Natafuta kazi, nina Shahada ya Regional Development Planning

Natafuta kazi, nina Shahada ya Regional Development Planning

juakal

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2015
Posts
587
Reaction score
125
Heshima kwenu wakuu,

Tatizo langu halina tofauti na la wengi hapa jukwaani. Binafsi mimi nimehitimu chuo miaka minne iliyopita, ambapo nilipata shahada ya Regional Development Planning. Kwa lengo la kuwa Planning Officer (Afsa Mipango).

Lakini mpaka dakika hii ninapoandika huu uzi sijawahi kufanikiwa kupata kazi japo hata ya kujitolea tu. Nisiwachoshe sana ndugu zangu, lengo langu ni kuomba msaada kwa yeyote atakayeguswa, uwe wa kimawazo au kazi yoyote halali nitashukuru sana.

NB: Nina uwezo mzuri wa kufanya kazi.

Asanteni.
 
Angalia pia uwezekano wa kuongeza elimu hadi ngazi ya Shahada ya uzamili.
 
Duh kumbe tupo wengi sana...pole mkuu km unapata chance ya kusoma soma master...otherwise omba sana MUNGU hopefully mambo yatakua poa...usije fanya maamuzi ya kishetani
 
Angalia pia uwezekano wa kuongeza elimu hadi ngazi ya Shahada ya uzamili.
Ushauri mbaya. Aongeze elimu wakati hata degree moja tu hapati kazi. Akiongeza elimu ili iweje? Kwani kakosa kazi kwa sababu elimu ndogo?
 
Ajira sasa n za kujuana. Ila wewe ni afisa mipango, jiajiri best. Weka mipango yako fresh pata mkopo endesha maisha.

Asante best. Tatizo mikopo yenyewe masharti yake najikuta siyawezi
 
Angalia pia uwezekano wa kuongeza elimu hadi ngazi ya Shahada ya uzamili.

Ni kweli, lakini pia naweza kuongeza elimu bado mambo yakawa magumu vile vile
 
Duh kumbe tupo wengi sana...pole mkuu km unapata chance ya kusoma soma master...otherwise omba sana MUNGU hopefully mambo yatakua poa...usije fanya maamuzi ya kishetani

Tupo wengi mkuu
 
Asante best. Tatizo mikopo yenyewe masharti yake najikuta siyawezi
Lakini mkopo unaozungumziwa na wa shilingi ngapi kwani unachotakiwa ni kuanza pale ulipo kwani "mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe" hivyo usifikirie mtaji kwa big picture wewe angalia kwa level ya hapo ulipo ni shughuli gani unaweza kuifanya na ikakuingizia kipato.

Siku hizi kuna mikopo midogo midogo ya laki 2 mpaka 5 kwenye taasisi za mikopo ila unachotakiwa ni uvumilivu tu kwa kuwa huwezi kamata laki 5 au milioni mpaka uanze na kiduchu wanakuwa wanapandisha kadiri unavyo gain.

Mie nilivyomaliza A level nilikaa mtaani 2 years life ikawa tight na huwezi amini niliishi kwa wekundu watatu (30,000) kwa mwaka mzima yaani nilikuwa nakaa sehemu nadaka kuku kwa kuvizia wale wanaotoka vijijini na nilikuwa na network yangu ya wauuza chipsi.

Nadaka kuku watatu kwa hiyo hela nakwenda kuuza napata faida 15,000 siku nyingine mwekundu nikawa nazuga zuga hivyo hivyo mjini huku unasoma ramani mpaka nilipoingia chuo (nimetoa mfano huu ambao unatkiwa kufikiria kwanza kwa pale ulipo na usifikirie mtaji wa mamilioni hata laki 2 au 3 kwani kwa watoto wa mjini anaweza akawa anadaka mitumba mikali alafu anaiuza kwa kuvizia yaani akimwona mjanja mwenzake anamzukia na kumpa issue maisha yanakenda.
 
Jodoki Kalimilo

Nimekuelewa sana mkuu. Asante sana kwa ushauri. Lakini hayo mambo nilisha jaribu lakini kutoka imekuwa ngumu. Unajua nataka kumake life na sio kusurvive tu ilimradi siku ziende. Kwahiyo angalau kwa mtaji wa 1M inaweza kusound kidogo. Pia naweza nikafanya kitu kikaonekana
 
Last edited by a moderator:
Jodoki Kalimilo

Nimekuelewa sana mkuu. Asante sana kwa ushauri. Lakini hayo mambo nilisha jaribu lakini kutoka imekuwa ngumu. Unajua nataka kumake life na sio kusurvive tu ilimradi siku ziende. Kwahiyo angalau kwa mtaji wa 1M inaweza kusound kidogo. Pia naweza nikafanya kitu kikaonekana
Kuna msemo huwezi kwenda peponi mpaka ufe, milioni kwa sasa huna, je utakaa tu chini kuisubiri, najua wewe umesoma masuala ya Planning na by definition tunasema PROJECT is set of investment using available resources to accomplish a certain objective, ukiangalia hiyo definition, Na wewe unachotakiwa kuangalia nguvu yako iko wapi kwa sasa ndio maana nikakupa case study yangu. Hata yule unaemwona ana biashara ya milion 30 sio kwamba alifumania hiyo ela alikuwa na yeye ana wazo kama lako nikiwa na milion 1 ama 2 nitafanya kitu lakini wakati akiwa hana hiyo milioni akawa anafanya vitu ambavyo vitamfanya aweze ku-survive kwanza huku lengo lake linakuwa palepale. Hivyo hata wewe unahitaji kuwa na shughuli ambayo itakufanya ku-survive ili iweze kukujengea network na wadau mbalimbali hata kama wadau unaokutana nao wana elimu ndogo kuliko yako lakini wana experience ya maisha. Kwa juhudi unatakayoinyoshesha kuna faida nyingine ambayo wengi hatuiangalii yaani kuna watu huwa wanasaidia watu wenye juhudi tayai

Hiyo shughuli ya ku-survive ndio itakuwezesha kujipanga kuelekea kutafuta hiyo milioni 1 ambayo unadhani ukiipata unaweza ukafanya jambo kwani

Kazi zipo ipo siku mungu ataleta heri kikubwa ni usijitenge na jamii kwani kuliko na watu ndipo kuna issue
 
Wandugu
Tanzania tuna kazi kweli kweli. Mimi naona nimuunge mkono Augustine Moshi kwa hoja yake ya under-funding kwenye elimu. Kwanza ni kweli ndugu Jasusi kwamba huu utapeli unafanywa kwa kukosa uzalendo kwa hao culprits.

Lakini huo utapeli unapata nguvu na mazingira mazuri(conducive environment) mbele ya public isiyoelimika. Nyinyi mnadhani Kikwete angepata kura zote hizo kwenye uchaguzi kutoka kwa watu walio huru kielimu?

There are too few enlightened people in this land. And so follows....ignorance among wabongo is rampant.

Mzee Moshi you have a point!

Asante sana mkuu. Nimekuelewa sana
 
Back
Top Bottom