Habari za leo wachambuzi wenzangu, mi napenda kuwauliza swali moja jepesi, hivi wewe unadhani upinzani wa kweli kwa taifa letu kongwe kiumri na changa kimaendeleo ulikuwepo enzi za mwalimu/ kipindi cha mzee wa ruksa/ au mzee Ben au upo kwa mzee wa kasi mpya, nguvu mpya na ari zaidi au upo katika kipindi chake cha pili cha ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi ? Nitafurahi zaidi ikiwa utanifafanulia kwa marefu na mapana. Ni hayo tu kwa leo.