Samcezar
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 13,096
- 22,627
Unakuta ukiwa bwana mdogo kipindi bado bikra wa maisha, Wazazi na ndugu wanakuwa na shinikizo la kukukazia utafute maisha kwa ugumu.
Kama ni mzazi utamuomba pesa ya mtaji atakwambia katafute au anzia chini ukue kidogo kidogo ( sio wazazi wote wapo hivi).
Utahitaji pesa za mavazi au mahitaji yako madogo madogo ili uweze kumudu maisha ukiwa bado tegemezi lakini utakuwa unachezea upinzani mkubwa sana ukiambiwa maneno ya kufedhehesha na kukudhaliliisha kwa dharau kuwa wewe ni mzembe na mvivu na goigoi.
Ukienda kukaa kwa ndugu utapata misuko suko ya kukupa joto ya jiwe ili utoke hapo kwao na uache kuwaegemea.
Sawa haya yote ni namna sahihi ya kumkomaza kijana ili aanze kujitegemea na kusimama mwenyewe na kujijenga.
Sasa swali linakuja, mbona huyu kijana akifanikiwa kimaisha na kuanza kujitegemea bila msaada na kuwa vema, ndugu wale wale wanakuwa mstari wa mbele kuomba sapoti mbali mbali za kifedha.
Je, vijana mliofanikiwa na kupitia mazingira ya namna hii, hamuoni kuwa ni wakati muafaka wa kuwahoji hawa ndugu kuwa kwann hawajiwekei akiba ya maisha na uzee ili kuweza kupata uwezo wa kujikimu badala ya kutegemea kusaidiwa na vijana ambao wao waliwapotezea na kuwa wajibisha kipindi wakiwa wadogo na hawajui lolote kuhusu maisha.
I mean si tulikubaliana kuwa maisha ni kupambana na kujikaza kiume na kutopenda kubebwa na kusaidiwa kizembe. Sasa mbona kama mnarudia kosa lile lile ambalo tulikubaliana kuwa si sawa kufanya?
Wembe ni ule ule ila upande wa kukata sasa ni tofauti.
Naandika uzi huu baada ya kumpa makavu ndugu yangu ambaye alikuwa akimpa kauli dogo mtoto wa ndugu yake na malkia(mama).
Akimind dogo kuwa katoka mkoa baada ya kumaliza form six halafu anang'aa macho tu hajishughulishi. Me nikamuhoji kuwa wewe umempatia msaada gani alipokwama zaidi ya kusema maneno ya kumuumiza ukiamini unampa nguvu ya kutoka akapambane?!
Why usitumie lugha kurupushi ila ambayo ni rafiki?! Badala ya kumlaumu why usimuongoze na kumuonyesha vya kufanya halafu umfunze kujisimimia. Huyu akitoka kesho na kesho kutwa atakukumbuka kama mentor wake na kiongozi kama utakwenda nae kwa upendo na urafiki.
Ukimlaumu na kumfedhehesha atakukumbuka kama mnyanyasaji na mfedheheshaji wake.
Kama ni mzazi utamuomba pesa ya mtaji atakwambia katafute au anzia chini ukue kidogo kidogo ( sio wazazi wote wapo hivi).
Utahitaji pesa za mavazi au mahitaji yako madogo madogo ili uweze kumudu maisha ukiwa bado tegemezi lakini utakuwa unachezea upinzani mkubwa sana ukiambiwa maneno ya kufedhehesha na kukudhaliliisha kwa dharau kuwa wewe ni mzembe na mvivu na goigoi.
Ukienda kukaa kwa ndugu utapata misuko suko ya kukupa joto ya jiwe ili utoke hapo kwao na uache kuwaegemea.
Sawa haya yote ni namna sahihi ya kumkomaza kijana ili aanze kujitegemea na kusimama mwenyewe na kujijenga.
Sasa swali linakuja, mbona huyu kijana akifanikiwa kimaisha na kuanza kujitegemea bila msaada na kuwa vema, ndugu wale wale wanakuwa mstari wa mbele kuomba sapoti mbali mbali za kifedha.
Je, vijana mliofanikiwa na kupitia mazingira ya namna hii, hamuoni kuwa ni wakati muafaka wa kuwahoji hawa ndugu kuwa kwann hawajiwekei akiba ya maisha na uzee ili kuweza kupata uwezo wa kujikimu badala ya kutegemea kusaidiwa na vijana ambao wao waliwapotezea na kuwa wajibisha kipindi wakiwa wadogo na hawajui lolote kuhusu maisha.
I mean si tulikubaliana kuwa maisha ni kupambana na kujikaza kiume na kutopenda kubebwa na kusaidiwa kizembe. Sasa mbona kama mnarudia kosa lile lile ambalo tulikubaliana kuwa si sawa kufanya?
Wembe ni ule ule ila upande wa kukata sasa ni tofauti.
Naandika uzi huu baada ya kumpa makavu ndugu yangu ambaye alikuwa akimpa kauli dogo mtoto wa ndugu yake na malkia(mama).
Akimind dogo kuwa katoka mkoa baada ya kumaliza form six halafu anang'aa macho tu hajishughulishi. Me nikamuhoji kuwa wewe umempatia msaada gani alipokwama zaidi ya kusema maneno ya kumuumiza ukiamini unampa nguvu ya kutoka akapambane?!
Why usitumie lugha kurupushi ila ambayo ni rafiki?! Badala ya kumlaumu why usimuongoze na kumuonyesha vya kufanya halafu umfunze kujisimimia. Huyu akitoka kesho na kesho kutwa atakukumbuka kama mentor wake na kiongozi kama utakwenda nae kwa upendo na urafiki.
Ukimlaumu na kumfedhehesha atakukumbuka kama mnyanyasaji na mfedheheshaji wake.