Ndolanga achezea kichapo msikitini

Ndolanga achezea kichapo msikitini

Status
Not open for further replies.
Hivi huyu mzee hivi bado anayo ile Benzi yake macho ya panzi.. nakumbuka alikwa ana parking maalumu pale maktaba bill ikafika milioni wacha akunje ngumi kukataa kulipa...
 
Jambo la msingi hapa ni kuwa hii taasis haijui ilitendalo, kama kweli ndolanga alikuwa/ni mjumbe wa baraza la wadhamini wa msikiti akifanya jambo lisilotakiwa anatakiwa ashitakiwe katika vyombo husika na kwa kufuata taratibu/katiba/ miongozo ya baraza la wadhamini. Nilitegemea kusikia ameshitakiwa BAKWATA ama BAMITA ama kwenye shura ya Maimam au taasis yoyote ya kiislam, inashangaza kuwa wanamvua nguo mwislam mwenzao tena msikitini kisha wanampeleka polisi au hawa polisi ni taasis ya kulinda maimum?!, hawajifunzi kwa wakatolik ambao hushitakiana ndani ya vyombo vya kanisa na hukumu zinaheshimika?. OK, labda angekuwepo KADHi wangeshitakia huko na si kupigana ngumi na kisha kupelekana kwa Afande Mwema.
Hivi kama sehemu ya ibada ambako Mungu wanaamini yupo wanakosa uvumilivu sasa huku nje itakuwaje kama si watatuchoma moto kabisa. Dini nyingine ni za Lucifer kabisa, hata kama alikosea si kumpiga ila ni kufuata taratibu za msikiti.
 
Jambo la msingi hapa ni kuwa hii taasis haijui ilitendalo, kama kweli ndolanga alikuwa/ni mjumbe wa baraza la wadhamini wa msikiti akifanya jambo lisilotakiwa anatakiwa ashitakiwe katika vyombo husika na kwa kufuata taratibu/katiba/ miongozo ya baraza la wadhamini. Nilitegemea kusikia ameshitakiwa BAKWATA ama BAMITA ama kwenye shura ya Maimam au taasis yoyote ya kiislam, inashangaza kuwa wanamvua nguo mwislam mwenzao tena msikitini kisha wanampeleka polisi au hawa polisi ni taasis ya kulinda maimum?!.
You have hit the nail on the head!
 
Anataka kuleta mambo ya utapeli ya FAT Msikitini kachezea kichapo
 
Jambo la msingi hapa ni kuwa hii taasis haijui ilitendalo, kama kweli ndolanga alikuwa/ni mjumbe wa baraza la wadhamini wa msikiti akifanya jambo lisilotakiwa anatakiwa ashitakiwe katika vyombo husika na kwa kufuata taratibu/katiba/ miongozo ya baraza la wadhamini. Nilitegemea kusikia ameshitakiwa BAKWATA ama BAMITA ama kwenye shura ya Maimam au taasis yoyote ya kiislam, inashangaza kuwa wanamvua nguo mwislam mwenzao tena msikitini kisha wanampeleka polisi au hawa polisi ni taasis ya kulinda maimum?!, hawajifunzi kwa wakatolik ambao hushitakiana ndani ya vyombo vya kanisa na hukumu zinaheshimika?. OK, labda angekuwepo KADHi wangeshitakia huko na si kupigana ngumi na kisha kupelekana kwa Afande Mwema.

Wewe kaa kimya una huwezo wa kuwashauri Waislam eti wajifunze kwa wakatoliki, nyie wenyewe mmeshindwa kuwashtaki Mapadre kwa kuwafanyia unyama vijana wa kiume.

Wewe mambo sio yako unaleta porojo, kamshauri Papa huko Vatican amrudishe yule Padre mwenye watoto wawili.
 
Hao waliomtupia kichapo wakae chonjo. Jamaa ana tabia za babaubaya hadi sura wanafanana, lazima atarudi.
 
Ilikuwa ni jana baada ya swala,Ndolanga akachukua mike nakuanza kuwatangazia waumini kuwa kuna mabadilliko ya uwongozi,na kusema kuwa ma imam wasaidizi wawili mikataba yao imekwisha watachaguliwa wangine,ndipo hapo watu wakaanza kuhoji yeye kama nani na katokea wapi wakati wanajua yeye hupenda kuswali msikiti wa manyema......wanajua kilichompekapale ni pesa,ule msikiti na miradi mingi sana na mfadhili mwenye mshiko....ndipo zongo lilipo anza japokuwa Ndolanga alikuwa amekuja na mabaunsa wa nne lakini walishindwa kumsaidia,asichezee makofi,yule mzee alichezea makofi mengi sana kutoka kwa vijana pale,baadaye walipiga tanganyika jeki akiwa pekupeku wakampeleka kituo cha polisi usalama magomeni.......
hiyo tanganyika jeki ni shambulio la aibu maana hata 'nuts' zenyewe zinaweza kupasuka...lakini nyumba ya ibada ni sehemu ya amani...kulikoni?
 
Gama tunajua nyinyi munaambiwa ni wanakondoo mufuate tu bila ya kuhoji.

Si ndiyo mana hamusemi kitu? Ila wenzenu wa Ulaya wameshtuka sasa ndiyo wanaanza kufurukuta.
 
ningeweza ningewapa zawadi maalum waliompa kichapo lol
tamaa zingine bana....lol
 
​mnnh me nkajua kaacha shughuli za utapeli

ankoli ndolanga kapeka karata tatu hadi kwa wazee wa karatee na bora kapigiwa mchangani ingekuwa mtambani sijui tungekuwa tunaongelea mwingine..
 
naombea isje mkaenda nje ya lengo la uzi huu, maana wengine wameshaanza udadisi
 
habari za Ndolanga mbona zilitangazwa sana ikawaje tena akaaminika msikitini? sitaki kuamini au ni udaku huu
 
Yule si alikuwa na a.k.a ya Tyson! Huwezi jua anaweza akawa yeye ndo kawadunda wenzie, maana amewahi kumchapa Matep Quaresi enzi za kuuza vitalu vya uwindaji

Yah! Tyson alikutana na Evander!
 
ALIYEWAHI kuwa mwenyekiti wa Chama cha soka Tanzania (FAT) sasa TFF ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Muhidin Ndolanga jana aliponea kipigo toka kwa wa Waumini wa Msikiti wa Kichangani, Magomeni Mapipa.
Tukio hilo lilitokea mara baada ya kumalizika kwa swala ya Ijumaa ambapo kama si askari wa jeshi la polisi kumuokoa mambo yangekuwa mengine.
Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika toka katika msikiti huo, ni kwamba Ndolanga ambaye ni Mwenyekiti wa bodi ya msikiti huo, alikumbana na maswahibu hayo mara baada ya kusoma taarifa ya kwa ajili ya kuwasilisha maamuzi yaliyofikiwa na Bodi ya Udhamini iliyokutana kujadili mambo mbalimbali ya msikiti huo.
Imeelezwa kwamba kwa takribani miezi miwili viongozi wa msikiti huo wamekuwa kwenye mgogoro mzito ambao umewahi kufika kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kwa usuluhishi bila mafanikio.
Tukio hilo lilitokea katika msikiti huo baada ya kumalizika kwa Swala ya Ijumaa ambapo inadaiwa Ndolanga, alisimama kwa ajili ya kuwasilisha maamuzi yaliyofikiwa na Bodi ya Udhamini iliyokutana kujadili mambo mbalimbali ya msikiti huo.
Imeelezwa kuwa baada ya kuisoma taarifa hiyo, waumini wa msikiti huo, walipinga taarifa hiyo na kudai kuwa ni tofauti na matakwa ya waumini na ndipo waumini hao walipopandwa na jazba na kutaka kumpiga makonde kiongozi huyo.
Hata hivyo Polisi waliwahi kumwondosha na kumkimbiza katika Kituo cha Polisi Magomeni.
SOURCE: Unique Entertainment
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom