Ryaro wa Ryaro
JF-Expert Member
- Oct 4, 2010
- 2,659
- 1,422
Kwa mwelekeo huu wa nchi kuwa gizani na bila kuwa na uhakika wa lini patakucha ni bora tuigawe nchi maana watawala wetu wamekosa maono na kubakia watumwa wa Posho na Rushwa.Nashauri tuanze na kanda ya Ziwa na nchi hii tuipe jina The Republic of Lake Victoria.(Mwanza, Mara, Kagera , Shinyanga, Kilimanjaro , Arusha na Manyara). Tukiamua tunawaza mbona GoSS ( Sudan ya Kusini) wameweza na kwa nini tuendelee kuteseka kwa sababu ya viongozi wanaoshindwa kuchukua maamuzi mazito na magumu ya kuinusuru nchi na Mufilisi.