Naungama...! Natubu..!

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,411
Reaction score
829,740
Tumeuanza mwaka 2018 masaa machache yaliyopita... Nawiwa kuongea jambo ili nipate wepesi wa nafsi rohoni... Mizigo ya kiroho hutuliwa kwa kunena(kutubu) ama kulia... Mimi sijalia nanena...!!!
Mimi ni mwanadamu na si malaika.. Si mkamilifu nina mapungufu yangu pia... Pamoja na upole na uwezo wa kuhimili hasira lakini kuna nyakati nimejikuta nashindwa kuzuia hasira zangu
Mwaka uliopita kuna watu niliowafanyia ukorofi.. Walinikera na kupitiliza... Nikawafanyia mambo mabaya.. Nikautumia ulimi wangu kuwanenea mabaya nayo yakawadhuru kwa njia moja au nyingine... Kuna baadhi matendo yangu ya ghadhabu yaliwaletea Maumivu mengi.... Nafsi imenituma niseme neno.. Kisha niungame... Nitubu...
Sikupaswa kutenda niliyotenda... Sikupaswa kuuumiza uumbaji usio wangu... Sikutenda kwa fikra za kimungu bali niliongozwa na urari wa kibinadamu kutaka kujionesha kuwa mimi ni zaidi.. Mimi ni kiboko na mimi ni mimi.... Nimeamua kufanya kitubio na sasa niko huru...
Nawe ni mmojawapo uliyetenda kama mimi... Kama ukiongozwa na fikra za tafakuri kuu ungana nami kwenye kitubio hiki kwa mabaya yote uliyowatendea wengine ili uweze kuwa mpya....

TOBA sio udhaifu bali ni alama ya ushindi kujali na kujitambua..... Fanyeni kitubio tuweze kuiponya nchi iliyojaa majeraha kutokana na matendo yetu hasi
 
Sina neno.Natumai umeniongozea sala ya toba.Nami naitika ..."AMEN"...[HASHTAG]#mshanajr[/HASHTAG]
Aaamen barikiwa zaidi.. Na tukapande pando jipya lisilo na mawaa... Tuachane na pando la ubatili lililopita.. Mazao yake yalijaa mbigili na miba za visasi, mateso, majigambo, kejeli, ubabe, vitisho na Matokeo yake tukamwaga damu nyingi isiyo na hatia... Tukaungame na kutubu sasa tutaliponya taifa
 
mkuu naungana nawewe katika hilo jambo jema ambalo linasifa ya kufanywa na WAUNGWANA
wenye kuitambua nguvu ya Mungu
na Utu kwa Binaadamu wenzao

sina budi kutangaza kuwa NATUBU


[HASHTAG]#ATUBU[/HASHTAG]
 
Aaamen barikiwa zaidi... Haki huinua TAIFA... Tuliponye TAIFA kwa kuepusha kuilisha ardhi na kuyanywesha maji damu isiyo na hatia.. Damu ya waliopoteza uhai kwa matendo mabovu ya binadamu... Uumbaji uliopotezwa kwa chuki na visasi. .. Tuliponye TAIFA na laana hii...
 
MKUU KAMA NA WEWE UMEWAHI KUROGA MTU YAN KUTUMIA VIBAYA TAALUMA UTUBU PIA.
[HASHTAG]#Atubu[/HASHTAG]
Nimefanya kitubio kwa matendo yangu yote yaliyomchukiza Mungu wangu... Matendo ambayo sikutenda kwa weledi... Matendo ambayo yaliunajisi uumbaji
 
Mshana umetubu natumai mwenye ujumbe wake ameuona na katubu pia .. heri ya mwaka mpya
 
hivi mkuu mshana ni kweli uliwahi jihusisha na uchawi/ushirikina au ni Story tu xa jf?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…