Nawezaje kuwa stable hapa

Nawezaje kuwa stable hapa

Captain mopao

Senior Member
Joined
Feb 25, 2021
Posts
133
Reaction score
384
Habar zenu waadau.

Naomba niende directly, kuna mahali flan mkoa wa manyara hua nafanya kilimo, katika halakat zangu za kilimo nikaona niwe napeleka na biashara ya nguo.

Nikanunua robota moja la suruali za kiume nikapeleka na biashara ikawa nzuri tu.

Nikawa nazunguka na kwenye magulio ya vijiji vya jirani kiukweli biashara sio mbaya ukanda huu .

Kuna lafiki yangu mmoja akanishauri kwamba nifungue saloon.

Maana eneo hilo kuna uhitaji wa saloon na zilizopo hazikidhi viwango kias kwamba watu wenye hadhi husafili umbali mrefu kwenda kutafta saloon zenye hadhi hasa walimu watendaji wafanyakaz wa zahanati.

Nikaufanyia kazi ushauri nikaludi home nikajipanga nikanunua sofa kali mziki mnene mashine na kila kitu.

Nikapata flame nzuri kbsaa yenye hadhi nikaanza kutafuta kinyozi.

Kuna jamaa akasema yupo kijana ambae yeye hua ananyoa kwa kutumia wembe anakubalika kijiji chote hivo nimtafute.

Nikamtafuta na nikamwambia nataka awe ananilipa kwa week, ijapokua sikua nimepanga ni kiwango gan kwa sababu sikua nimejua mzunguko wa biashara.

Tukakubaliana tukae week moja wote tuone ratio yake.

Lakini akaniambia kua bado anavuna mazao yake kwa hio akimaliza ataanza rasmi lakini atakua anakuja siku anauokua free nikamkubalia.

Kiukweli baada ya kufungua saloon yangu nilifanya saloon nyingine wafunge na wengine kuhama kijiji.

Watu wote waliiipenda saloon yangu kwa jinsi nilivoipangalia.

Shida ikaanza kwa huyu kinyozi wangu amemaliza kuvuna lakini haishiwi visingizio kila leo atasema kaenda msibani kesho atasema ni zamu yake kuchunga kesho kutwa atasema mtoto kaumwa kampeleka hospital.

Yaani kwa week anaweza kuja siku tatu au nne, ipo hivi hulka ya hiki kijiji vijana wakiwa na mahindi ndani kazi hawafanyi kabisaaa

Nimewekeza nusu ya mtaji wangu wa nguo hapo nikitegemea utarudi kichwa kinawaza mpk sijui nifanyeje

Na kupata kijana mwingine ni ishu sana kias kwamba kuna dogo hua namtafuta akae huyu kinyozi akiwa hayupo , lakini wateja wakija wanasema kama muhusika hayupo hawanyoi na kuondoka

Kuna muda anaweza akaja kazini akafunga ukimuuliza kaenda kuangalia mechi mara kaludi nyumbani kula

Wadau Hapa nipo dilema nini nifanye
 
Habar zenu waadau
Naomba niende directly, kuna mahali flan mkoa wa manyara hua nafanya kilimo, katika halakat zangu za kilimo nikaona niwe napeleka na biashara ya nguo

Nikanunua robota moja la suruali za kiume nikapeleka na biashara ikawa nzuri tu

Nikawa nazunguka na kwenye magulio ya vijiji vya jiran kiukweli biashara sio mbaya ukanda huu

Kuna lafiki yangu mmoja akanishauri kwamba nifungue saloon

Maana eneo hilo kuna uhitaji wa saloon na zilizopo hazikidhi viwango kias kwamba watu wenye hadhi husafili umbali mrefu kwenda kutafta saloon zenye hadhi hasa walimu watendaji wafanyakaz wa zahanati

Nikaufanyia kazi ushauri nikaludi home nikajipanga nikanunua sofa kali mziki mnene mashine na kila kitu

Nikapata flame nzuri kbsaa yenye hadhi nikaanza kutafuta kinyozi

Kuna jamaa akasema yupo kijana ambae yeye hua ananyoa kwa kutumia wembe anakubalika kijiji chote hivo nimtafute

Nikamtafuta na nikamwambia nataka awe ananilipa kwa week, ijapokua sikua nimepanga ni kiwango gan kwa sababu sikua nimejua mzunguko wa biashara

Tukakubaliana tukae week moja wote tuone ratio yake,

Lakini akaniambia kua bado anavuna mazao yake kwa hio akimaliza ataanza rasmi lakini atakua anakuja siku anauokua free nikamkubalia

Kiukweli baada ya kufungua saloon yangu nilifanya saloon nyingine wafunge na wengine kuhama kijiji

Watu wote waliiipenda saloon yangu kwa jinsi nilivoipangalia

Shida ikaanza kwa huyu kinyozi wangu amemaliza kuvuna lakini haishiwi visingizio kila leo atasema kaenda msibani kesho atasema ni zamu yake kuchunga kesho kutwa atasema mtoto kaumwa kampeleka hospital

Yaani kwa week anaweza kuja siku tatu au nne, ipo ivi hulka ya hiki kijiji vijana wakiwa na mahindi ndani kazi hawafanyi kabisaaa

Nimewekeza nusu ya mtaji wangu wa nguo hapo nikitegemea utaludi,
kichwa kinawaza mpk sijui nifanyeje

Na kupata kijana mwingine ni ishu sana kias kwamba kuna dogo hua namtafuta akae huyu kinyozi akiwa hayupo , lakini wateja wakija wanasema kama muhusika hayupo hawanyoi na kuondoka

Kuna muda anaweza akaja kazini akafunga ukimuuliza kaenda kuangalia mechi mara kaludi nyumbani kula

Wadau Hapa nipo dilema nini nifanye
Katafute kama kijana toka mjini,mpe somo la kuwa msafi,muongeaji vizuri na wateja,mpangie chumba,huyo hatakimbia na wala hatakuwa na visingizio,maana ni mgeni huko.Kazi iendeleee.
 
Back
Top Bottom