Nawasihi ACT Zanzibar, hawajachelewa kujinasua na kabali ya ZZK!

Nawasihi ACT Zanzibar, hawajachelewa kujinasua na kabali ya ZZK!

Mikopo Consultant

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2024
Posts
2,235
Reaction score
4,382
Kufanya kosa sio kosa, ila endapo ukiendelea kukosea baada ya kulitambua kosa lako la awali, hapo yafaa kabisa wewe kuwekwa kwenye kundi la wapumbavu!

Ujumbe huo uwaendee ACT Zanzibar; waliojitumbukiza kwenye chama la wana, wakakutana na kabali ya mwana - ZZK! Mwana ambaye huu mwaka wa 10 sasa ametumia nguvu ya ACT Zanzibar kama dhamana ya kujitengenezea nafasi ya kuibagaza demokrasia kotekote - Bara na Visiwani.

Kwasisi tuliosoma harakati za Maalim Seif Sharif Hamad na namna alivyokuwa anapambania haki kwenye ardhi ya wazanzibari, Zanzibari ambayo ilikuwa, na bado inayo, mgawanyiko mkubwa kwenye jamii yake kati ya Waafrika, Washiraz, Waarab, Wahindi, na Wacomoro; ni wazi, muunganiko wa ZZK na ACT Zanzibar, haujazaa tija ya kupambana na matatizo lukuki kwenye jamii ya wazanzibari, ikiwemo kuzisikiliza sauti za wazanzibari zilizojificha.

Kulingana na aina ya demokrasia ya chama cha ACT Wazalendo, kuna hatari ya kuwafanya ACT Zanzibar kama tawi la CCM huko Zanzibar, ikikinzana kabisa na historia ya mapambano ya haki na demokrasia yaliyopambaniwa kwa jasho na damu na Maalim Seif Sharif Hamad

Kwa mwenendo wa sasa, kuna hatari ya kutozisikia sauti za wazanzibari wanaopigania haki na uhuru wa kidemokrasia.

Ikiwa ACT Zanzibar wanataka kurejesha mapambano ya kweli ya haki, hawana budi kujinasua kwanza kwenye mikono ya vibaraka wa CCM; hawana budi ya kung'oka kwenye kabali ya ZZK!

Walifikirie na hili!
MC
 
Hata baba levo aambiwe na watu wake wa karibu kua bungeni haendi pale kawekwa kama chambo tu.
Lile jimbo ni la Zitto iwe kwa kura halal au vinginevyo.
Namuona baba levo ashaanza kijiaminisha kua kigoma mjini ni yake.
Ushaur asijetumia hela zake kizembe aende kwa step kubwa sana lile jimbo ni la kimkakati sana.
 
Mkiambiwa Zitto Kabwe ni dalali wa CCM muwe mnaelewa
Wanapaswa kuona hii drama ya Luhaga Mpina, inaonekana kabisa ni planned move. Ni tukio lingine linalopaswa kuwapa ishara ya kujinasua, na kwamba wanatumika kama dhamana ya kupiga madili.
 
Zitto kaua kabisa harakati za siasa Zanzibar. Tena wamempa uwenyekiti mwanaccm OMO.
Kwa sasa ni kama jamii ya Zanzibari haina shida yeyote na wanaishi kwa raha mstarehe; siamini hivo kwa 100% japo kuna neema fulani lakini siamini kabisa kwamba wazanzibari hawana madukuduku
 
Hata baba levo aambiwe na watu wake wa karibu kua bungeni haendi pale kawekwa kama chambo tu.
Lile jimbo ni la Zitto iwe kwa kura halal au vinginevyo.
Namuona baba levo ashaanza kijiaminisha kua kigoma mjini ni yake.
Ushaur asijetumia hela zake kizembe aende kwa step kubwa sana lile jimbo ni la kimkakati sana.
Nina hisia kama hizo pia, ila gia inaweza kubadilika angani ikiwa mambo kwa ground yatabadilika sana.

Kuna viashiria vikubwa vya Baba Levo kupata uungwaji mkono; hii inaweza kuleta sintofahamu ikiwa ZZK atakuwa kiuhalisia hajashawishi watu halafu atake mbeleko ya kupewa jimbo.. Itakuwa mtiti
 
Kwa sasa ni kama jamii ya Zanzibari haina shida yeyote na wanaishi kwa raha mstarehe; siamini hivo kwa 100% japo kuna neema fulani lakini siamini kabisa kwamba wazanzibari hawana madukuduku
zanzibar kwa sasa tumestarehe.lam kila kona na flei over nayo inakamilika hapa kwerekwe. halikadhalika kwa sisi wakaaz wa shamba bus no 346 kituo kwa sio zari lami yetu mpaka makunduchi via kizimkaz mkeka tu twateleza. tobo la pili hapa sema tu sisi kinamama wa beshara ndogondgo mgambo hapa darajan hawana utu wanachkua samak
 
Kufanya kosa sio kosa, ila endapo ukiendelea kukosea baada ya kulitambua kosa lako la awali, hapo yafaa kabisa wewe kuwekwa kwenye kundi la wapumbavu!

Ujumbe huo uwaendee ACT Zanzibar; waliojitumbukiza kwenye chama la wana, wakakutana na kabali ya mwana - ZZK! Mwana ambaye huu mwaka wa 10 sasa ametumia nguvu ya ACT Zanzibar kama dhamana ya kujitengenezea nafasi ya kuibagaza demokrasia kotekote - Bara na Visiwani.

Kwasisi tuliosoma harakati za Maalim Seif Sharif Hamad na namna alivyokuwa anapambania haki kwenye ardhi ya wazanzibari, Zanzibari ambayo ilikuwa, na bado inayo, mgawanyiko mkubwa kwenye jamii yake kati ya Waafrika, Washiraz, Waarab, Wahindi, na Wacomoro.

Ni wazi, muunganiko wa ZZK na ACT Zanzibar, haujazaa tija ya kupambana na matatizo lukuki kwenye jamii ya wazanzibari. Kulingana na aina ya demokrasia ya chama cha ACT Wazalendo, kuna hatari ya kuwafanya ACT Zanzibar kama tawi la CCM huko Zanzibar, ikikinzana kabisa na historia ya mapambano ya haki na demokrasia yaliyopambaniwa kwa jasho na damu na Maalim Seif Sharif Hamad

Kwa mwenendo wa sasa, kuna hatari ya kutozisikia sauti za wazanzibari wanaopigania haki na uhuru wa kidemokrasia.

Ikiwa ACT Zanzibar wanataka kurejesha mapambano ya kweli ya haki, hawana budi kujinasua kwanza kwenye mikono ya vibaraka wa CCM; hawana budi ya kung'oka kwenye kabali ya ZZK!

Walifikirie na hili!
MC
Japo haujaeleza ubaya wa Zitto kwenye uzi huu
 
Maalim Seif alijichanganya sana kuungana na huyu dalali

Wasipounda serikari ya Mseto tena nadhani wazanzibar watatafuta wataunda chama chao
 
Back
Top Bottom