Ndoa na Ndugu

Ndoa na Ndugu

Ectus

Member
Joined
Jan 19, 2013
Posts
36
Reaction score
9
Hakuna kitu wanandoa wengi tunakosea kama kuchanganya ndoa na ndugu zako. Kwa maana kwamba kuona ndugu zako ni muhimu kuliko mkeo au mumeo. Sio kwamba hawatakiwi kuwa muhimu ila mwenzio wako ni muhimu zaidi maana anakujua vilivyo. Inashangaza kuona mume anapelekeshwa na mawazo ya ndugu au mke kadhalika. Tujifunze wana ndoa kutofautisha hivi vitu.
 
Hakuna kitu wanandoa wengi tunakosea kama kuchanganya ndoa na ndugu zako. Kwa maana kwamba kuona ndugu zako ni muhimu kuliko mkeo au mumeo. Sio kwamba hawatakiwi kuwa muhimu ila mwenzio wako ni muhimu zaidi maana anakujua vilivyo. Inashangaza kuona mume anapelekeshwa na mawazo ya ndugu au mke kadhalika. Tujifunze wana ndoa kutofautisha hivi vitu.

ushamba tu wa watu......
kuna bidada mmoja ye ndo huwa msemaji mkuu kwenye ndoa ya mdogo ake wa kiume!!!!
ooh mkeo mbona hajasoma ooh mkeo ana nini sijui nakereka kama nini nyambaaaffff.
 
huenda wakawa bado hawajapata somo zuri juu ya thamani ya mke. mke ana haki zaidi ya kusikilizwa endapo jambo lake halina ubaya. Tuwe makini juu ya hili vinginevyo tutakuwa tunatwanga maji katika kinu, pia ikumbukwe kuwa kila nayeoa naoa kwa malengo na sio tu ilimradi ajulikane ana mke. hivyo ni vema kuwa makini sana na jambo hili. Ni hayo tu, kweli nakuunga mkono.

Thanks:
Staryte - Home page
 
usiombe kukuta mke au mume asiyena msimamo.....ndugu wataendesha ndoa kwa remote....
 
usiombe kukuta mke au mume asiyena msimamo.....ndugu wataendesha ndoa kwa remote....
Unajua sikuzote mwanaume ndani ni chachu ya maendeleo. Ukigundua tu anamtazamo wa kindugu na kutokusikiliza mawazo ya mke,Mwanamke itabidi ajipange upya katka kuleta maendeleo binafsi. Isije tokea mume kafariki kumbe mali kaandika majina ya ndugu zake na watoto wakawa hawawma kitu.
 
Mke asie na msimamo atanyooshwa na mkewe. Mwanaume asie na msimamo ni kichaka cha miiba. Manake yeye ndo kichwa cha nyumba afu anazungusha kichwa in circles!
Ndugu wana sehemu yao (strong bond built over 30 intimate years, huwezi kuifuta aisee). Lakini kila mmoja apewe sehemu yake na mke nae apate stahili yake. Kama mwanaume wa kweli, atajua kubalance.
usiombe kukuta mke au mume asiyena msimamo.....ndugu wataendesha ndoa kwa remote....
 
Mke asie na msimamo atanyooshwa na mkewe. Mwanaume asie na msimamo ni kichaka cha miiba. Manake yeye ndo kichwa cha nyumba afu anazungusha kichwa in circles!
Ndugu wana sehemu yao (strong bond built over 30 intimate years, huwezi kuifuta aisee). Lakini kila mmoja apewe sehemu yake na mke nae apate stahili yake. Kama mwanaume wa kweli, atajua kubalance.

ni kweli kabisa.....
Ila tatizo wanaume wengi wanaungana na wake zao mwanzoni then wanavutwa masikio na kujiunga na ndugu zao...hapo lazima nyumba igwukw chungu....( hapa sijawainclude mama's boy ambao mkipanga jambo ataenda kwanza kumwambia mama yake...halafu mama mkwe anabadilisha uamuzi unashtukia tu kama mlipanga kununua kiwanja badala ya kiwanja inaletwa harrier)
 
Unajua sikuzote mwanaume ndani ni chachu ya maendeleo. Ukigundua tu anamtazamo wa kindugu na kutokusikiliza mawazo ya mke,Mwanamke itabidi ajipange upya katka kuleta maendeleo binafsi. Isije tokea mume kafariki kumbe mali kaandika majina ya ndugu zake na watoto wakawa hawawma kitu.

kweli aisee nimeshuhudia ndoa imevunjika kisa mume aliandikisha mali tena walizochuma na mkewe dasa zake(alianza na mkewe akiwa na godoro tu) baada ya mke kuamua kuanza kusaka vyake mume akavitolea macho...vyake vya dada yake vya mke navyo viwe vyake..... Miaka 7 sasa wametengana
 
Back
Top Bottom