Nawahabarisha mambo kadhaa...

Hongera sana mwanakijiji na wote ambao mmekuwa mkichangia mada mbalimbali. Huu ni mwanzo tu, lazima kieleweke.
 
Heshima mbele Mwanakijiji.
Tutakuunga mkono, pamoja na ugeni wetu hapa kijijini. Endelea kukamua.
 
Hi Mwanakijiji,

I am very new to the JF, but I am getting more and more excited.

Ninafuatilia kila siku habari hapa JF na kweli watanzania sasa tume-advance.

Napenda nikupongeze na kukushukuru kwa kazi nzito unayofanya, and of course support will come just a matter of time.

Can't wait to hearing the Mwalimu Nyerere 'hotuba' and the sunday session as well


Good Luck.
 
Kati ya mambo ambayo nilikuwa nafuatilia ni la msiba wa vijana wetu hawa. Naomba niweke habari ambazo zimetolewa leo bungeni:

‘Waliohusishwa kuwaua Watanzania wamehojiwa’
Mwandishi wetu
HabariLeo; Saturday,November 03, 2007 @00:06

SERIKALI imesema kuwa watuhumiwa mbalimbali waliohusishwa na kuuawa kwa Watanzania, Walter Mazula na Vonetha Nkya nchini Marekani mwaka jana, wameshahojiwa kuhusiana na mauaji hayo.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Seif Ally Iddi alisema kuwa licha ya watuhumiwa kadhaa kuhojiwa bado hakuna mtu aliyekwishakamatwa au kufikishwa mahakamani kwa kuhusika na mauaji hayo.

“Uchunguzi bado unaendelea…Idara ya Upelelezi wa kesi za mauaji ya Detroit, imeeleza ugumu wa kuelezea kwa kina ni hatua gani haswa waliyofikia kwa sasa kwani hali hiyo inaweza kuvuruga uchunguzi wao,” alisema.

Hata hivyo alisema Idara hiyo ya Upelelezi imeahidi kutoa taarifa ya jumla ambayo itagusia hatua iliyokwishafikiwa katika uchunguzi wao.

Hadi sasa serikali kupitia ubalozi wake wa Washington DC imekuwa ikiendelea kuwasiliana na maofisa wa Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Mauaji huko Detroit kwa ajili ya kupata maendeleo ya uchunguzi wa vifo hivyo.

Septemba 22 mwaka jana Mazula na Nkya waliuawa na watu wasiofahamika wakiwa huko Detroit, Michigan nchini Marekani.

Balozi Seif Ally Iddi alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Mfenesini, Mossy Suleiman Mussa (CCM), aliyetaka kufahamu kwa namna gani serikali imefuatilia suala hilo.
 
🙏🙏🙏
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…