Bufa
JF-Expert Member
- Mar 31, 2012
- 13,645
- 28,811
Hangaya anapenda sana kujizunguka na watu wenye elimu za kuunga unga kama yeye. Ukiangalia walioko karibu naye, utajua tu kwamba nchi hii haipo serious hata kidogo.
Mwanasheria Mkuu Hamza Johari, kasoma bachelor's na master's Ukraine huko — hiyo inatosha kukuonyesha kila kitu unachohitaji kujua. Kadhalika hajawahi kuwa wakili nchini ila bado kawa AG.
Gavana wa BOT, Emmanuel Tutuba, kasoma Advance Diploma na MBA Mzumbe. JPM alimpa nafasi ya kuwa RAS Mwanza, halafu Hangaya akamchukua moja kwa moja kutoka uRAS hadi kuwa Gavana wa Benki Kuu. Wakati magavana wa nchi nyingine wanatoka IMF na World Bank, wetu anatoka ofisi ya RAS Mwanza. Ni dhahiri kabisa hapa hatuzingatii vigezo wala hadhi ya nafasi.
Halafu kuna Jenista Mhagama — aliteuliwa kuwa Waziri wa Afya wakati ana stashahada ya ualimu. Wote tunakumbuka aibu aliyoleta UN, alipokuwa amezungukwa na mawaziri wa afya waliobobea kwenye taaluma zao. Ilikuwa fedheha tupu.
Hangaya mwenyewe hana hata rekodi ya elimu inayoeleweka. Ni diploma za kuunga unga tu ambazo hazina uthibitisho wowote. Hii nchi imepoteza mwelekeo kabisa — tumepigwa na kitu kizito chenye ncha kali, na bado tupo tu tumeziba macho.
Sitashangaa Bashite akipewa uwaziri wa fedha au mambo ya nje.
Mwanasheria Mkuu Hamza Johari, kasoma bachelor's na master's Ukraine huko — hiyo inatosha kukuonyesha kila kitu unachohitaji kujua. Kadhalika hajawahi kuwa wakili nchini ila bado kawa AG.
Gavana wa BOT, Emmanuel Tutuba, kasoma Advance Diploma na MBA Mzumbe. JPM alimpa nafasi ya kuwa RAS Mwanza, halafu Hangaya akamchukua moja kwa moja kutoka uRAS hadi kuwa Gavana wa Benki Kuu. Wakati magavana wa nchi nyingine wanatoka IMF na World Bank, wetu anatoka ofisi ya RAS Mwanza. Ni dhahiri kabisa hapa hatuzingatii vigezo wala hadhi ya nafasi.
Halafu kuna Jenista Mhagama — aliteuliwa kuwa Waziri wa Afya wakati ana stashahada ya ualimu. Wote tunakumbuka aibu aliyoleta UN, alipokuwa amezungukwa na mawaziri wa afya waliobobea kwenye taaluma zao. Ilikuwa fedheha tupu.
Hangaya mwenyewe hana hata rekodi ya elimu inayoeleweka. Ni diploma za kuunga unga tu ambazo hazina uthibitisho wowote. Hii nchi imepoteza mwelekeo kabisa — tumepigwa na kitu kizito chenye ncha kali, na bado tupo tu tumeziba macho.
Sitashangaa Bashite akipewa uwaziri wa fedha au mambo ya nje.