Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,411
- 829,740
Mimi ni mwanadamu na si malaika.. Si mkamilifu nina mapungufu yangu pia... Pamoja na upole na uwezo wa kuhimili hasira lakini kuna nyakati nimejikuta nashindwa kuzuia hasira zangu
Mwaka uliopita kuna watu niliowafanyia ukorofi.. Walinikera na kupitiliza... Nikawafanyia mambo mabaya.. Nikautumia ulimi wangu kuwanenea mabaya nayo yakawadhuru kwa njia moja au nyingine... Kuna baadhi matendo yangu ya ghadhabu yaliwaletea Maumivu mengi.... Nafsi imenituma niseme neno.. Kisha niungame... Nitubu...
Sikupaswa kutenda niliyotenda... Sikupaswa kuuumiza uumbaji usio wangu... Sikutenda kwa fikra za kimungu bali niliongozwa na urari wa kibinadamu kutaka kujionesha kuwa mimi ni zaidi.. Mimi ni kiboko na mimi ni mimi.... Nimeamua kufanya kitubio na sasa niko huru...
Nawe ni mmojawapo uliyetenda kama mimi... Kama ukiongozwa na fikra za tafakuri kuu ungana nami kwenye kitubio hiki kwa mabaya yote uliyowatendea wengine ili uweze kuwa mpya....
TOBA sio udhaifu bali ni alama ya ushindi kujali na kujitambua..... Fanyeni kitubio tuweze kuiponya nchi iliyojaa majeraha kutokana na matendo yetu hasi