Natafuta soko la pilipili mbuzi

Natafuta soko la pilipili mbuzi

KIPANYA

Member
Joined
Jan 3, 2011
Posts
61
Reaction score
2
Jamani nina shamba la pili pili mbuzi, zipo tayari kwa kuvunwa, naomba kupata soko lake na bei
 
Mia tano kariakoo napata kisado muwe mnafanya research kwanza kabla hamjateketeza pesa za mkopo kwenye biashara kichaa
 
Uzuri wa Pilipili ni zao linavunwa endelevu hata mwaka mzima na bei huwa zinapanda na kushuka ...
Naenda wewe mwenyewe soko LA mabibo au karikoo kule shimoni utafute madalali utauza mkuu
Achana na watu wasiokuwa hata na tuta LA mchicha
 
Jamani nina shamba la pili pili mbuzi, zipo tayari kwa kuvunwa, naomba kupata soko lake na bei
Ungekuwa umelima nyanya saiv ungekuwa unapiga hela,kuna mazao mengine yana changamoto kwenye soko hvyo kabla ya kulima zao flan ni vzr ukafanya utafiti wa uhitaji ndipo ulime
 
Ungekuwa umelima nyanya saiv ungekuwa unapiga hela,kuna mazao mengine yana changamoto kwenye soko hvyo kabla ya kulima zao flan ni vzr ukafanya utafiti wa uhitaji ndipo ulime
Mkuu wewe ulishawahi kulima??ungekuwa umeshawahi kulima kilimo cha mazao hasa haya ya bustani usingesema hivyo!!mala ngapi nyanya zimewaliza watu hadi ndoo ilifikia shilingi 500!!pale gairo?na mwaka jana tu watu pilipili wamepiga pesa si mchezo!!haya mazao inategemea na muda utakaovuna je demand iko vipi kulinganisha na supply!!
 
Mkuu wewe ulishawahi kulima??ungekuwa umeshawahi kulima kilimo cha mazao hasa haya ya bustani usingesema hivyo!!mala ngapi nyanya zimewaliza watu hadi ndoo ilifikia shilingi 500!!pale gairo?na mwaka jana tu watu pilipili wamepiga pesa si mchezo!!haya mazao inategemea na muda utakaovuna je demand iko vipi kulinganisha na supply!!
Demand kubwa ya zao la nyanya ipo dsm ,sasa mtu lazima ajiongeze, kama huko kuna wakulima wengi wa hilo zao ni dhahiri kabisa supply capacity itakuwa kubwa kushinda demand so lazima hiyo excess upeleke sehem ambapo wakulima wa hilo zao hawapo
 
Demand kubwa ya zao la nyanya ipo dsm ,sasa mtu lazima ajiongeze, kama huko kuna wakulima wengi wa hilo zao ni dhahiri kabisa supply capacity itakuwa kubwa kushinda demand so lazima hiyo excess upeleke sehem ambapo wakulima wa hilo zao hawapo
Mkuu soko kubwa la haya mazao ya bustani ni masoko yaliyopo dsm kariakoo,tmk sterio ,wakulima wa iringa,morogoro,kilimanjaro wengi soko lao ni dar na ndiko kwenye bei nzuri,ila hata kwnyewe pakibadirika utalia
 
Back
Top Bottom