G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Taifa langu ni taifa la wanafiki wengi, hawana uzalendo na hawajui wasimame wapi kuutetea uishi na utashi wao.
Ndugu yangu Humphrey Polepole nakuomba ujione wa thamani na kuijenga upya haiba yako mbele ya jamii, mimi huko nyuma nilishakataa kuwa mnafiki nikamueleza mheshimiwa yule kuwa mimi siyo wa aina yake, nikatengua. Mimi ningefarijika sana kama ungejitokeza na kuukataa ukuu wa wilaya kwa kuonyesha dhahiri kuisimamia rasimu uliyopendekeza, hiyo ndiyo siasa safi na kujitambua.
Humphrey Polepole kwa kweli ukienda kuapa tena nitakufutilia mbali kwenye watu wangu wa karibu na sitokupa ushirikiano wowote ndani ya uongozi wako. Nitakuwa mpinzani wako mkubwa na kukupinga kwa kila jambo kiuchumi, kisiasa na kijamii. Nachukia sana undumilakuwili na sitaki kukuona tena kwa mara nyingine ukirudia kosa hilo la undumilakuwili.
Nausubiri kwa hamu kubwa msimamo wako ili nikuheshimu au kukupuuza kama ambavyo nimewapuuza wengine ndani ya chama chako.
Ndoto njema utakayoishi itakufanya kuwa mkuu mbele ya mataifa siku za usoni!
Ndugu yangu Humphrey Polepole nakuomba ujione wa thamani na kuijenga upya haiba yako mbele ya jamii, mimi huko nyuma nilishakataa kuwa mnafiki nikamueleza mheshimiwa yule kuwa mimi siyo wa aina yake, nikatengua. Mimi ningefarijika sana kama ungejitokeza na kuukataa ukuu wa wilaya kwa kuonyesha dhahiri kuisimamia rasimu uliyopendekeza, hiyo ndiyo siasa safi na kujitambua.
Humphrey Polepole kwa kweli ukienda kuapa tena nitakufutilia mbali kwenye watu wangu wa karibu na sitokupa ushirikiano wowote ndani ya uongozi wako. Nitakuwa mpinzani wako mkubwa na kukupinga kwa kila jambo kiuchumi, kisiasa na kijamii. Nachukia sana undumilakuwili na sitaki kukuona tena kwa mara nyingine ukirudia kosa hilo la undumilakuwili.
Nausubiri kwa hamu kubwa msimamo wako ili nikuheshimu au kukupuuza kama ambavyo nimewapuuza wengine ndani ya chama chako.
Ndoto njema utakayoishi itakufanya kuwa mkuu mbele ya mataifa siku za usoni!