nziriye
JF-Expert Member
- Jan 23, 2011
- 1,051
- 361
Nilipozaliwa miaka 47 zama ziiilee ,nilikuwa najivunia kuwa mmoja wa wazaliwa ktk ji-nchi hili ,miaka ya 1985 wakapeana vijiti lol matumaini yakawepo na nikawa sina hofu kutamka mbele ya mataifa kuwa mie ni nchi yenye maziwa na asali,milima na mabonde,rutuba na hali nzuuri ya hewa ,miaka ikaenda akaja mwingne miaka ya 1995 huyu hana tatizo kidogo hali ya kujivuna ikawa ipo kwa mbaaali kama mie ni wahapahapa ....miaka ya 2000 akaja handsome boy,mpenda kiduku,smilling face,kijana flani looh nilitoa sauti ya KASI ZAIDI,NGUVU ZAIDI NA HALI ZAIDI .....,hatukuelewa na sisi tukawa MAZUZU,VIONGOZI NAO WAKAWA MAZUZU ,NCHI IKAWA YA KIZUZU..,.maisha yakawa ya kizuzu,umeme wa kizuzu,mabomu yanalipuka kizuzu wanatoa sababu ya kizuzu ...haya kituko zaidi akaja bwana mmiliki wa dowans nae wa kizuzu wakaenda wahariri nao mazuzu wakashindwa kumkaba wakamwacha zuzu kaenda zake huku akijiona kuwa yupo juu amewaweza mazuzu...nadhani uwepo wa chama makini kama cdm ndo tiba ya mazuzu na viongozi mazuzu,wapendwa wanajf shime tuwe pamoja kunusuru nchi yetu ,nahakika miaka ikifika itakuwa poa,umoja ni nguvu na mwenye macho haambiwi tazama.