Habari wana Jf.
Naombeni ushauri kuhusu hili nimechanganyikiwa. Nina mdogo wangu yupo kwenye ndoa mwaka wa 12 sasa na ana watoto 3. Yeye na mumewe wanaonyesha wanaishi vizuri, yaani mume anamjali. Tatizo ni wiki 2 zilizopita nimeambiwa na mmoja wa ndugu za mumewe kwamba mume wake anatembea na mwanamke mwingine ambaye ndugu wa mume wengi wanamjua kwa kuwa huyo kimada alijipendekeza hadi kwa mama wa mume na mama kwa kupewa vizawadi au kwa roho mbaya akamkubali huyo bi mdogo na kuanza kumtambulisha kwa ndugu zake kama mke wa pili wa mwanae.
Huyo kimada kwenye sherehe za ndugu wa mume huwa anakwenda wakati huohuo na mdogo wangu yupo ila sasa yeye hamjui, maskini yeye yupo busy ukweni akifanya lile na lile kumbe anajichora tu bila kujua. Huku mama mkwe akiwepo na kuangalia tu pamoja na ndugu wengine wanaojua hilo. Na wakati mwingine huyo kimada anaenda hadi kulala kwa ndugu wa mume na anapokelewa vizuri kwa shangwe.
Huyo mdogo wangu hana ugomvi wowote kwa hao ndugu wa mume akiwemo mama mkwe wake, yaani wakimwona wanamchekea vizuri na kumkumbatia na wanashirikiana naye kwa mambo mbalimbali iwe shida au raha kuonyesha wanampenda na wamemkubali wakati huohuo wanamzunguka.
Sasa basi mmoja wa hao ndugu imekuwa ikimuuma hiyo hali ila kumwambia mke halali anashindwa ndo kanitafuta mimi dada mtu kanipa mchapo mzima na nimeonyeshwa huyo kimada na kuchunguza nimegundua ni ukweli mtupu. Sasa nimekuwa na mtihani mkubwa je nimwambie mdogo wangu hali ilivyo au nifanyaje?
Wao kama familia wanaishi vizuri kwa amani yaani mume anamjali.ile mbaya waweze sema ni ndoa ya amani na ukaitamani lkn mume na nduguze ndo wanamzunguka kiaina hiyo.
Siyo ndugu wote wa mume wanafanya hivyo ila kuna kikundi kama cha watu 7 ndo wapo busy na huyo kimada na wakati huohuo wakimfanya rafiki na kumpenda mke halali.
USHAURI TAFADHARI NIMWAMBIE MKEWE?