Nchimbi asipuuzwe, aungwe mkono

Nchimbi asipuuzwe, aungwe mkono

Mushkov

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2024
Posts
612
Reaction score
1,265
Nadhani kwa situation iliyopo sasa katika Nchi, ni bora zaidi tufuate wosia wa Nchimbi badala ya kumshambulia au kumpuuza.

Wengine wanasema, huyu asituchanganye kwa sababu naye yupo ndani ya mfumo, lakini, Je, shetani akikwambia kuwa, usipite njia hiyo, kuna hatari, na pengine kwa umbali na wewe unaiona hiyo hatari, hutamsikiliza kwa sababu tu yeye ni shetani?

Soma pia Dkt. Nchimbi: Hakuna sheria inayotengua Katiba. Watanzania pambaneni kupata Katiba mpya
 
Tumesikia anachosema, lakini asitegemee trust yetu hata kidogo. Hatumuamini mwanaccm yoyote. Inshort tumeichoka CCM na wanaccm wote. Ifahimike yeye ndio anapaswa kutuunga mkono na sio kinyume chake.
 
MIMI NADHANI TUYAUNGE MKONO HAYA MABUNGE YA WAFU WENYE AKILI TIMAMU.

4. MASHARTI NA MUDA MAALUMU KUTOKA COMMONWEALTH CMAG(The Ultimatum)

Kutokana na mapendekezo ya Mjumbe Maalum, CMAG imetoa maelekezo yenye ukomo wa muda (Time-bound actions) kwa Tanzania:

Ndani ya Siku 30: Kutatua suala la kushikiliwa kwa Tundu Lissu kupitia njia za kisiasa au kisheria, na kuwaachia wengine wote wanaoshikiliwa kwa kutumia haki zao kwa amani.

Ndani ya Siku 60: Kurejesha upatikanaji kamili wa mitandao ya kijamii na kuacha vitisho dhidi ya vyombo vya habari na watetezi wa uhuru wa kujieleza.

Ndani ya Siku 90: Kuitisha jukwaa shirikishi na la kuaminika la vyama vya siasa (likiongozwa na mwezeshaji huru) kujadili mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi, ushindani wa kisiasa, wafungwa, na uwajibikaji.

Bila Kuchelewa: Kuanza uchunguzi huru wa makosa ya jinai uliopendekezwa na Tume ya Uchunguzi, pamoja na fidia kwa wahanga.

MWISHO WA UBAYA NI AIBU.
 
Back
Top Bottom