Natangaza nia mwaka 2015

Natangaza nia mwaka 2015

kwanza nauza sera zikikubalika mtanijua maana mchakato ni mrefu
...sera ni maneno tu,hata kwenye kanga yapo,jitokeze tujue kama unauwezo wa kusimamia sera hizo...
 
8.
...sera ni maneno tu,hata kwenye kanga yapo,jitokeze tujue kama unauwezo wa kusimamia sera hizo...
Tunahitaji mabadiliko makubwa sana Tanzania hasa kiuchumi lakini ili kufikia huko tunahitaji mabadiliko makubwa sana katika siasa zetu. Kiongozi sifa kubwa anayotakiwa kuwa nayo ni mipango aliyonayo ambayo wananchi wanatakiwa kuangalia kati ya hawa wenye mipango bora ni nani anasifa za ziada kushinda wengine. Cha kusikitisha siasa zetu zimepoteza mwelekeo watu wanasimamia majina yao, wanasimamia kejeli na matusi kwa wengine, wanasimamia mitandao. kwa wananchi wanaotaka maendeleo ni lazima watambue kuwa mipango au sera kama wengine wanavyoita ndio namba moja katika kutathmini viongozi. ninaonyesha mfano ninategemea na wagombea wenzangu watafuata. wananchi lisaidieni taifa hili ili siasa zibadilike ziwe mipango mbele alafu sifa binafsi za mtu ndio zinafuata. kwa yeyote anayetaka kuwa raisi wa nchi yetu au kwa lugha nyingine anayetaka kuwa msimamizi mkuu wa mali za watanzania jambo la kwanza aulizwe unamipango gani juu ya mali zetu akionekana mipango anayo ndio sasa aulizwe wewe ni nani na ni nini cha ziada ulichonacho zaidi ya hawa wenye mipango mizuri kama ya kwako. kwa yeyote asiyekuwa na mipango asiruhusiwe hata kufikiria kugombea maana hawa ndio wanaturudisha nyuma kwa kukalia kiti cha uongozi wakidhani ni sehemu ya kupata heshima tu na kusaini documents.
 
Tunahitaji mabadiliko makubwa sana Tanzania hasa kiuchumi lakini ili kufikia huko tunahitaji mabadiliko makubwa sana katika siasa zetu. Kiongozi sifa kubwa anayotakiwa kuwa nayo ni mipango aliyonayo ambayo wananchi wanatakiwa kuangalia kati ya hawa wenye mipango bora ni nani anasifa za ziada kushinda wengine. Cha kusikitisha siasa zetu zimepoteza mwelekeo watu wanasimamia majina yao, wanasimamia kejeli na matusi kwa wengine, wanasimamia mitandao. kwa wananchi wanaotaka maendeleo ni lazima watambue kuwa mipango au sera kama wengine wanavyoita ndio namba moja katika kutathmini viongozi. ninaonyesha mfano ninategemea na wagombea wenzangu watafuata. wananchi lisaidieni taifa hili ili siasa zibadilike ziwe mipango mbele alafu sifa binafsi za mtu ndio zinafuata. kwa yeyote anayetaka kuwa raisi wa nchi yetu au kwa lugha nyingine anayetaka kuwa msimamizi mkuu wa mali za watanzania jambo la kwanza aulizwe unamipango gani juu ya mali zetu akionekana mipango anayo ndio sasa aulizwe wewe ni nani na ni nini cha ziada ulichonacho zaidi ya hawa wenye mipango mizuri kama ya kwako. kwa yeyote asiyekuwa na mipango asiruhusiwe hata kufikiria kugombea maana hawa ndio wanaturudisha nyuma kwa kukalia kiti cha uongozi wakidhani ni sehemu ya kupata heshima tu na kusaini documents.

...yaani wewe from this analysis hufai kuwa kiongozi hata wa mtaa maana hujui siasa ya tanzania na tanganyika. Tatizo tulilonalo tanganyika sio sera na ahadi nzuri nooooooooo...!! zipo sera nzuriiisana za ccm lakini tatizo ni mfumo mzima wa siasa za ccm na washirika wake ndo zimetufikisha hapa tulipo leo. tuliamini maneno mazuri na ahadi nzuri kwa miaka mingi bila kuona matokeo ndo maana tunaikataa ccm na wazushi wote kwakuwa ni wazuri wa sera na kulindana na kupeana ulaji. Tunataka mtu ambaye hata tukimuangalia usoni tunajua hakika anaweza kukisimamia anachokisema,sio kujifichaficha..unaogopa nini..?? kama unania jitokeze tukupe makavu live uyajibu tujue uwezo wako usijekukimbia midahalo...
 
9.
...yaani wewe from this analysis hufai kuwa kiongozi hata wa mtaa maana hujui siasa ya tanzania na tanganyika. Tatizo tulilonalo tanganyika sio sera na ahadi nzuri nooooooooo...!! zipo sera nzuriiisana za ccm lakini tatizo ni mfumo mzima wa siasa za ccm na washirika wake ndo zimetufikisha hapa tulipo leo. tuliamini maneno mazuri na ahadi nzuri kwa miaka mingi bila kuona matokeo ndo maana tunaikataa ccm na wazushi wote kwakuwa ni wazuri wa sera na kulindana na kupeana ulaji. Tunataka mtu ambaye hata tukimuangalia usoni tunajua hakika anaweza kukisimamia anachokisema,sio kujifichaficha..unaogopa nini..?? kama unania jitokeze tukupe makavu live uyajibu tujue uwezo wako usijekukimbia midahalo...

Kuna tatizo ambalo wengi hatulijui utakuta mtu anasema tuna sera nzuri lakini tatizo ni utekelezaji lakini ukimuuliza sera gani mfano nzuri tuliyonayo hajui hata moja sasa utashuhudiaje kuwa kuna sera nzuri bila kuzijua. huu umekuwa kama ni wimbo tuna sera nzuri. labda nikuulize za chama ulichokitaja kuhusu uchumi zinasemaje? sera za chama ulichokitaja kuhusu rasilimali za taifa zinasemaje? Nijuavyo mimi maandishi yaliyoandikwa katika kitabu yakiitwa sera ni mkusanyiko wa shida za wananchi zimetajwa kwa ujumla wake tu raisi akiingia madarakani anaweza atakayotekeleza sawa asiyotekeleza hata walioyatunga hakuna wa kuhoji. bali chama hiki kimekuwa na sera mbadala zinazoitwa ahadi za wagombea. hizi ahadi ndio zimekuwa na nguvu mpaka bunge linahoji ahadi za raisi. Bado nashindwa kuelewa unatumia kigezo gani kwa kusema sera nzuri lakini mimi nakushauri hivi sera nzuri ni ule mpango unaoangalia tatizo la taifa nini na ukatoa suluhisho la utatuzi. mfano kuhusu swala la kandarasi za ujenzi mfano barabara. sera za wanaotutawala kwa sasa ni kuwashauri wakandarasi wazalendo kuungana. mimi sera yangu kwanza ni kuweka malengo ya kufanya asilimia inayofanywa na wazalendo kuwa 75% ya kandarasi zote. Kuna changamoto kubwa kwa Tanzania kuunda ushirika kwani risk ni kubwa hivyo wananchi wanaogopa lakini sisi mkakati wetu utakuwa kuunda makampuni ya taifa na kuwauzia wananchi hisa na kuwa wayaendeshe, kuwajengea mazingira ya kuungana na kutengeneza ushirika wa kwao, kuweka sheria za kila kampuni ya kigeni inayokuja kufanya kandarasi nchini sharti ishirikiane na kampuni ya kizalendo
 
10. binafsi napendekeza wagombea wa uraisi wote wawe wa vyama au binafsi kama wataruhusiwa na katiba mpya sharti la kwanza liwe ni kuwasilisha sera au malengo yao katika tume ya taifa ya uchaguzi, tume ipitie malengo haya na wale wasio na malengo ya kupeleka taifa letu mbele majina yao yaondolewe katika kinyang'anyiro hicho. na kwa raisi atakayeshinda uchaguzi mpango wake uwasilishwe katika bunge na ndio uwe mwongozo wa bunge kusimamia utendaji wa serikali. Mimi binafsi moja ya malengo yangu ni kuimarisha mfumo wa utawala wa wa nchi yetu kwa kuhakikisha uhuru mihimili mitatu ya nchi hii kila mmoja unafanya kazi yake kwa kujitegemea na kwa mujibu wa katiba kwa kuondoa minaya yote ya kulindana. Ni mategemeo yangu kuwa huu utakuwa mwanzo mzuri wa sisi tutakaokuwa tukiendesha shughuli za serikali kuhakikisha tunatimiza yale tuliyoyabainisha kuwa malengo yetu wakati tukiomba ridhaa ya wananchi kwani tutakuwa na usimamizi kutoka kwa mhimili wa bunge ambao ni mategemeo yangu kuwa kikatiba watakuwa na uwezo wa kuiwajibisha serikali kwa ujumla au sehemu ya serikali na iwapo watakuwa na malengo yaliyoainishwa kazi itakuwa rahisi kwao kuipima serikali. lakini pia ki mtizamo wangu ninapendekeza kupitia katiba mpya makundi ya kijamii yapewe uwezo wa kufungua kesi mahakamani iwapo serikali imeshindwa kutimiza yale iliyoahidi kwa wananchi na mahakama itoe maamuzi yake kwa kuliagiza bunge kuchukua hatua dhidi ya serikali. kwa mfumo kama huu nategemea utajenga uwajibikaji kwa serikali yangu na serikali nyingine zitakazofuatia.
 
11. binafsi ningependa wabunge wote wawe wakazi wa eneo lake la ubunge kwa maana ya kwamba kila mbunge awe akitoka bungeni anaenda katika jimbo lake la uchaguzi ambako anakuwa na ofisi. Mbunge anafanya kazi ya kusimamia utendaji wa serikali jimboni kwake kuangalia bajeti ya serikali ilivyotengwa ndivyo inavyotekelezwa jimboni kwake, anafuatilia uwajibikaji wa watumishi wa umma katika jimbo lake, anasikiliza matatizo yaliyoko katika jimbo lake, anahamasisha shughuli za maendeleo katika jimbo lake. Katika kufanya haya anakusanya takwimu ambazo akirudi bungeni anaenda kuwasilisha takwimu na bunge llinajadili takwimu zilizowasilishwa na wabunge kupima utendaji wa serikali na kushauri. Binafsi ningependa bunge liwe na mfumo wake kuanzia juu mpaka chini kama ilivyo serikali hivyo madiwani wote wanakuwa katika jimbo ofisi yao kuu ni ofisi ya mbunge. hawa madiwanani ndio wanafanya kazi ya usimizi kwa ngazi ya kata na kuwasilisha takwimu zao katika ofisi ya mbunge na ofisi ya mbunge inacambua taarifa za madiwani pamoja na kufuatilia utendaji wa halmashauri na kupata data kamili ambazo madiwani watazitumia kuhoji halmashauri yao na pia takwimu hizo kupelekwa bungeni ili zijumuishwe na takwimu za taifa ili kupata hoja za bunge. Bahati mbaya hili halitakuwa mikononi mwangu kama raisi bali liko mikononi mwa wananchi wenyewe pengine tuombe katiba mpya tuwekewe mfumo ambao utamfanya mbunge awajibike katika jimbo lake, mfumo ambao bunge litaisimamia vizuri serikali.
 
Katika yale niliyokwisha eleza naomba mrejesho wenu iwe ni swali, hoja ya kuboresha au kukosoa yote nakaribisha
 
Back
Top Bottom