Nauza nyumba Kigoma

Nauza nyumba Kigoma

Mheshimiwa Rais, nimefurahishwa vilivyo na jinsi ulivyoanza uongozi wako wa awamu ya nne kwa ziara za kushtukiza unazozifanya sehemu mbalimbali ambazo unahisi kuna matatizo yanayowaelemea wananchi. Kwa jambo hilo nakupa hongera sana. Wasiwasi wangu ni kwamba, je,baada ya ziara kama hizo ufumbuzi wa matatizo uliyoyaona utapatikana kwa wakati wake? Mfano; Muhimbili wagonjwa kulala chini, mpaka leo hatujasikia hatua zilizochukuliwa. Je, Vitanda vitapatikana lini? Umeme bei juu lini utapunguzwa? Au ni kutokana na hii hali ya ukame…labda! Na kule kwenda sokoni na kuona bei ya vyakula kuwa juu, je kwa kauli yako wafanya biashara wamefanya lolote kupunguza bei? Mheshimiwa nafikiri wakati umefika wa kuwatumia wasaidizi wako wafanye kwanza utafiti wa kina wa matatizo ya sehemu unazoziona zina shida, ili unapotembelea sehemu hizo utoe hitimisho na kauli zilizofanyiwa utafiti wa kina. Kwa bahati mbaya Mheshimiwa rais nchi yetu ina matatizo mengi sana kila nyanja, nachelea kusema kwamba sehemu ambazo utakuwa hujatembelea wajanja watatumia kigezo hicho kwamba hawajaonekana hivyo kuzidi kutunyanyasa. Pia kama ziara hazitakuwa na ukali wa utekelezaji, basi wataona ni kawaida ya rais kututembelea na kuongea...!
Kuna jambo lingine tena Mtukufu Rais ambalo ni muhimu kwako kuliangalia, UWAJIBIKAJI WA PAMOJA (total responsibility). Serikali yako bado ni changa sana madarakakani hivyo inahitaji mawasilianao ya karibu sana katika utendaji wake ili kuimarisha msingi wa mtandao wa utekelezaji wa yale manayoyakusudia. Kitendo cha hivi karibuni cha wewe kwenda kutembelea daraja la muda bila kuwepo kwa mhusika yeyote wa ngazi za juu katika wizara inayohusika, ni cha kushangaza na kuacha maswali mengi nyuma.
Yako mengi sana Mheshimiwa yanayonipa mashaka na maswali mengi kichwani kama kauli zinazopingana kuhusu wafanyabiasha wadogo (wamachinga), Namna zoezi la ukamataji wa wafanyabiashara wanaohusishwa na ujambazi unavyofanyika na hatima yake….ni megi, mengi…nitarudi tena mhesimiwa rais.

ngatuni.

Nop!! Mimi nafanya kazi kigoma kwenye ishu za wakimbizi kwa sasa nakaa Nolad.
 
Wewe kweli ni mwenyeji,, barabara ipo na inapitika siku 365/6, nilikuwa na kigari mfano wa vits na kalikuwa kanapanda tu bila shida.

Kiwanja ninacho pia, maeneo ya juu ya Kigoma secondary, ni Low density pia kiko mlimani. ukinipa 10 mil nakuachia.
basi kwa hapo mambo mazuri nyumba nzuri.
Unajua mji mwema ni sawa na Oysterbay kwa hadhi ya Dar.
Vipi hicho kiwanja cha mji Juu ya Kigoma Seco kinaangalia Ziwa au?Maana nilikuwa napenda Maeneo ambayo unapata view ya Ziwa kama hapo kwako.
Mungu akipenda nataka baada ya miaka miwili nijenge huko,unajua mie mwenyeji na mzaliwa wa huko.Nilisomea pale Kigoma Primary jirani na shule ya kiezya kisha nikaingia Kigoma Secondary mwaka 1994 ambapo Zito Kabwe alikuwa Kaka mkuu.Then nikaanza kukatambuga kama swala pala kutafuta maisha.

Kigoma mji mzuri sana ila pesa ngum kupita maelezo,Kuna ndugu yangu alikuwa na nyumba tatu mji mwema zote UN wamezikodi yeye yupo Dar anakula bata,yaani pesa nzuri sana.
 
Kiwanja chako kina hati na kimehakikiwa na watu wa Ardhi?? Kuna jamaa yangu aliwahi kuuziwa kiwanja fake na wale madalali njaa wa Ujiji
 
Kiwanja chako kina hati na kimehakikiwa na watu wa Ardhi?? Kuna jamaa yangu aliwahi kuuziwa kiwanja fake na wale madalali njaa wa Ujiji

Kina haki mkuu, mimi sio dalali na kiukweli sipendi kuwahusisha madalali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom