ndayilagije
JF-Expert Member
- Nov 7, 2016
- 7,492
- 8,295
Heri ya Noeli waungwana
Nimewiwa kuwakumbusha na hili nalo tunapoelekea kuanza mwaka mpya tulitie moyoni.
Vijana wanazaliwa, wanakua, wanasoma, wanaoana na kujaliwa watoto. Hii inapendeza. Shida yangu ni hao tunaoanzisha nao familia.
Mwanaume ataacha wazazi wake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.
Unapochagua sehemu yako ya kukamilisha mwili(mwenza) ni muhimu kuitazama siyo kesho yako ila keshokutwa yenu itakavyokuwa.
Kuna mengi ya kujiuliza kama kijana.
1. Je nikifukuzwa kazi huu ubavu utabakia?
Je, nikistaafu huu ubavu utaniheshimu?
Je, nikipata ulemavu tutaendelea kuwa pamoja kweli?
Na vipi kama hatutapata watoto tutaendelea kupendana?
2. Hivi tutakapokuwa wazee na watoto kutuacha kama tulivyowaacha wazazi wetu, purukushani za mji zikiwa ngumu kwetu tutaishije na wapi?
3. Vipi kama itatokea mmoja wetu kujikuta ana jukumu la kutunza ndugu/mzazi wake nitakuwa tayari kutoa msaada na kuvumilia?
4. Hivi wazazi wangu walipatia wapi na walikosea wapi?
Kimsingi ndoa inakupa mitihani kila siku na haitoi lecture hata siku moja, wala haisahihishi. Utasahihisha wewe na marks utajipa wewe. Ndiyo maana inahitaji uwe umepevuka ili kuyajua hayo na kuyakabili pia.
Hata hivyo ni muhimu tuoane tu, ila sasa kuishi kwa amani kwenye ndoa hiyo ni habari nyingine.
Ushauri.
Olewa /oa mtu na siyo watu/vitu.
Oa /olewa kwa ajili yako siyo watu wengine.
Chagua wakati sahihi kwako usiruhusu msongo wowote kutoka nje.
Usioe/olewe kama kulipa fadhila, epuka ndoa ya huruma.
Kubali kuwa ulivyo leo sivyo utakavyokuwa miaka 20 ijayo.
Jiandae na Mungu akubariki.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimewiwa kuwakumbusha na hili nalo tunapoelekea kuanza mwaka mpya tulitie moyoni.
Vijana wanazaliwa, wanakua, wanasoma, wanaoana na kujaliwa watoto. Hii inapendeza. Shida yangu ni hao tunaoanzisha nao familia.
Mwanaume ataacha wazazi wake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.
Unapochagua sehemu yako ya kukamilisha mwili(mwenza) ni muhimu kuitazama siyo kesho yako ila keshokutwa yenu itakavyokuwa.
Kuna mengi ya kujiuliza kama kijana.
1. Je nikifukuzwa kazi huu ubavu utabakia?
Je, nikistaafu huu ubavu utaniheshimu?
Je, nikipata ulemavu tutaendelea kuwa pamoja kweli?
Na vipi kama hatutapata watoto tutaendelea kupendana?
2. Hivi tutakapokuwa wazee na watoto kutuacha kama tulivyowaacha wazazi wetu, purukushani za mji zikiwa ngumu kwetu tutaishije na wapi?
3. Vipi kama itatokea mmoja wetu kujikuta ana jukumu la kutunza ndugu/mzazi wake nitakuwa tayari kutoa msaada na kuvumilia?
4. Hivi wazazi wangu walipatia wapi na walikosea wapi?
Kimsingi ndoa inakupa mitihani kila siku na haitoi lecture hata siku moja, wala haisahihishi. Utasahihisha wewe na marks utajipa wewe. Ndiyo maana inahitaji uwe umepevuka ili kuyajua hayo na kuyakabili pia.
Hata hivyo ni muhimu tuoane tu, ila sasa kuishi kwa amani kwenye ndoa hiyo ni habari nyingine.
Ushauri.
Olewa /oa mtu na siyo watu/vitu.
Oa /olewa kwa ajili yako siyo watu wengine.
Chagua wakati sahihi kwako usiruhusu msongo wowote kutoka nje.
Usioe/olewe kama kulipa fadhila, epuka ndoa ya huruma.
Kubali kuwa ulivyo leo sivyo utakavyokuwa miaka 20 ijayo.
Jiandae na Mungu akubariki.
Sent using Jamii Forums mobile app