Nisiwachoshe
Ni miaka miwili toka nioe bint toka Tanga,nilijuana nae nikiwa Mwanza yeye yupo chuo fulani cha ualimu mm nikiwa kwenye shughuli zangu ktk NGO,S moja jijini hapo,
alionesha ni mcha Mungu tulianzisha mahusiano lakini sikua na lengo nae lakini kadri tulivyoendelea na mahusiano alikua ameficha makucha huku akilalamikia wanaume huwa ni waongo mara hapendi kuchezewa basi nikaona ni malaika wa kuishi nae tukaenda kupima nikawa nakula kama kawaida tulipozoeana alianza kubadilika anakua mkali,mtu wa commanding nikajua atajirekebisha akatulia mwaka 2014 tukafunga ndoa hapo ndipo nilipoanza kuona rangi ya huyu binti ana rangi gani,amekua mtu wa kulalamika mlalamishi hata mambo ya kawaida,wivu wa kijinga hata nikiongea na mtu anajudge hata kanisani,katika maisha ya kawaida anapenda kujibizana na mm,akikosea hawezi kuomba msamaha,anapenda kususa hovyo, amekua mtu wa commanding,anachokitaka kifanyike,majibu ya hovyo mbele wa dada wa kazi,tukidiscuss jambo ambalo linatakiwa tufanye maamuz ananiambia wewe si ndio baba fanya utakavyo halaf sasa nikiwasiliana na mzazi wa kike mama akinishauri jambo basi hununa sana na kusema ndoa inaongozwa na mama ,yaani ni mtu wa hasira hasira mda wote mara nikirud kanuna tu,nikiumwa hatilii maanani ,juz nimerud kichwa kinauma nina mawazo mambo yangu ya chuo na mengine anayoniletea yeye akaanza mara mbona nimemkasirikia nikamwambia sijamkasirikia ila nina msongo wa mawazo akasema hawezi kuishi maisha ya hapa mara anahisi nina mwanamke na akasema anaondoka na leo jion kaondoka nimemuuliza dada wa kazi ameniambia amesema anaenda mjini
sasa naombeni ushauri mm huyu nimechoka nimeongea habadiliki kwa chochote anataka kuwa na sauti kunizidi mm,
je niwape taarifa nyumbani kwa huyu bint niwasimulie yote
au niwaambie na nyumbani kwetu habari zake
naombeni ushauri wenu na je kama ameamua kulala nje kuna haja ya kumkaribisha tena kuwa mke?au nikae kimya moja kwa moja au nimpe displine gani itakayo mfanya atambue thamani ya mume tafadhalini ushauri wenu ni muhimu sana
BACKGROUND
Amelelewa katika maisha ambayo hakuoneshwa upendo sana na bibi yake alikua mshirikina na amekua akiwachezea toka mdogo na hata kwenye ufungaji ndoa bibi yule alifanya vimbwanga ili ndoa isifungwe lkn ilishindikana hapo ni sendoff kwanza baadae alifatilia harusi itafungwa wapi akaharibu kumkomoa