Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA), Yosepher Komba amelalamika kudhalilishwa wakati Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Jackline Msongozi akitoa ushauri kuwa Msajili wa Vyama aingilie kati CHADEMA kutokana na tuhuma zinazotolewa juu ya chama hicho ikiwemo za Wabunge kukatwa fedha na baadhi ya Wabunge Wanawake kulalamika kudhalilisha Kingono
Wakati Msongozi anaongea, Komba aliomba kutoa taarifa na alipopewa nafasi alisema “Anachokifanya Mbunge Jackline ni kuzidi kuwadhalilisha Wanawake na nimuombe awashauri hao wanaolalamika waende kwenye Vyombo vya Dola”
Spika Ndugai alipokea na kusema “Ndicho anachokifanya. Hivyo kaa chini tuweze kumsikiliza.” Na kisha kumuambia Mbunge Jackline achukue ushauri huo aliopewa
Hata hivyo, Mbunge Jackline alijibu na kusema “Huyu anayeongea (Yosepher) pia aliwahi kunifuata, kama dada yake maana naye anatoka Ruvuma na akaniambia naye ana tatizo hilo hilo. Hivyo Spika, naomba nikuambie katika hilo wenzetu wamekuwa wakiteseka sana”
Wakati Mbunge Jackline akiendelea kutoa hoja yake Mbunge Yosepher aliwasha kipaza sauti na kuanza kuomba utaratibu huku akisema hayupo tayari kudhalilishwa. Spika Ndugai alimtaka kukaa chini na kumuambia asiongee kwani hajaruhusiwa kusema na anafanya fujo
Baada ya kuambiwa hivyo, Yosepha aliwasha kipaza sauti na kusema atashughulika na Mbunge Jackline nje ya Bunge. Spika Ndugai alisema "Umewasha kipaza sauti na kila ukielekezwa husikii, naomba kwa usalama na amani utupishe."
Aidha,Mbunge Jackline alimalizia kusema chama kama hivyo (CHADEMA) vinabidi vifute kwani mbaya zaidi Mwenyekiti wa CHADEMA amefanya vitu vya hovyo kabisa. Amesema "Ameenda kustarehe halafu anasema amepigwa na watu gani? Sisi tunaishi pale Medeli tumemsikia kabisa akienda kwa nyumba ndogo yake"
Wakati Msongozi anaongea, Komba aliomba kutoa taarifa na alipopewa nafasi alisema “Anachokifanya Mbunge Jackline ni kuzidi kuwadhalilisha Wanawake na nimuombe awashauri hao wanaolalamika waende kwenye Vyombo vya Dola”
Spika Ndugai alipokea na kusema “Ndicho anachokifanya. Hivyo kaa chini tuweze kumsikiliza.” Na kisha kumuambia Mbunge Jackline achukue ushauri huo aliopewa
Hata hivyo, Mbunge Jackline alijibu na kusema “Huyu anayeongea (Yosepher) pia aliwahi kunifuata, kama dada yake maana naye anatoka Ruvuma na akaniambia naye ana tatizo hilo hilo. Hivyo Spika, naomba nikuambie katika hilo wenzetu wamekuwa wakiteseka sana”
Wakati Mbunge Jackline akiendelea kutoa hoja yake Mbunge Yosepher aliwasha kipaza sauti na kuanza kuomba utaratibu huku akisema hayupo tayari kudhalilishwa. Spika Ndugai alimtaka kukaa chini na kumuambia asiongee kwani hajaruhusiwa kusema na anafanya fujo
Baada ya kuambiwa hivyo, Yosepha aliwasha kipaza sauti na kusema atashughulika na Mbunge Jackline nje ya Bunge. Spika Ndugai alisema "Umewasha kipaza sauti na kila ukielekezwa husikii, naomba kwa usalama na amani utupishe."
Aidha,Mbunge Jackline alimalizia kusema chama kama hivyo (CHADEMA) vinabidi vifute kwani mbaya zaidi Mwenyekiti wa CHADEMA amefanya vitu vya hovyo kabisa. Amesema "Ameenda kustarehe halafu anasema amepigwa na watu gani? Sisi tunaishi pale Medeli tumemsikia kabisa akienda kwa nyumba ndogo yake"