Natafuta mchumba ili baadaye aje kuwa mke

Natafuta mchumba ili baadaye aje kuwa mke

Troubleshooter

Senior Member
Joined
Mar 30, 2016
Posts
130
Reaction score
151
Habari wana JF,

Mimi ni kijana wa kitanzania niliyejitokeza kwenye jukwaa hili nikiamini kuwa upo uwezekano mkubwa wa kukutana na life partner katika jukwaa hili.

Sababu kubwa iliyo nifanya nitumie jukwaa hili ni kuwa wapo watumiaji wengi wa aina tofauti na wengine wenye uhitaji wa kupata wenzi wa ndoa kama mimi.

Kimsingi maisha yamebadilika na ubize umekuwa mwingi sana kiasi kwamba inakuwa vigumu kuweza kusocialize au kuchangamana na jamii ya vijana katika sehemu mbalimbali, hivyo naamini kupitia jukwaa hili upo uwezekano mkubwa wa kumpata mwenzi wangu wa ndoa.

Mimi sifa zangu: ni mweupe mrefu mwembamba kiasi, elimu chuo kikuu naishi Dar es Salaam umri wangu ni miaka 30.

Sifa za mwenza; awe mweusi au maji yakunde sio mnene sana, na asiwe mfupi, elimu ya chuo, awe anakazi au anajishughulisha na shughuli zinazomwingizia kipato. dini mkristo

Kwa wenye sifa tajwa hapo juu tafadhali naomba uni PM ili nikupe details zangu zaidi ahsanteni na karibuni.
 
Japo maelezo mengi lakini umeeleweka, wasubiri watakufuata inbox then ukishapata usisahau kuja kutoa feedback mapema
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom