1.baada ya kutafakari kwa kina nimeamua kutangaza nia ya kugombea uraisi mwaka 2015 sera zangu.
miundo mbinu: ninapanga kufanya usafiri wa treni kuwa njia kuu ya usafirishaji tanzania. kwa hapa ninapanga kuimarisha reli ya kati kwa viwango vya kimataifa, kuijenga mpaka DRC, ninapanga kujenga reli kutoka bandari ya mtwarakupitia mbeya, rukwa katavi hadi tabora, kuimarisha reli ya tanga musoma. kwa kuanzia ninapanga kuimarisha bandari ya dar kwa kuongeza uwezo wake. ninategemea kuweka treni za kisasa reli ya kati kuanzia dar hadi mwanza na kigoma. ninategemea kuanzisha treni kutoka mtwara kupitia mbeya, rukwa, katavi, kupitia tabora hadi mwanza, kuanzisha treni kutoka dar kupitia tanga kilimanjaro hadi musoma. baada ya kutengeneza mtandao huu wa reli nitaanza kujenga bara bara za lami kuwa feeder za reli.
mategemeo yangu hapa ni kupunguza gharama za usafiri kwa wananchi, kuimarisha usafiri baina ya kanda na kanda, kuongeza kiwango cha mizigo ya nchi jirani inayopitia kwetu hivyo kuongeza pato la taifa. nategemea usafiri wa treni utachochea utalii wa ndani na hivyo kutengeneza ajira. Pia treni kuanzia mtwara kupitia ukanda wa kusini hadi mwanza itafungua soko la mazao ya chakula yanayozalishwa kusini kwa nchi za kasikazini
rasilimali za taifa: sera yangu kuhusu rasilimali za taifa ni kwamba mbia atakaribishwa kuwekeza pale tu serikali itakapokuwa inapata asilimia 50% ya mapato ghafi au zaidi. pungufu ya hapo ni hasara kwa taifa hatutaruhusu mgeni kuja kuvuna hiyo mali bali tutafanya mipango ya kuwawezesha wazalendo kifedha na kiteknolojia waje kuvuna mali hizo.
mategemeo ni kuwa sera hii italinda mali za taifa zisiporwe kupitia rushwa na kutokujua.
Kilimo: nikiingia madarakani ninategemea kulifanya ghala la chakula la taifa kuwa shirika linalonunua chakula wakati wa msimu nchi nzima kila zao linalohifadhika na kuuza wakati wa upungu. nitatoa msamaha wa kodi kwa mazao yote ya chakula yanayosafirishwa nje ya nchi na nitafungua mipaka yote chakula kiuzwe nje. nitahamasisha utengezaji wa bidhaa zitokanazo na mazao ya chakula kwa wingi.
lengo la sera hii ni kutoa soko kwa mkulima na soko la chakula ndilo pekee litakalochochea ukuaji wa kilimo kwa wakulima kuongeza kilimo kila msimu. serikali itajitahidi kwa upande wake kujenga mabwawa ya maji, mifumo ya umwagiliaji. pia itawawezesha wakulima kupata pembejeo kwa urahisi. kutokana na kufungua soko mategemeo ni kwamba kwa kuanzia kunaweza kusababisha upungufu wa chakula jambo ambalo serikali itatenga fungu la dharula kuagiza chakula kutoka nchi zilizokwisha jidhatiti katika kilimo ili kukabiliana na upungufu. ninaamini nguvu ya soko itawasukuma wakulima kuongeza ukulima na kuvutia watu kuwekeza katika kilimo na kufanya tujitosheleze na soko la jirani katika kipindi cha miaka michache.
kandarasi: sera yangu ni kufanya kandarasi za ujenzi kufanywa na wazalendo kwa asilia 75 na wageni kufanya asilia 25 tu. hii nitaifanya kwa kuanzisha kituo cha kuwaunganisha wataalamu wazalendo kupitia kampuni zitakazoanzishwa ama na wao wenyewe au na serikali na kuwauzia watanzania hisa. kila kampuni itayokuwa inakuja kufanya kazi nchini lazima tuweke masharti ya kushirikiana na kampuni za kizalendo ndio wapate kazi.
wafungwa: sera yangu ni kwamba ni naamini magereza ni sehemu ya kumrekebisha mtu tabia hivyo ninaamini kila mfungwa ana haki ya kufanya kazi. nitanya kazi ya kilimo isiyo na mshahara kuwa ndio kazi ya wafungwa. Hapa wafungwa watakuwa wakiishi kila mtu na sehemu yake ya kulala kama maisha ya mtanzania wa kipato cha chini bali anakuwa anafanya kazi isiyokuwa na mshahara na kutengwa na familia yake, tutafungua mashamba makubwa maporini na magereza zote zitahamishiwa maporini. huko watakuwa wakifanya kazi ya kilimo na mazao yatokanayo na kilimo yatauzwa na kuwaboreshea mazingira ya kuishi. iwapo watazalisha sana ziada watakuwa wakitunziwa na kukabidhiwa pale wanapotoka magerezani ili wakaanzie maisha.
nitaendelea kutoa sera zangu kadiri muda unavyokwenda kabla ya 2015
miundo mbinu: ninapanga kufanya usafiri wa treni kuwa njia kuu ya usafirishaji tanzania. kwa hapa ninapanga kuimarisha reli ya kati kwa viwango vya kimataifa, kuijenga mpaka DRC, ninapanga kujenga reli kutoka bandari ya mtwarakupitia mbeya, rukwa katavi hadi tabora, kuimarisha reli ya tanga musoma. kwa kuanzia ninapanga kuimarisha bandari ya dar kwa kuongeza uwezo wake. ninategemea kuweka treni za kisasa reli ya kati kuanzia dar hadi mwanza na kigoma. ninategemea kuanzisha treni kutoka mtwara kupitia mbeya, rukwa, katavi, kupitia tabora hadi mwanza, kuanzisha treni kutoka dar kupitia tanga kilimanjaro hadi musoma. baada ya kutengeneza mtandao huu wa reli nitaanza kujenga bara bara za lami kuwa feeder za reli.
mategemeo yangu hapa ni kupunguza gharama za usafiri kwa wananchi, kuimarisha usafiri baina ya kanda na kanda, kuongeza kiwango cha mizigo ya nchi jirani inayopitia kwetu hivyo kuongeza pato la taifa. nategemea usafiri wa treni utachochea utalii wa ndani na hivyo kutengeneza ajira. Pia treni kuanzia mtwara kupitia ukanda wa kusini hadi mwanza itafungua soko la mazao ya chakula yanayozalishwa kusini kwa nchi za kasikazini
rasilimali za taifa: sera yangu kuhusu rasilimali za taifa ni kwamba mbia atakaribishwa kuwekeza pale tu serikali itakapokuwa inapata asilimia 50% ya mapato ghafi au zaidi. pungufu ya hapo ni hasara kwa taifa hatutaruhusu mgeni kuja kuvuna hiyo mali bali tutafanya mipango ya kuwawezesha wazalendo kifedha na kiteknolojia waje kuvuna mali hizo.
mategemeo ni kuwa sera hii italinda mali za taifa zisiporwe kupitia rushwa na kutokujua.
Kilimo: nikiingia madarakani ninategemea kulifanya ghala la chakula la taifa kuwa shirika linalonunua chakula wakati wa msimu nchi nzima kila zao linalohifadhika na kuuza wakati wa upungu. nitatoa msamaha wa kodi kwa mazao yote ya chakula yanayosafirishwa nje ya nchi na nitafungua mipaka yote chakula kiuzwe nje. nitahamasisha utengezaji wa bidhaa zitokanazo na mazao ya chakula kwa wingi.
lengo la sera hii ni kutoa soko kwa mkulima na soko la chakula ndilo pekee litakalochochea ukuaji wa kilimo kwa wakulima kuongeza kilimo kila msimu. serikali itajitahidi kwa upande wake kujenga mabwawa ya maji, mifumo ya umwagiliaji. pia itawawezesha wakulima kupata pembejeo kwa urahisi. kutokana na kufungua soko mategemeo ni kwamba kwa kuanzia kunaweza kusababisha upungufu wa chakula jambo ambalo serikali itatenga fungu la dharula kuagiza chakula kutoka nchi zilizokwisha jidhatiti katika kilimo ili kukabiliana na upungufu. ninaamini nguvu ya soko itawasukuma wakulima kuongeza ukulima na kuvutia watu kuwekeza katika kilimo na kufanya tujitosheleze na soko la jirani katika kipindi cha miaka michache.
kandarasi: sera yangu ni kufanya kandarasi za ujenzi kufanywa na wazalendo kwa asilia 75 na wageni kufanya asilia 25 tu. hii nitaifanya kwa kuanzisha kituo cha kuwaunganisha wataalamu wazalendo kupitia kampuni zitakazoanzishwa ama na wao wenyewe au na serikali na kuwauzia watanzania hisa. kila kampuni itayokuwa inakuja kufanya kazi nchini lazima tuweke masharti ya kushirikiana na kampuni za kizalendo ndio wapate kazi.
wafungwa: sera yangu ni kwamba ni naamini magereza ni sehemu ya kumrekebisha mtu tabia hivyo ninaamini kila mfungwa ana haki ya kufanya kazi. nitanya kazi ya kilimo isiyo na mshahara kuwa ndio kazi ya wafungwa. Hapa wafungwa watakuwa wakiishi kila mtu na sehemu yake ya kulala kama maisha ya mtanzania wa kipato cha chini bali anakuwa anafanya kazi isiyokuwa na mshahara na kutengwa na familia yake, tutafungua mashamba makubwa maporini na magereza zote zitahamishiwa maporini. huko watakuwa wakifanya kazi ya kilimo na mazao yatokanayo na kilimo yatauzwa na kuwaboreshea mazingira ya kuishi. iwapo watazalisha sana ziada watakuwa wakitunziwa na kukabidhiwa pale wanapotoka magerezani ili wakaanzie maisha.
nitaendelea kutoa sera zangu kadiri muda unavyokwenda kabla ya 2015