Emanuel Gabriel
Member
- Feb 7, 2013
- 16
- 5
OMBWE
Tuzimulike asasi, za umma na binafsi,
Malengo yake asisi, tuanze kuyaasesi,
Hasa wetu maafisi, muhimu tuwadadisi,
Ombwe linaoneka, wakuliziba ni sisi
Akali tunaiona, kwenye zetu taasisi,
Kwenye viti wametuna, hasa waziba nafasi,
Wengi waliojazana, wanatia wasiwasi,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Ukiwachunguza sana, hukikosi cha kuhisi,
Jinsi wanavyokazana, kwa malengo binafsi,
Vya umma kuvigawana, ajenda kutufirisi,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Rajua wengi hawana, wamekosa akhlasi,
Huduma bora hakuna, japo kila mtu bosi,
Ule ubwana utwana, pia unashika kasi,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Siyo siri tumekwama, weledi una nakisi,
Nchi inarudi nyuma, kwa kukosa ufanisi,
Nisemayo si shutuma, bali ni halihalisi,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Wanazichota mapema, kisha wanatudhiaki,
Maisha kama kiama, wongo umetamalaki,
Kila kona ni dhuruma, maskini hana haki,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Migogoro chungu nzima, siku moja haipiti,
Wafugaji wakulima, machweo ni hatihati,
Wale tuliowatuma, wamekosa mikakati,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Tuna mali nchi nzima, faida hatuipati,
Zatitirika hujama, wachache wanadhibiti,
Tumebakizwa yatima, kundi limetusaliti,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Kila mtu ameona, mengi yenye ukakasi,
Ni bora tukaungana, wenye nchi ndio sisi,
Yote yanawezekana, tuamkeni upesi,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Emanuel. G. Someke
0753191035
Tuzimulike asasi, za umma na binafsi,
Malengo yake asisi, tuanze kuyaasesi,
Hasa wetu maafisi, muhimu tuwadadisi,
Ombwe linaoneka, wakuliziba ni sisi
Akali tunaiona, kwenye zetu taasisi,
Kwenye viti wametuna, hasa waziba nafasi,
Wengi waliojazana, wanatia wasiwasi,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Ukiwachunguza sana, hukikosi cha kuhisi,
Jinsi wanavyokazana, kwa malengo binafsi,
Vya umma kuvigawana, ajenda kutufirisi,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Rajua wengi hawana, wamekosa akhlasi,
Huduma bora hakuna, japo kila mtu bosi,
Ule ubwana utwana, pia unashika kasi,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Siyo siri tumekwama, weledi una nakisi,
Nchi inarudi nyuma, kwa kukosa ufanisi,
Nisemayo si shutuma, bali ni halihalisi,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Wanazichota mapema, kisha wanatudhiaki,
Maisha kama kiama, wongo umetamalaki,
Kila kona ni dhuruma, maskini hana haki,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Migogoro chungu nzima, siku moja haipiti,
Wafugaji wakulima, machweo ni hatihati,
Wale tuliowatuma, wamekosa mikakati,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Tuna mali nchi nzima, faida hatuipati,
Zatitirika hujama, wachache wanadhibiti,
Tumebakizwa yatima, kundi limetusaliti,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Kila mtu ameona, mengi yenye ukakasi,
Ni bora tukaungana, wenye nchi ndio sisi,
Yote yanawezekana, tuamkeni upesi,
Ombwe linaonekana, wakuliziba ni sisi
Emanuel. G. Someke
0753191035