Naziona dalili za Rais Magufuli kuwa mzito kuwachukulia hatua wateule wake

Salary Slip

Platinum Member
Apr 3, 2012
49,325
152,136
Naanza kuyakubali maneno ya Waziri mmoja mstaafu kuwa Magufuli anawasimamisha kazi maofisa wa serikali kwa tuhuma mbalimbali kwasababu hakuwateua yeye hivyo inakuwa rahisi kuwatimua.

Kwa mtazamo wangu,Waziri huyu mstaafu bila shaka alimanisha kuwa atakaowateua yeye mwenyewe itakuwa vigumu kuwawajibisha kirahisi kama anavyofanya kwa hawa aliowakuta maofisini.

Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa hali hii imeshaanza kujitokeza kwani mpaka leo hii teyari kuna wateule wake kadhaa teyari wametuhumiwa kwa mambo kadhaa lakini ni wazi kuna kigugumizi cha wao kuchukuliwa hatua.

Kwa mfano,kuna waziri mmoja ametuhumiwa kutumia madaraka yake vibaya mwaka jana mwezi wa 9 katika sakata la kuagiza mafuta kutoka nje ya nchi wakati huo akiwa waziri chini ya Kikwete ila mpaka sasa anapeta.

Waziri mwingine alituhumiwa kuvujisha siri kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo kabla ya Ziara ya Waziri Mkuu jambo ambalo ni kinyume na maadili ya uongozi ila naona nae amepeta!

Waziri fulani kijana kutoka Tanga nae alipata tuhuma ikimuhusisha yeye na dada yake kumtapeli fedha raia wa nchi fulani kashifa ambayo ilizua mijadala mitandaoni lakini akaishia kukanusha na sasa kimya!

Kuna mwingine anatuhumiwa kuteua raia wa Uganda na kumpa ulaji katika Taasisi fulani ya umma huyu nae sijui maamuzi yake yalikuwa sahihi au laa mimi sijui ila naona nae anapeta tu!

Hivi sasa kuna mjadala unaendelea kuhusu mteule wake mwingine aliekuwa CEO katika Taasisi moja kubwa tu ambapo Taasisi hiyo inatuhumiwa kwa ufisadi wa mabilioni ya shilingi ila naona mpaka sasa hakuna kinachoendelea huku mteule huyo akisubiri mahali atapopangiwa.

Naamini kadri siku zinavyosonga mbele orodha inaweza kuongezeka na hivyo Waziri yule mstaafu akawa sahihi kabisa.

Tukumbuke hawa wanaowajibishwa hutakiwa kukaa pembeni mara moja kupisha uchunguzi wa tuhuma juu yao sasa sijui labda hawa wengine tuhuma zao ni story tu za mtaani mimi sielewi!!
 
Hivi nyie mmeishiwa hoja!!?
Mara mlalamike anapo chukua hatua
Mara mseme hachukui hatua

Kama siasa zimewashinda mfanye kazi zingine.
Upinzani sio kupinga hata visivyo kuwapo
Nimiezi 5 Magu akiwa kazi ni
Ulitaka afanyeje kwa kipindi kifupi kama hicho!!
 
Hivi nyie mmeishiwa hoja!!?
Mara mlalamike anapo chukua hatua
Mara mseme hachukui hatua

Kama siasa zimewashinda mfanye kazi zingine.
Upinzani sio kupinga hata vivyo kuwapo
Nimiezi 5 Magu akiwa kazi ni
Ulitaka afanyeje kwa kipindi kifupi kama hicho!!
Kumbuka hayo maneno yalikuwa ni ya waziri kutoka chama chenu.
 
Hivi nyie mmeishiwa hoja!!?
Mara mlalamike anapo chukua hatua
Mara mseme hachukui hatua

Kama siasa zimewashinda mfanye kazi zingine.
Upinzani sio kupinga hata visivyo kuwapo
Nimiezi 5 Magu akiwa kazi ni
Ulitaka afanyeje kwa kipindi kifupi kama hicho!!

Mkuu hoja ya salary slp inamashiko sana...tumia busara kujadili.. Siyo kukurupukia upizani... Ivi hata unajua kua bila upizani imara hata magufuli leo hii asingekua rais...... Jitahidi kupanua akili yako aiseh
 
Mkuu hoja ya salary slp inamashiko sana...tumia busara kujadili.. Siyo kukurupukia upizani... Ivi hata unajua kua bila upizani imara hata magufuli leo hii asingekua rais...... Jitahidi kupanua akili yako aiseh
Sasa kuna upinzani imara upi Tanzania!!?
Kama sio upinzani unao lindwa na Vilaza Nyumbu
 
Kwani inachukua siku ngapi kwa mtu kuwajibishwa? Wengine unesema ni tuhuma kama kwa huyo unayesema anatoka Tanga, unaweza tusaidia ni mamlaka gani imethibitisha huo udalali wake au unataka Rais achukue hatua kwa taarifa za humu jf?
 
Mi nadhani anajaribu kuwa na busara pia katika kasi yake. Kwa mfano hapo umetaja mawaziri 4, sasa jiulize angekuwa amewang'oa mawaziri hao wanne kwa kipindi hiki kifupi je ingekuwa sahihi au ndio mgesema zaidi?
 
Natafakari na kupiga picha mbele mkuu atakapokabidhiwa uenyekiti wa Chama. Sijui utumbuaji utaendelea ama itakuwaje. Sipati picha!
 
Hivi hujamjua maghu kwa kupenda sifa anapoona camera, yule mkuu wa bandari waliyemsimamisha kwa upotevu wa makontena karudi kazini kimya kimya bila waandishi wa habari kuitwa
 
Naanza kuyakubali maneno ya Waziri mmoja mstaafu kuwa Magufuli anawasimamisha kazi maofisa wa serikali kwa tuhuma mbalimbali kwasababu hakuwateua yeye hivyo inakuwa rahisi kuwatimua.

Kwa mtazamo wangu,Waziri huyu mstaafu bila shaka alimanisha kuwa atakaowateua yeye mwenyewe itakuwa vigumu kuwawajibisha kirahisi kama anavyofanya kwa hawa aliowakuta maofisini.

Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa hali hii imeshaanza kujitokeza kwani mpaka leo hii teyari kuna wateule wake kadhaa teyari wametuhumiwa kwa mambo kadhaa lakini ni wazi kuna kigugumizi cha wao kuchukuliwa hatua.

Kwa mfano,kuna waziri mmoja ametuhumiwa kutumia madaraka yake vibaya mwaka jana mwezi wa 9 katika sakata la kuagiza mafuta kutoka nje ya nchi wakati huo akiwa waziri chini ya Kikwete ila mpaka sasa anapeta.

Waziri mwingine alituhumiwa kuvujisha siri kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo kabla ya Ziara ya Waziri Mkuu jambo ambalo ni kinyume na maadili ya uongozi ila naona nae amepeta!

Waziri fulani kijana kutoka Tanga nae alipata tuhuma ikimuhusisha yeye na dada yake kumtapeli fedha raia wa nchi fulani kashifa ambayo ilizua mijadala mitandaoni lakini akaishia kukanusha na sasa kimya!

Kuna mwingine anatuhumiwa kuteua raia wa Uganda na kumpa ulaji katika Taasisi fulani ya umma huyu nae sijui maamuzi yake yalikuwa sahihi au laa mimi sijui ila naona nae anapeta tu!

Hivi sasa kuna mjadala unaendelea kuhusu mteule wake mwingine aliekuwa CEO katika Taasisi moja kubwa tu ambapo Taasisi hiyo inatuhumiwa kwa ufisadi wa mabilioni ya shilingi ila naona mpaka sasa hakuna kinachoendelea huku mteule huyo akisubiri mahali atapopangiwa.

Naamini kadri siku zinavyosonga mbele orodha inaweza kuongezeka na hivyo Waziri yule mstaafu akawa sahihi kabisa.

Tukumbuke hawa wanaowajibishwa hutakiwa kukaa pembeni mara moja kupisha uchunguzi wa tuhuma juu yao sasa sijui labda hawa wengine tuhuma zao ni story tu za mtaani mimi sielewi!!
Namashaka, kama hii sio ajira yako basi familia yako itaathirika kiuchumi.
Ungetoa tuhuma makini hatua zingechukuliwa. Sasa mtu kuwa na dada mlaghai aachishwe kazi kwa lipi? Hata kama unalipwa na kutumia hii pesa kulisha familia jua zitakuathiri. Sidhani kama Mungu anabariki mambo haya.
 
Back
Top Bottom