Natamani kusikia hili kutoka kwa Bashe

Natamani kusikia hili kutoka kwa Bashe

Tiote

Senior Member
Joined
Mar 6, 2011
Posts
139
Reaction score
36
Majuma kadhaa yaliyopita, yule mshambuliaji wa kujitoa Mhanga aitwae Hussein Bashe (Certificate CBE) alitoa tuhumua nzito dhidi ya Waziri Membe, akimhusisha na tukio baya la shambulio dhidi ya Mhariri nguli wa magazeti ya New Habari Corportion, mmoja Bwana Absalom Kibanda ambaye bado anahudhuria matibabu huko Afrika Kusini. Huku wenye akili zetu tukijua na kuamini kwamba tuhuma zile zilichochewa na chuki dhidi ya mtuhumiwa na mchezo wa kisiasa uliopangiliwa vilivyo na mafisadi wasioisha kuweweseka, juma moja lililopita mwanasiasa na wakili mahiri nchini Mabere Marando alikuja na tuhuma na majina kumi ya watu ambao kwa madai yake ndiyo waliohusika na ukatili huo na ule aliofanyiwa Dr. Steven Ulimboka. Katika majina hayo, ambayo mtoa tuhuma alisema ana ushahidi wa kuhusika kwao, jina la Membe halikutajwa wala kuhusiahwa na unyama huu.

Hili bila shaka ni pigo kwa mshambuliaji huyu (Bashe) na principals wake maana sasa umma wa watanzania umebaini kwamba madai ya Bashe yalichochewa na chuki na kujihami, kwa staili ile ile ya Dodoma. Hakika Bashe amejivika kilemba cha kichekesho na kulazimika kuula mkate wa majonzi!
 
Mimi huamini kwamba Mungu huwa na wale walio katika wema. Katika hili Membe amekuwa na Mungu kwa vile ni dhahiri kwamba hakuhusika wala hakuwahi kuwa na dhamira ya kudhuru yeyote,akiwemo Kibanda ambaye kamwe hajapata kuwa adui yake. Sasa watafute lingine lakini likiwa la staili hii hii basi wataendelea kuaibika.
 
Nimependa hii staili ya Membe ya kukataa kujibizana na mbwa wakati mwenye mbwa ambaye ndiye saizi yake yupo. Bashe alipaswa kujua kwamba a quiet fool is considered wise. Angekaa kimya tusingejua ujuha wake.
 
wewe huenda ni membe au kibara wa membe, ila kifupi nikwambie we ni mnafiki pia kama huyo bashe, ccm wote ni wanafiki.
 
wewe huenda ni membe au kibara wa membe, ila kifupi nikwambie we ni mnafiki pia kama huyo bashe, ccm wote ni wanafiki.

nilitarajia umkosoe kwa data na ushahidi badala ya kung'ang'ana na kauli zisizoeleweka. Ccm imeingiaje humu? Toa makengeza wewe!
 
nilitarajia umkosoe kwa data na ushahidi badala ya kung'ang'ana na kauli zisizoeleweka. Ccm imeingiaje humu? Toa makengeza wewe!

acheni kumjadili hayawani. Yule dogo anatafuta uhalali wa kuendelea kuishi nchini baada ya uraia wake kuleta mawaa. Nchi hii ukiwa na mawaa jiunge na mafisadi utapona.
 
Leteni hoja za maana si hizi zisizo kuwa na mashiko, ya Membe na Bashe hawa waliyaanza dhamani kwani si Membe alisema kwenye dakika 45 ITV kuwa ana maadui wakiwemo waandishi wahabari na kama yeye anaona Bashe amemtuhumu visivyo mimi na wew hatuna haja yakuwa kasuku huyo Membe angetoka akasema au aende mahakamani basi kwamba ka kashifiwa! naaza kukubaliana na wakina Mtambuzi kuwa kuna watu humu wanatumiwa na wanasiasa na vibaraka wa watu fulani, acheni kuwa watumwa wa mawazo hata nyie mkijiamini mnaweza kuwa kama wao badala ya kujidhalilisha na thread za kikasuku!
 
Majuma kadhaa yaliyopita, yule mshambuliaji wa kujitoa Mhanga aitwae Hussein Bashe (Certificate CBE) alitoa tuhumua nzito dhidi ya Waziri Membe, akimhusisha na tukio baya la shambulio dhidi ya Mhariri nguli wa magazeti ya New Habari Corportion, mmoja Bwana Absalom Kibanda ambaye bado anahudhuria matibabu huko Afrika Kusini. Huku wenye akili zetu tukijua na kuamini kwamba tuhuma zile zilichochewa na chuki dhidi ya mtuhumiwa na mchezo wa kisiasa uliopangiliwa vilivyo na mafisadi wasioisha kuweweseka, juma moja lililopita mwanasiasa na wakili mahiri nchini Mabere Marando alikuja na tuhuma na majina kumi ya watu ambao kwa madai yake ndiyo waliohusika na ukatili huo na ule aliofanyiwa Dr. Steven Ulimboka. Katika majina hayo, ambayo mtoa tuhuma alisema ana ushahidi wa kuhusika kwao, jina la Membe halikutajwa wala kuhusiahwa na unyama huu.

Hili bila shaka ni pigo kwa mshambuliaji huyu (Bashe) na principals wake maana sasa umma wa watanzania umebaini kwamba madai ya Bashe yalichochewa na chuki na kujihami, kwa staili ile ile ya Dodoma. Hakika Bashe amejivika kilemba cha kichekesho na kulazimika kuula mkate wa majonzi!

Nimesoma na BASHE MZUMBE UNIVERSITY degree ya kwanza acha umbea wewe na propaganda za ovyo, unatakiwa kupewa BAN kwa uongo na uzandiki
 
Naungana na BASHE mpaka pale MEMBE atakapo taja hadharani kwa majina yao wale maadui wake wale pamoja na waandishi wawili wa habari.

Vp ni kweli ajahojiwa na polisi kuhusu kauli yake? au wanasubiri mpaka ateuliwe kugombea urais?
 
Back
Top Bottom