Nchi yetu ni masikini lakini wa kujitakia. Tuuze gesi jumla tuwagawie wananchi pesa Yao

Major

JF-Expert Member
Dec 20, 2007
1,865
2,439
Kwa hesabu nilizokwisha kuona tena za kitaalamu, ni kwamba Tanzania tuna akiba nyingi sana ya gesi huko mtwara. Kimahesabu ni kwamba tukiamua kumuuzia mtu kwa bei ya jumla, kila raia atapewa mgao wake wa Tsh bilion 1.17.

Sasa kwanini tusiuze ili kila mtanzania awe tajiri? Au, hivi kuwa masikini ni sifa?. Mimi Kama mimi, kwa mfano nikiwa Rais hata sasa hivi, kitu cha kwanza ni kupiga bei hiyo gesi ambayo kwa sasa inaonekana haina kabisa manufaa yoyote kwa mwananchi.

Kila mwananchi namfungulia account na namwingizia pesa yake. Lakini ningewashauri wananchi wangu wafungue fix account ili hizo pesa Mimi Kama serikali nizikopeshe hizi nchi za Africa mashariki na wananchi wangekuwa wanakula RIBA tu. So nchi za Africa mashariki kusingekuwa na haja ya kwenda kupiga magoti world bank.

Ni hesabu rahisi sana. Maana Kama tukisema tuache, kwa huu mfumo uliopo ni kazi bure. Tena Nina imani kila mwanachi Akiwa tajiri basi hata kampeni za kugombea Uraisi kwa kipindi kingine nisingekuwa na haja nazo. Kwa sababu najua kila mwananchi Ana furaha na lazima anipe kura ya ndiyo tu.
 
Back
Top Bottom