Tanzania tuna tatizo kubwa sana la watu/taasisi kukaa na kusubiri kila kitu kiletwe kwenye sahani. Tumeona polisi inavyotaka 'muathirika' awe ndio mpelelezi badala ya wao kufanya kazi hiyo, sasa NEC nayo inasubiri iletewe kila kitu. Kama hao wakubwa wamesikia taarifa inayohusu ofisi yao kwenye vyombo vya habari, wameshindwa kitu gani kuwasiliana (kwa barua) na ofisi husika ili wapate barua 'maalum?