puza46b
Member
- Nov 3, 2010
- 91
- 261
Nalopoka Nilichowaza:
- Hivi itakuwaje iwapo kesho wanaanchi wakaamua kumshangilia kwa nguvu sana Tundu Lissu anapoenda kutoa heshima yake kwa Marehemu Mkapa? Itakuwaje pale wengine wakaamua kupitiliza na kusema Tundu Lissu ni Rais wakiimba raisi raisi raisi, huku mabalozi na wageni wengine wa nchi za nje wakiangalia?
- Hivi itakuwaje pale itakapongundulika wale waliokuwa wakikimbiza magari ni kwa sababu ya upenzi wa watanzania kushangaa kila tukio?
- Hivi itakuwaje pale ambapo ACT Wazalendo, kwa kuangalia mbele, wakaamua kumpa nafasi Lisu agombee uraisi na wakaunganisha nguvu na CHADEMA kwenye uchaguzi?
- Hivi itakuwaje pale ambapo wale waliojaribu, wakashindwa, wakaamua kumalizia kazi? Mungu tupilia mbali.