Watanzania wenzangu nimekuwa nikitatizwa na mawazo kila nikisikia kipindi cha matangazo ya kifo kuwa mipango ya mazishi inafanyika BAA FULANI. Natatizwa na moyo wangu hasa nikiangalia jinsi mahusiano ya vitu viwili hivi yalivyo tofauti kabisa.
Nikiiangalia Baa na namna Watanzania tulivyoifanya kuwa ni sehemu ya machafu yote na baadae nikiangalia ile safari ya yule anaeandaliwa kuenda naona kuwa kama yule maiti hatendewi haki. Kupenda kwetu kote kwa mastarehe naamini moyoni kuwa unapofika umauti mambo hayo yote huwa hayana faida kwa maiti bali swala na dua ndio kitu kinachomfaa.
Dini zote hata za kuabudu mizimu inajali safari ya mwisho sasa tunapoamuwa kuijadili na kuitayarisha safari hiyo pahala panapofanyika machafu ndio tunajali safari hiyo? Tukumbuke kuwa Waswahili walisema 'muosha nae huoshwá'na kama tunaamini dini zetu basi na sisi utakapofika wakati wetu safari zetu zitapangwa kwenye vilabu vya pombe, sijui kama safari za namna hiyo zitakuwa za kubarikiwa?
Nikiiangalia Baa na namna Watanzania tulivyoifanya kuwa ni sehemu ya machafu yote na baadae nikiangalia ile safari ya yule anaeandaliwa kuenda naona kuwa kama yule maiti hatendewi haki. Kupenda kwetu kote kwa mastarehe naamini moyoni kuwa unapofika umauti mambo hayo yote huwa hayana faida kwa maiti bali swala na dua ndio kitu kinachomfaa.
Dini zote hata za kuabudu mizimu inajali safari ya mwisho sasa tunapoamuwa kuijadili na kuitayarisha safari hiyo pahala panapofanyika machafu ndio tunajali safari hiyo? Tukumbuke kuwa Waswahili walisema 'muosha nae huoshwá'na kama tunaamini dini zetu basi na sisi utakapofika wakati wetu safari zetu zitapangwa kwenye vilabu vya pombe, sijui kama safari za namna hiyo zitakuwa za kubarikiwa?