Haijulikani upo mkoa gani...
Pili matataizo ya AC kwa magari huwa ni universal..Leakage ya freon, Compressor, evaporator na kadhalika.....
Kwa mfano kama ni freon imeisha Ina maana kuna leakage fundi anatakiwa azibe na ku recharge upya..bei zipo ila sometimes ni maelewano...
Lakini kibongo bongo ukisema unatafuta fundi a AC za Subaru, utapigwa pesa sana...
Kwa kuwa umeshaweka mbele neno fundi wa ac za subaru, atakuja fundi akuambie freon kwenye Subaru tunajaza laki 4 na freon atakayojaza ni 134a ambyo ndiyo recommended kwa magari mengi sana na ndiyo zimejaa mtaani....wakati bei za kawaida hiwa ni elfu 70, 60, 50 kuyegemeana na eneo unaloishi..
Ushauri wangu, tafuta findi mzuri wa AC za magari na si AC za Subaru.
Toyota, Nissan, Subaru, Suzuki, na magari mengi tu ya Ulaya freon inayotumika ni 134a....
Kama compressor ndiyo imekufa, hapo ndiyo utalipa pesa kulingana na bei ya spea ya gari husika....Toyota haitakuwa bei mja na Subaru.