa fursa zote. Majukumu yenu nyie kama wenye mamlaka na uchaguzi huu ni nini kama hamuwezi kutuwekea mazingira yaliyo sawa, huru wala ya haki?

Mbona Sirro amejitahidi na juhudi zake walau zinaonekana?

Pongezi Sirro, Mahakama na Tume ya Uchaguzi kazi kwenu

Nakazia - NEC na ZEC msiache tufikie kuwapa makavu tunapoendelea kujizuia tukitegemea haki kutoka kwenu.

Ninawasilisha.
 
Pana haja ya vyama vilivyo athirika na maamuzi yao hawa kuwapa tarehe ya mwisho (deadline) ya kuwarejesha wagombea wote kwenye utaratibu wa uchaguzi.

Tume zisitumike kama rubber stamp ya kuhalalisha haramu.
 
Naona CDM wanajaribu kutumia ubavu wa Maalim kujitutumua, si CDM mtoe tamko tu nyie si ndio chama kikuu cha upinzani, kwa nini mnahangaika kusubiri tamko la Maalim Seif ?
 
Kwa bahati mbaya hakuna chochote cha ajabu kitakachotokea hata baada ya ZEC na NEC kupitisha panga na mahali pengine wakiendelea kuchelewesha majibu ya rufaa za wagombea zaidi ya kauli za kila siku za "sasa basi na tuwe na subira"

Maalim Seif amekua ni shock absorber wa hali ya kisiasa ya Zanzibar tangia yale mauwaji ya 2001 akizuia watu kuchukua hatua maana ataleta maafa na umwagaji damu. Kwavyovyote vile na mwaka huu pia atakuja na maneno na njia ya kuhakikisha mambo yanabaki kama yatakavyo amuliwa na tume za uchaguzi
 
Naona CDM wanajaribu kutumia ubavu wa Maalim kujitutumua, si CDM mtoe tamko tu nyie si ndio chama kikuu cha upinzani, kwa nini mnahangaika kusubiri tamko la Maalim Seif ?

Ndiyo mnavyojidanya? Kwa taarifa yenu CDM na ACT lao moja.

Zenu si huwa kurukia mambo here and there?

Hamkuwahi kusema Maalim mtu wenu? Mara Membe mtu wenu? Hamkuwahi kusema Zitto mtu wenu? Mara Mbowe mtu wenu?

Si muda mrefu mtasema na Lissu mtu wenu?

Subirini dawa ichemke mlikuwa mmezoea. Safari hii hatudanganyiki!

Uchaguzi huru na wa haki. Vinginevyo ICC itawahusu watu fulani safari hii.
 
Kwa bahati mbaya hakuna chochote cha ajabu kitakachotokea hata baada ya ZEC na NEC kupitisha panga na mahali pengine wakiendelea kuchelewesha majibu ya rufaa za wagombea zaidi ya kauli za kila siku za "sasa basi na tuwe na subira"

Maalim Seif amekua ni shock absorber wa hali ya kisiasa ya Zanzibar tangia yale mauwaji ya 2001 akizuia watu kuchukua hatua maana ataleta maafa na umwagaji damu. Kwavyovyote vile na mwaka huu pia atakuja na maneno na njia ya kuhakikisha mambo yanabaki kama yatakavyo amuliwa na tume za uchaguzi

Mkapa (rip) hayupo. Ni mmoja wa watu walioonya kiaina kabla kifo chake.

Hilo hata jiwe analijua.

Mdanganyeni huyo ngosha. Kenya ICC haikuwahusu maafisa vipenyo bali Uhuru na Ruto - yale mapapa!

Wajiandae ki saikolojia.

Za Mwizii 40. Ya forty ni hii. Jaribuni tena kukwiba muone.
 
Mkapa (rip) hayupo. Ni mmoja wa watu walioonya kiaina kabla kifo chake.

Hiyo la jiwe analijua.

Mdanganyeni huyo ngosha. Kenya ICC haikuwahusu maafisa vipenyo bali Uhuru na Ruto - yale mapapai!

Wajiandae ki saikolojia.
Mkuu guts za Wakenya sio za wabongo. Wapemba wanaweza kuonyesha jambo lakini wapo wangapi? Zaidi ya yote kuna watu wanaamini kwamba lama alivyo ZZK, BKM, na wengine kibao pale ACT hata Maalim ni Afisa Kificho/Kipenyo
 
Mkuu guts za Wakenya sio za wabongo. Wapemba wanaweza kuonyesha jambo lakini wapo wangapi? Zaidi ya yote kuna watu wanaamini kwamba lama alivyo ZZK, BKM, na wengine kibao pale ACT hata Maalim ni Afisa Kificho/Kipenyo
Mbaya zaidi CDM ndio wanaongoza kumchafua Zitto kuwa ni wakala wa TISS, leo wanamhitaji, wanahitaji support ya ACT ndio wanamuona ana maana.
 
Mkuu guts za Wakenya sio za wabongo. Wapemba wanaweza kuonyesha jambo lakini wapo wangapi? Zaidi ya yote kuna watu wanaamini kwamba lama alivyo ZZK, BKM, na wengine kibao pale ACT hata Maalim ni Afisa Kificho/Kipenyo

Kwamba ni afisa vipenyo hizo ni nyimbo za maafisa vipenyo ambazo kwa leo hazina wanenguaji.

Nyimbo hizo hazivutii tena. Kwani umesikia nani anatukumbusha tena kuwa Membe, Maalim, Zitto au hata Mbowe eti ni wenzao?

Tuna washauri wamwongeze na Lissu kwenye hiyo list labda itawasaidia. Ila safari hii wanalo.

Kama ni nia yenu kuwatambulisha maafisa vipenyo mbona yule petro katawi hamkuwahi kumtambulisha na hata wa leo?

Kama ni disco basi safari hii kaingia morani!
 
Kwani shida ni nini?
Kwenye siasa hakuna adui wa kudumu wala rafiki wa kudumu.. bali kuna maslahi ya kudumu

Kwao hao jitihada zozote za kuikomboa hii nchi toka kwa mkoloni mweusi ni msiba mkubwa.

Hawa wanaongozwa na njaa zao zaidi kuliko mustakabala sahihi wa nchi.
 
Mbaya zaidi CDM ndio wanaongoza kumchafua Zitto kuwa ni wakala wa TISS, leo wanamhitaji, wanahitaji support ya ACT ndio wanamuona ana maana.

Kwa hiyo unamshauri Zitto asiwasikilize kabisa CDM Ila akusilize wewe?

Haya si ndiyo yale Machozi ya mamba sasa?
 
Kumbuka katika siasa hakuna hasimu wala rafiki wa kudumu, isipokuwa kuna maslahi ya kudumu.

Unadhani hata kuwa hawaelewi basi? Mbona kina mamvi na mzee ziro walipokelewa kwa bashasha? Mbona hata ki-nana, marope na yule wa mtama ilikuwa vile? Kwani lile la washamba nani alitamka?

Kwa kiswahili hao huitwa "wenye kukaanga mbuyu."

Huwa ni wenye kukuaanga mbuyu na kuwaachia wenye meno watafune.

Zama zimeshabadilika mno. Za leo kila mtu na acheze ngoma zake. Ngoma zao hatuna haja nazo, wakae nazo tu.

Wanajaribu kila mbinu mradi kutotenganisha. Ni vyema wakajua kuwa tunawajua vyema.

Hatudanganyiki!
 
Mahakama kusimamisha kesi za Lissu tumeona haki inawezekana. Polisi pia tumeona.

NEC na ZEC mmegusa gusa mzizi wa fitina bado.

Tupeni raha kwa kutupa haki tu wana wa nchi hii.

Hii nchi ni yetu sote.
 
Back
Top Bottom