Kaka, nimevutiwa na tangazo lako, sio kwa sababu mimi ni mnunuzi, la hasha, bali kwa kuwa niko katika maandalizi ya kulima mpunga.
Hongera kwa kulima na kufanikiwa kupata mchele mwingi.
Hata hivyo ningekushauri katika Tangazo lako uongeze taarifa zifuatazo: Mahali mchele ulipo, namna ambayo wateja watarajiwa (seriuos prospective buyers only) wanaweza ona sampuli ya mchele wako, kiasi gani cha mchele, kwa kilo, unacho, bei elekezi kwa kilo na mchele wako ni aina gani hasa ukizingatia kuwa Shule wanazingatia zaidi uwezo wa mchele kuvimba ukipikwa zaidi ya harufu.
Ninakutakia mafanikio mema!