Hujazuiwa kununua toka japan.
Ukienda Yard za magari utakuta hiyo inaenda kwa 11m au 12m.
From Japan kwa $2800 (CIF) Gx 100 (2000) labda iwe na zaidi ya 150,000km.
Unazungumzia mil 8; vipi kuhusu risk ya kutapeliwa, muda wa kusubiri je? Hivi ndo unasema waTz tume "elimika"????
Waache wenye pesa zao wanunue mashine hiyo.
Haaaaaaaa Realman unanichekesha sana tena sana,ngoja nikufafanulie
1.Gari unaouziwa wewe kwenye yard imezidi kuanzia mil1.5-3m,kama ni mil 11mil mpaka 13m basi ujue wao wameleta kwa mil8 hadi 9mil,sasa kwa nini ninunue gari limetumika bongo miaka miwili tena kwa bei zaidi ya bei ambayo mimi ningeagiza kutoka japan?
2.Kwa taarifa yako ukinipa gari zote za aina moja iliyotumika bongo na ina km15,000 na iliyotumika japan ina km 160,000 nachagua ya japan yenye km nyingi,mie gari nayotembelea niliagiza japani na ilikua na km 130,000 lakin ni mpya sana condition nzuri sana,za bongo si ndo hizo zinazopita bara bara ya mtogole?
3.Dunia ni kijiji,siwezi kuruhusu uwaibie watu kwa kuweka bei ya juu,bora tuwaelimishe hela ngumu sana hauwezi mtapeli mtu wakati ma GT tupo tunashuudia,nasisitiza bei hyo ni kubwa sanaaaa labda kwa mil5 reasonable
Risk ya kutapelia:
Utanunuaje gari japan kichwa kichwa tu? Kuna watz wengi tunawajua wapo jpn kwhy nitaagiza kwa kumtumia huyo mtu na mie ndo nilivyofanya pili kama haumjui mtu unaweza tumia paytrade(tradecarview) na pia kuhusu risk hata bongo kuna risk ya kuibiwa vile vile
Mda wa kusubiri ni siku 21-24 hadi bongo na wiki moja tu mpaka unaiclear,so waiting time ni mwezi m1 so waitin time sio issue kwani umewezaje kusubiri kuchanga hela zaidi ya miaka ndo ushindwe kusubiri mwezi?
So hoja zote hazina mashiko