Nauza gari Tsh 7m

Nauza gari Tsh 7m

Speedo

Member
Joined
Feb 15, 2011
Posts
70
Reaction score
19
Ni Toyota Cresta; 1997 model; 1998cc; AT; 99850km (10 July 2012); lipo katika hali nzuri; lipo Dar es Salaam; linauzwa wakati wowote na unanunua na kuendelea kulitumia wakati huo huo kwani halina tatizo lolote. Insurance Comprehensive; Valid Road License etc etc etc.
Bei Tsh 7m.
Call: 0685386608
 

Attachments

  • Cresta1.jpg
    Cresta1.jpg
    146.4 KB · Views: 240
  • Cresta2.jpg
    Cresta2.jpg
    129.5 KB · Views: 221
  • Cresta inside.jpg
    Cresta inside.jpg
    218.6 KB · Views: 181
safi sana bei iko reasonable. Kuna watu watakuja hapa kuuliza eti kwa nini unauza.
 
Kwa dunia ya leo GX100 tena kavu ni ndoa ya maisha!!!mkataba.......napita watakuja!!wapenzi wa speed!!
 
Kwa dunia ya leo GX100 tena kavu ni ndoa ya maisha!!!mkataba.......napita watakuja!!wapenzi wa speed!!
.

KakaKiiza;
Kwa uzoefu mdogo nilionao, mara nyingi vinavyodumu huwa havinunuliwi mara kwa mara (mzunguko mdogo).
Kwa uzoefu wa miaka sita sasa nimetumia CRESTA GX100; 1997 Model kama hiyo inayouzwa. Sijawahi kupata tatizo kubwa la kiufundi zaidi ya service, kubadili tyres, bulbs (taa) za mbele na moja ya nyuma. hiyo gari nimeiuza mwezi March 2012 kwa shs 6.8m. Aliyenunua yupo hapa hapa mjini DSM na anaitumia vizuri tuuuu.

Kusema kuwa nayo ni kufunga nayo ndoa ya maisha nadhani unaweza kuwa sawa kwa kuwa huna haja ya kuiuza wakati haikusumbui.
Ni gari yenye nguvu,
Inahimili mikiki kuliko gari zingine za aina hiyo,
"Engine" yake haitetereshwi na vitu vidogovidogo kama mafuta yaliyo chakachuliwa, etc,
Ukitaka kusafiri nayo ndio utafurahia zaidi - kwa wanao yatumia watakubaliana na mimi --hili dude barabarani linatulia.
Sifa zaidi zipo nadhani ukitafuta utafahamu.

Wanaopenda kununua gari la aina hii wasisite. Hili hapa jamvini sifahamu hali yake, sifa nilizotoa ni za ujumla wa Toyota Cresta GX100 ya mwaka 1997.
Asanteee
 
KASRI umekuwa wa msaada, constructive. Asante
 
Last edited by a moderator:
.

KakaKiiza;
Kwa uzoefu mdogo nilionao, mara nyingi vinavyodumu huwa havinunuliwi mara kwa mara (mzunguko mdogo).
Kwa uzoefu wa miaka sita sasa nimetumia CRESTA GX100; 1997 Model kama hiyo inayouzwa. Sijawahi kupata tatizo kubwa la kiufundi zaidi ya service, kubadili tyres, bulbs (taa) za mbele na moja ya nyuma. hiyo gari nimeiuza mwezi March 2012 kwa shs 6.8m. Aliyenunua yupo hapa hapa mjini DSM na anaitumia vizuri tuuuu.

Kusema kuwa nayo ni kufunga nayo ndoa ya maisha nadhani unaweza kuwa sawa kwa kuwa huna haja ya kuiuza wakati haikusumbui.
Ni gari yenye nguvu,
Inahimili mikiki kuliko gari zingine za aina hiyo,
"Engine" yake haitetereshwi na vitu vidogovidogo kama mafuta yaliyo chakachuliwa, etc,
Ukitaka kusafiri nayo ndio utafurahia zaidi - kwa wanao yatumia watakubaliana na mimi --hili dude barabarani linatulia.
Sifa zaidi zipo nadhani ukitafuta utafahamu.

Wanaopenda kununua gari la aina hii wasisite. Hili hapa jamvini sifahamu hali yake, sifa nilizotoa ni za ujumla wa Toyota Cresta GX100 ya mwaka 1997.
Asanteee
Kwa yote uliyosema mimi naunga mkono 100%......Hii kitu nimekaanayo 2008-2010 Ndiyo maana nimesema naungana na wewe....ila kwa mtu yeyote mwenye kuhitaji akanunue sijamkataza...ila ni mkataba ukiwa nayo kuuza mbinde kwani wengi wanaiogopa kwa kula mafuta asikudanganye mtu ukiwa nayo mtu wakwanza nivizuri au ukawa na VVTi angalau utajikongoja ila kama umehamia bunju kazi posta na wewe siyo mfanyabiashara mkubwa ni dhahiri ujiweke tayari kutembea na kidumu kwenye buti.
 
nimeipenda,tatizo wese....

Tarlisha;
Kizuri kina gharama zake. Ila tusiwatishe ambao hawajawahi kuyatumia haya magari. Tofauti ya matumizi ya mafuta ni ndogo kiasi fulani. Kwa mfani Hii GX100, 6cylinder inakwenda kwa wastani wa kilomita 8-10 kwa lita (mwendo wa kawaida mjini). Spacio/Carina Si/Corona Premio and alike zinakwenda wastani wa kilomita 10-12 kwa lita (naomba kusahihishwa kama nimekosea). Ninalinganisha magari yote yaliyotumika/siyo mapya na yote yawe yanatumika hapa mjini.

Kinachonifanya nisijutie hiyo tofauti ya matumizi ya mafuta ni utofauti wa haya magari. Unapoendesha/endeshwa ndani ya GX100 ni tofauti kabisa na unapokuwa ndani ya hayo magari niliyotaja hapo juu (Magari yote yawe ya mwaka 1999 kurudi nyuma kwenda 1996). Raha ninayoihisi inanifanya nisitamani hizo gari hapo juu (simaanishi kuwa ni mabaya bali natofautisha tu jinsi yalivyo ukiwa ndani). Wanaoyatumia na walisha wahi kutumia hayo mengine wataniunga mkono. Hii ni sawa na unapoendesha magari mengine GX110 +++, Verossa, ..... yanakufanya uhisi kule kwingine ulipoteza muda.

Kwa kusema hayo naamini hata wale wanaotumia magari mengine makubwa (Landcruisers - V8 nk, Harrier 3.0, Hummer, etc) wanajisikia vizuri zaidi kuliko kuwa na haya madogo.

TOFAUTI YA HIZO KILOMITA CHACHE UNAFIDIA NA BURUDANI UNAYOIPATA KWA KUTUMIA/ENDESHA GX100.


Ni mtazamo tuuuuuuuuuuuuu
 
  • Thanks
Reactions: GP
Nimeipenda hiyo Cresta. Will call you
 
Isije kuwa huyu KASRI na Speedo anayeuza gari ni mtu mmoja. Maana naona huyu KASRI anapigia chapuo sana hii GX 100.
 
Back
Top Bottom