Nchi kubwa zinajiendesha vizuri zaidi kwa utawala wa Kimajimbo. Tuzingatie hili kwenye katiba mpya

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,599
46,244
USA, Canada, Russia, Brazili, China, Australia, India, Argentina ambazo ni nchi kubwa zaidi duniani na zilizopiga hatua kubwa za maendeleo zote zinatumia mfumo wa utawala wa majimbo kujiendesha.

Ni vigumu sana kwa nchi kubwa kama Tanzania kuweza kupata maendeleo ya haraka kwa mfumo wa uongozi centralised sana/ unitary kama tulio nao sasa. Sababu ni nyingi ikwemo

Hakuna uharaka wa kufanya maamuzi, maendeleo yanayahitaji uharaka kuamua mambo. Mfumo tulio nao sasa hautoi fursa hiyo. Jambo dogo linalopaswa kufanyiwa uamuzi ndani ya wiki moja linaweza hata kuchukua zaidi mwaka kwa sababu ya mlolongo mrefu wa uamuzi. Tumeshudia baadhi ya mambo yakisubiria hadi Rais afike mahali kuyatolea uamuzi. DEDs, RCs na DCs wanasubiria mambo yaamuliwe wizarani au na Rais au kusoma upepo ndipo watakeleze. Kwa nchi kubwa hivi tutuchakua hata miaka 200 ili kuleta maendeleo kwa mfumo huu

Vipaumbele tofauti vya maeneo na jamii tofauti za watu, kuna kanda au mikoa kipaumbele chao kikubwa ni miondombinu ya biashara, wengine ni kilimo, wengine ufugaji, wengine uvuvi n.k Kipaumbele ni muhimu sana kwenye jamii. Ukifanya mradi wa kujenga shule nchi nzima wakati kuna maeneo wanazo shule za kutosha na walihitaji barabara unakuwa umepoteza rasilimali tu, ukijenga uwanja wa ndege mahali watu wanahitaji kwanza maji masafi ya bomba unakuwa unatapanya rasilimali adimu tu. Hili ni tatizo kubwa sana kwenye unitary states ambazo ni kubwa.

Usimamizi dhaifu wa rasilimali, Mfumo wa unitary unazifanya rasilimali nyingi kuwa kama hazina mwenyewe japo zinasemwa ni za wote.Umilikaji wa rasilimali ni jambo muhimu sana katika kuzithamini, kuzitunza na kuzitumia kwa usahihi. Msitu unaosimiwa na jimbo utakuwa na uangalizi mzuri zaidi kuliko serikali central, watu wanaouuzunguka wataelewa huo msitu ni maisha yao na watoto hivyo wakiuharibu wao ndio watakuwa wachuma janga wa kwanza, vivyo hivyo kwa maziwa katika uvuvi, ardhi n.k

Muono tofauti wa mambo mengi ya kijamii.
Kuna jamii ziko conservative sana na zinataka kubaki na mtindo wake wa maisha wa muda mrefu, mila na tamaduni zake, nyingine ziko conservative kidogo na hazioni shida kuachana na mila na tamaduni zake nyingi. Unaweza kukuta waziri au mamlaka inajikita katika kutafuta vazi la taifa na kuna watu wanapenda hivyo ila wengine wao wanataka kuvaa suti au kanzu tu sasa hapo kunakuwa na mpishano mkubwa sana amabao ungeepukika kwa watu kufanya mambo kimajimbo.

Udhaifu katika uwajibikaji wa viongozi na kuwatuza viongozi. Udhaifu mkubwa wa mfumo centralised/unitary ni ugumu wa kumwajibisha kiongozi moja kwa moja. Leo hii mkuu wa mkoa au wilaya akiharibu lawama kubwa anatupiwa Rais au waziri, pia anaweza kuondolewa au asiondolewe. Pia mkuu wa mkoa,.wilaya au DED anayefanya vizuri anaweza kuondolewa kirahisi na wakati wowote. Katika mfumo wa utawala wa majimbo hayo mambo yanawekwa vizuri kwa sababu wananchi wenyewe ndio wanaamua nani anafaa kubaki, kuingia au kutoka.

Katiba mpya bila mfumo wa majimbo itakuwa sawa na kupata nusu mkate tu.
 
Vipaumbele tofauti vya maeneo na jamii tofauti za watu, kuna kanda au mikoa kipaumbele chao kikubwa ni miondombinu ya biashara, wengine ni kilimo, wengine ufugaji, wengine uvuvi n.k Kipaumbele ni muhimu sana kwenye jamii. Ukifanya mradi wa kujenga shule nchi nzima wakati kuna maeneo wanazo shule za kutosha na walihitaji barabara unakuwa umepoteza rasilimali tu, ukijenga uwanja wa ndege mahali watu wanahitaji kwanza maji masafi ya bomba unakuwa unatapanya rasilimali adimu tu. Hili ni tatizo kubwa sana kwenye unitary states ambazo ni kubwa.
Umetoa uzi bora kabisa kwa mwaka huu wa fedha.
 
Jamaa wanaogopa utawala wa majimbo kwa kudhani utaleta upendeleo/kuyatenga baadhi ya maeneo, wanaona uwepo wa hiyo system ya utawala utaifanya sehemu moja ya taifa ijione iko juu zaidi ya nyingine kimaendeleo.

Wanaogopa kwa mfano, vipi yale maeneo ambayo hayana rasilimali nyingi, wao mapato yao ya kuendeleza maeneo yao watayapata wapi?

Ukiangalia kwa hii nchi yetu kwa mfano, kuna maeneo kuna uchimbwaji wa madini na shughuli za kiuchumi na kibiashara zimechangamka zaidi, hii itasaidia kukuza pato la halmashauri/jiji kwenye kuendeleza eneo husika.

Lakini maeneo mengine hali yao ni tofauti, mapato yao ni madogo, asilimia kubwa wanategemea mazao ya kilimo ambacho hutegemea na soko la dunia likoje, soko likiwa baya, na hali ya kipato itayumba.
 
Mikoa gani miwili au mitatu Tanzania ambayo tunaweza sema ina rasilimali chache sana?
Jamaa wanaogopa utawala wa majimbo kwa kudhani utaleta upendeleo/kuyatenga baadhi ya maeneo, wanaona uwepo wa hiyo system ya utawala utaifanya sehemu moja ya taifa ijione iko juu zaidi ya nyingine kimaendeleo.

Wanaogopa kwa mfano, vipi yale maeneo ambayo hayana rasilimali nyingi, wao mapato yao ya kuendeleza maeneo yao watayapata wapi?

Ukiangalia kwa hii nchi yetu kwa mfano, kuna maeneo kuna uchimbwaji wa madini na shughuli za kiuchumi na kibiashara zimechangamka zaidi, hii itasaidia kukuza pato la halmashauri/jiji kwenye kuendeleza eneo husika.

Lakini maeneo mengine hali yao ni tofauti, mapato yao ni madogo, asilimia kubwa wanategemea mazao ya kilimo ambacho hutegemea na soko la dunia likoje, soko likiwa baya, na hali ya kipato itayumba.

Uzuri wa mfumo wa majimbo utakuja kuwaamsha watendaji, ufuatiliaji wa shughuli za kila siku utakuwa wa karibu zaidi na wa haraka zaidi, itakuwa rahisi kuwashughulikia wabadhirifu na kuelekeza pesa kwenye maendeleo ya eneo husika.
 
Mikoa gani miwili au mitatu Tanzania ambayo tunaweza sema ina rasilimali chache sana?
Hiyo ni theory inayoletwa na wasioutaka mfumo wa majimbo, na hizo ni miongoni mwa sababu wanazozitaja, nyingine ikiwemo sababu za kiusalama.

Mfano, hayo majimbo hayatakuwa na majeshi yake? viongozi wa hayo majeshi watatoka wapi? hawatakuwa na uungwaji mkono na vikosi vya maeneo yao mwishowe waje kujitenga na kujitangazia jamhuri zao?

Hayo ni baadhi ya mambo ambayo kwa namna moja au nyingine yanakwamisha uwepo wa serikali za majimbo kwenye nchi yetu, na sishani hata kama watauweka kwenye Katiba Mpya.
 
Mtoa hoja umeelezea Safi kabisa ila mifano ungetoa hata mmoja wa hapa hapa Africa, SA ina serikali za majimbo, ANC inatawala majimbo 8 n DA wana jimbo moja, kimaendeleo jimbo la DA lipo Safi mno na hawa so called black diamonds wanaiba kwenye majimbo yao na kwenda kujenga kwenye jimbo la DA(official opposition party),metro nyingi zipo chini ya serikali za metro chini ya DA, came 2024 ANC wana mlima mkali wa kupanda, watch the space...ccm bila dola ni wepesi kama karatasi
 
Ni theory mfu, kwa sababu hakuna mkoa Tanzania ambao hauna kitega uchumi kikubwa. Mikoa pia yenye vitega uchumi vikubwa zaidi kushinda mingine bado inaitegemea mikoa yenye vitega uchumi vichache kwa miondombinu. Chukulia DRCongo nchi yenye rasilimali nyingi zaidi barani Africa inavyotegemea Tanzania na Kenya kwenye bandari.
Hiyo ni theory inayoletwa na wasioutaka mfumo wa majimbo, na hizo ni miongoni mwa sababu wanazozitaja, nyingine ikiwemo sababu za kiusalama.

Mfano, hayo majimbo hayatakuwa na majeshi yake? viongozi wa hayo majeshi watatoka wapi? hawatakuwa na uungwaji mkono na vikosi vya maeneo yao mwishowe waje kujitenga na kujitangazia jamhuri zao?

Hayo ni baadhi ya mambo ambayo kwa namna moja au nyingine yanakwamisha uwepo wa serikali za majimbo kwenye nchi yetu, na sishani hata kama watauweka kwenye Katiba Mpya.
 
Hiyo ni theory inayoletwa na wasioutaka mfumo wa majimbo, na hizo ni miongoni mwa sababu wanazozitaja, nyingine ikiwemo sababu za kiusalama.

Mfano, hayo majimbo hayatakuwa na majeshi yake? viongozi wa hayo majeshi watatoka wapi? hawatakuwa na uungwaji mkono na vikosi vya maeneo yao mwishowe waje kujitenga na kujitangazia jamhuri zao?

Hayo ni baadhi ya mambo ambayo kwa namna moja au nyingine yanakwamisha uwepo wa serikali za majimbo kwenye nchi yetu, na sishani hata kama watauweka kwenye Katiba Mpya.
Nchi zote zenye mfumo wa majimbo nilizokutajia, majeshi yamebaki chini ya serikali kuu na mkuu wa majeshi ni Rais au Waziri Mkuu. Polisi na mgambo ndio wanakuwa chini ya gavana au mkuu wa jimbo.
 
Ni theory mfu, kwa sababu hakuna mkoa Tanzania ambao hauna kitega uchumi kikubwa. Mikoa pia yenye vitega uchumi vikubwa zaidi kushinda mingine bado inaitegemea mikoa yenye vitega uchumi vichache kwa miondombinu. Chukulia DRCongo nchi yenye rasilimali nyingi zaidi barani Africa inavyotegemea Tanzania na Kenya kwenye bandari.
Hapo uliposema; "Mikoa yenye vitega uchumi vikubwa inaitegemea mikoa yenye vitega uchumi vichache kwa maendeleo" sijakuelewa kabisa. Bahati mbaya mfano ulioenda kuutoa umeutoa nchi ya nje - DRC.

Ningependa ulete mfano kutokea humu Tanzania kwetu, ni mikoa gani midogo kiuchumi inayoinufaisha mikubwa kiuchumi?
 
Mtaongea sana ila jibu rahisi ni kuwa SERA YA MAJIMBO kwa sasa msahau maana itakuwa ni anguko la CCM, huu mfumo wa sasa unaipa nguvu CCM kwasababu kila kitu kipo chini ya RIMOTI moja tu...

Tukishakuwa na MAJIMBO ina maana nguvu ya kisiasa itahamia kwa WATU BINAFSI badala ya CHAMA, na wao CCM wanachotaka ni ku-control kila kitu kinachoendelea kwenye hili TAIFA ili waendelee kuneemeka na KOO zao.

Mfano leo kukiwa na KANDA ina maana kuna maamuzi yataishia huko huko bila kushirikisha SERIKALI KUU, sasa hawa jamaa kule juu wao si watakuwa wanaelea tu kimaamuzi.

Hata CCM wenyewe wanajua kuwa KUONGOZA HII NCHI KUPITIA MAJIMBO ndo njia rahisi ya kuharakisha MAENDELEO lakini wao KIPAUMBELE siyo maendeleo ya WATANZANIA bali ni WATAENDELEAJE KUKAA PALE JUU kuendelea kushikilia njia zote za hii NCHI.
 
Labda tugawe kwa Kanda
Kuna mikoa mingine itaumia ila tukiiweka kwenye kanda itabebwa

Dar ijitegemee

Pwani, Morogoro, Kusini

Kanda ya Kati

Kanda ya Kaskazini

Kanda ya Ziwa

Nyanda za Juu Kusini

Kanda ya Ziwa Tanganyika
 
Back
Top Bottom