Natangaza rasmi kujivua CCM na kuwa mwanachama wa CHADEMA; wewe je?

JATELO1

JF-Expert Member
Oct 31, 2011
1,230
301
WANAJF:
Kwa heshima na taadhima napenda kuutangazia Umma wa Watanzania popote walipo chini ya Jua kwamba nimeamua kwa dhati kabisa bila kushawishiwa na mtu yeyote bali ni kwa msukumo wa Uzalendo na upendo nilionao kwa nchi yangu ya Tanzania, ambayo imekuwa na hali mbaya sana na inazidi kuwa mbaya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kisiasa kila kukicha. Na mbaya zaidi hali ya maisha kwa wananchi walio wengi inazidi kuwa mbaya, kwani gharama ya maisha inazidi kupanda kila sekta.

Nimekuwa mwanachama wa CCM mwaminifu toka nilipozaliwa na sasa yapata miaka 33 na tawi langu ni Ubungo. Mwaka 2005 nikiwa chuoni, nilikuwa kati ya watu waliomfanyia kampeni Rais wangu Kikwete ili kuweza kuwa Rais wa Tz. Kwanza kabisa katika harakati za kupata mgombea wa CCM kule Chimwaga Dodoma, siku hiyo nilishinda kwenye TV nikiomba JK Kikwete ashinde. Na siku hiyo hata vipindi sikuweza kuhudhuria kwasababu ya msisimko niliokuwa nao na kutaka hasa Kikwete aweze kuwa mgombea kwa tiketi ya CCM, na ndivyo ilivyotokea. Hakika nilifurahi sana na mara moja nilianza kuhamasisha vijana wenzangu na hata ndugu zangu vijijini ili kumpigia Kikwete kura. Mwisho wa siku alishinda na hakika ilikuwa furaha yangu kuu sana, LAKINI, LAKINI, LAKINI!!!

Mara tu Rais wangu alipoingia madarakani na nikaanza kupima uwezo wa utendaji wake, teuzi zake ambazo nyingi hazizingatii vigezo bali zimejaa walakini, na mwelekeo wa nchi kiujumla, hakika nilianza kupoteza matumaini na Rais wangu na serikali yake kwa ujumla. Hatahivyo, niliendelea kuwa mwanachama wa CCM mwaminifu nikiwa na matumaini kwamba ipo siku Rais wangu akipata Uzoefu katika ngazi ya Urais, ndipo ataanza kuleta mabadiliko makubwa katika ngazi zote hasa za kiuchumi na maendeleo. Nilitoa kama miaka 3 kwa Rais wangu ili apate Experience, lkn sikuona faida ya huo uzoefu na hata sasa ana uzoefu wa miaka karibia 7 kwenye Urais lkn hakuna faida,na badala yake Tz imefanikiwa kuingia kwenye 3 Bora ya nchi zinazoongoza kwa Ombaomba Duniani,tukiwa na Iraq na Afghanistan.

Nimekuwa nikijiuliza maswali mengi sana kuhusu OMBAOMBA hasa TZ yenye rasilimali lkn sipati majibu, je ni kweli hatuna kabisa watu makini ambao wanaweza kusaidia uchumi wetu kuimarika? Jibu nililo nalo ni kwamba TZ ina watu wazuri sana lkn tatizo liko kwenye mfumo wa taasisi zetu mbalimbali na serikali yetu kiujumla. Pia nikasema na ninaamini kwamba RAIS wangu hakuwahi, hana, na hatakuwa na VISION ya wapi anataka kuipeleka Tanzania.

Ndg. Wanajf naomba nisiwachoshe na maneno mengi lkn naomba niseme hili, kwamba naomba msamaha kwa wana-CCM wenzangu ambao nimekuwa nao kwa kipindi chote hicho akiwemo marehemu baba yangu aliyewahi kuwa Kiongozi wa CCM na serikali katika ngazi ya Kata na Kijiji kuhusu maamuzi haya ya kuachana na CCM na kujiunga CHADEMA, chama ambacho kinaonekana kuwa na vision ya kuibadilisha Tanzania. Naomba wale wote nitakaowakwaza kwa maamuzi yangu haya wanisamehe na kamwe wasinilaumu kwasababu si mimi niliyeamua BALI NI MSUKUMO WA UZALENDO NA UPENDO KWA NCHI YANGU TANZANIA ndiyo maana nimeamua Kuvua Gamba na Kuvaa GWANDA.

KWAHIYO: Kuanzia leo tarehe 01.06.2012, Mimi TELO, nikiwa na akili zangu timamu na kwa uwezo wangu wote na kwa upendo na Uzalendo nilionao dhidi ya nchi yangu Tanzania, Natangaza Rasmi kwamba Nimekuwa Mwanachama wa CHADEMA.

WITO: Nawaomba Watanzania wote popote mlipo chini ya JUA, tuungane kwa pamoja kwa ajili ya ukombozi wa nchi yetu. Na huo muungano ninauongelea hapa ni kwa kujiunga na CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA).

Natanguliza shukrani sana, kwani hatimaye NIMEKUWA HURU; TENA HURU KWELI KWELI baada ya kuachana na maumivu ambayo nimekuwa nayo tangu mwaka 2005.

Ni mimi,
TELO
01.06.2012
 
Mkubwa! ulimechelewa wapi?njoo macopolo inanafasi za kumwaga,dreva makini

Hongera kwa kufanya uwamzi sahihi,kwa wakati sasa,kwa lengo sahihi
 
Karibu kamanda,ULIKUWA UKITUMIKA NA NAPE KWA UJIRA WA BUKU MBILI HUMU ILA 2MEKUSAMEHE
 
Hongera sana TULO kwa kuwa huru, na zaidi hongera sana kwa kuwatia shime waliokuwa wagumu kuthubutu.
Hakuna kulala!
 
Mkubwa! ulimechelewa wapi?njoo macopolo inanafasi za kumwaga,dreva makini

Hongera kwa kufanya uwamzi sahihi,kwa wakati sasa,kwa lengo sahihi

Ahsante sana. Tuko pamoja kwa ukombozi wa Tz.
 

Karibu sana, kumbuka huku hatutoi pesa wala kofia kwa wananchi ili watupigie kura, huku unatakiwa kuchangia chama ili kiende mbele
 
Karibu kamanda,ULIKUWA UKITUMIKA NA NAPE KWA UJIRA WA BUKU MBILI HUMU ILA 2MEKUSAMEHE

Ahsante sana mzee. Ila nikuweke sawa kidogo, Nape hana uwezo wa kunitumikisha kwa ujira wowote, kwani namzidi Nape kwa vingi vya maana.
 
Umechelewa tu lakini bado una nafasi na mchango mkubwa katika harakati za kuikomboa tanzania yetu!

Mungu Ibariki CHADEMA
Mungu Ibariki Tanzania
Na watu wote waseme aaamen!
 
Karibu sana, kumbuka huku hatutoi pesa wala kofia kwa wananchi ili watupigie kura, huku unatakiwa kuchangia chama ili kiende mbele

Ahasnte sana na mimi nafahamu hilo.
 
Pamoja TELO. Huku hatuna pesa za kugawa, huku kwetu ni kujitolea. Wewe ndiye unapaswa kukisaidia chama. Hongera mdogo wangu.
 
Daima ukweli utakuweka huru, tii nafsi yako, karibu katika jeshi la ukombozi.
 
Mungu ibariki CHADEMA,
wabariki viongozi wake,hekima umoja na amani,
Mungu ibariki CHADEMA na WATU wakee
Ibariki CHAADEMA,
ibariki CHAADEMA,
KIBARIKI CHADEMA NA WATU WAKEE....(usisahau kuweka picha ukirudisha kadi ya waoemu na kupokea hati ya ukombozi!!)
 
Aah! wapi changa la macho hilo. Hujawahi kuwa mwanaCCM labda mwanachama maslahi aina ya akina Ezekiel Maige. Kama nasema uongo tutajie namba yako ya uanachama pamoja na shina lako na tawi lako.
 
Hata huko ambako unasema umehamia kwa kuona kuna Vision ya maedeleo, ikitokea wakashindwa kuwa na vision ya kulisaidia taifa katika maendeleo, usije ukatutangazia kuwa umeamua kuwatosa. Tanzania yetu hii, usidanganyike, hakuna chama hata kimoja chenye vision ya kuleta maendeleo na kupunguza umaskini kwa watanzania. Narudia tena, hakuna chama hata kimoja chenye lengo la dhati la kuinua uchumi wa Tanzania. Nakaribisha matusi kutoka...
.
"LONELINESS IS THE MOST TERRIBLE POVERTY".
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…