Lisemwalo lipo, na kama halipo basi linakuja. Nasema hivi; natamani kuona siku moja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassani, anakunywa juisi Ikulu na Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu ambaye yuko gerezani akishtakiwa kwa Kesi ya Uhaini na Uchochezi.
Hili halitakuwa jambo geni kwa Rais kunywa juisi na wapinzani wake wa Kisiasa. Rais Kikwete enzi za uongozi wake aliwahi kuwaita wapinzani wakakaa meza moja Ikulu, na kunywa juisi mambo yakaenda.
Wanaofuatilia Siasa za Dunia wanajua upinzani uliopo baina ya Urusi na Marekani. Ni upinzani wa miaka nenda rudi. Majuma kadhaa yaliyopita Donald Trump alitoa siku kumi kwa Rais wa Urusi Vladmir Putin kukomesha vita na Ukraine ama la, Urusi ikumbane na vikwazo babu kubwa vya kibiashara baina yake, ndia na China.
Ajabu ni kwamba aliyetoa siku kumi huyo huyo kaomba kukaa meza moja na Putin ili wazungumze na mazungumzo yamefanyika jana huko Alaska kwenye Kambi moja ya Jeshi la Marekani. Wamekula wamekunywa.
Hiyo ndiyo Siasa, huo ndio ukomavu na huo ndio ukubwa.
Ukubwa jalala! Rais Samia, wewe ni Mwanasiasa mzoefu, naamini kwa Imani yako unayo hofu ya Mungu. Tundu Lissu ni mpinzani wako Kisiasa, kama ulivyofuta ya mtangulizi wako, ukawarudisha nyumbani akina Lissu na wenzake, FUTA ujinga wowote waliofanya kwako. mtoe humo alimo sasa.
Kaa naye meza moja mzungumze juu ya namna bora ya kuendesha Siasa hapa nchini kwa maslahi mapana ya nchi na watu wake.
Kila mtu anaweza kupata maono juu ya jambo lolote hata kama siyo Mchungaji au Nabii.
Hili halitakuwa jambo geni kwa Rais kunywa juisi na wapinzani wake wa Kisiasa. Rais Kikwete enzi za uongozi wake aliwahi kuwaita wapinzani wakakaa meza moja Ikulu, na kunywa juisi mambo yakaenda.
Wanaofuatilia Siasa za Dunia wanajua upinzani uliopo baina ya Urusi na Marekani. Ni upinzani wa miaka nenda rudi. Majuma kadhaa yaliyopita Donald Trump alitoa siku kumi kwa Rais wa Urusi Vladmir Putin kukomesha vita na Ukraine ama la, Urusi ikumbane na vikwazo babu kubwa vya kibiashara baina yake, ndia na China.
Ajabu ni kwamba aliyetoa siku kumi huyo huyo kaomba kukaa meza moja na Putin ili wazungumze na mazungumzo yamefanyika jana huko Alaska kwenye Kambi moja ya Jeshi la Marekani. Wamekula wamekunywa.
Hiyo ndiyo Siasa, huo ndio ukomavu na huo ndio ukubwa.
Ukubwa jalala! Rais Samia, wewe ni Mwanasiasa mzoefu, naamini kwa Imani yako unayo hofu ya Mungu. Tundu Lissu ni mpinzani wako Kisiasa, kama ulivyofuta ya mtangulizi wako, ukawarudisha nyumbani akina Lissu na wenzake, FUTA ujinga wowote waliofanya kwako. mtoe humo alimo sasa.
Kaa naye meza moja mzungumze juu ya namna bora ya kuendesha Siasa hapa nchini kwa maslahi mapana ya nchi na watu wake.
Kila mtu anaweza kupata maono juu ya jambo lolote hata kama siyo Mchungaji au Nabii.