Nappe katika siasa za Magufuli

Nappe katika siasa za Magufuli

Naona uko field unafanya rehearsal, JPM ashawasha moto kazi yenu saivi ni kuota tu. Hao wazee hadi waitwe chamani ni lini? Soma ibara ya katiba ya ccm inayo wahusu wazee. Kwa uchaguzi ujao hadi ushawishi utoke kwa wajumbe wote ndio JPM anaweza pata hofu. Ngonjera zenu hizo mnazidi kumpa mbinu tu ya kujipanga vizuri.
Kwa namna niijuavyo CCM uyo unaemsema anausalama wa Taifa na Majeshi anaweza kutolewa ndani ya dakika moja na pasiwepo hata dalili ya vurugu
Hajisimamii uchaguzi ndani ya chama
Hajipitishii jina wapo watu na ao watu ndio wenye CCM
 
Kwa namna niijuavyo CCM uyo unaemsema anausalama wa Taifa na Majeshi anaweza kutolewa ndani ya dakika moja na pasiwepo hata dalili ya vurugu
Hajisimamii uchaguzi ndani ya chama
Hajipitishii jina wapo watu na ao watu ndio wenye CCM
Weweee.. unazani mkimtoa ndio kazi imeishia hapo? KUMBUKA RAIS ANWEZA AKATANGAZA HARI YA HATARI AKAA IKULU MIAKA KAZAA NA HAO WASITAAFU WAKO WAKAPIGWA BANI HATARI. Acha kucheza na Amiri jeshi mkuu
Hata ccm wako hapo kwa sababu ya Majeshi yetu. Acha ushamba kabisaa
 
Tukutane Moshi tarehe 20 July
IMG_20190718_121930.jpeg
 
Ukweli na utuweke huru. JPM kulikuwa hamna namna ili kuikoa CCM kipindi kile na kuwaokoa hawa wanao jaribu kumhujumu sasa ilibi awe ndiye chaguo la Urais wa JMT. Haja hiyo bado iko palepale na imeongezeka uzito zaid sasai kuliko wakati mwengine wowote kutokana na utendaji wa Rais mwenyewe JPM

Hakuna ukiondoa Mkapa, kati ya wote wanao jaribu kumhujumu, aliye fikiria iko siku JPM atakuwa Rais. Ndio maana Kinana na Nape wamedhihirisha jinsi wanavyomchukulia JPM. Yaani kwao ni mshamba flani hivi, aliyechanganyikiwa nk nk. Kila kejeli unayo weza kuifikiria ndivyo wanavyo muona wao na genge la aina yao.

Lakini jambo la ajabu zaidi ni wao wanapofikiria eti ni sehemu ya kumfikisha JPM hapo alipo wakati kimsingi walio mfikisha hapo alipo pengine hata maadili ya kazi zao haya waruhusu kujitaja. Wana siasa ni watu wa ajabu sana linapo kuja suala la kutafuta sifa binafsi. Wanasema JPM kakabidhiwa kupaua nyumba. Wanachosahau ni nyumba yenyewe ilivyokuwa na cracks mpaka kwenye msingi. JPM amelazimika na anaendelea kuzikarabati nyufa hizo ili paa analojenga lisiangushe hiyo inayoitwa nyumba aliyoikabidhiwa kuipaua.

JPM, ndio walikuwa hawa namna nyengine, na walilazimika kumuweka mgombea wao wa CCM 2015 kama ambavyo wanalazimika kuwa ataendelea kama Rais wa JMT wapende wasipende.

Ukisikiliza clip yao ni watu walio jawa na hofu kuu juu ya mstakabali wao. Hiyo clip yao imesha backfire kinachosubiriwa na wengi sasa ni nini consequences juu yao na kwa kiasi gani?

Ni ujinga kumlinganisha JPM na Jumbe. JPM analinganishwa na Nyerere tena na watu wengi mno ndani na nje ya Tanzania. Tena watu wenye hekima na akili zao. Kinyume chake Nape, Kinana nawa aina yao wasubiri kufuata Jumbe's(rip) course.
CCM niijuavyo Mimi haijawahi kukosa mgombea hasa katika nafasi ya uraia walikuwepo watu safi akina Jaji Ramadhani Augustine lakini walipendekeza Magufuli ntachukua nchi sababu kuu ni ule utii alioonesha kwa wazee wa chama wakati akiwa waziri tofauti na Lowassa Kama unakumbuka mwenyekiti wakati wa JK Alikua Nani 2010 wakati JK anatafuta kipindi Cha pili don't play with CCM
 
Dhumuni la andiko lako kwa jicho la tatu unachochea nape akatwe,maana unajua m/kiti uwezo huo anao na akiamua hamna wa kuleta fyoko,please usimjaribu ndugu huyu.
Dhumuni langu ni kuleta maridhiano kuliko mashindano na kiburi
Nataka kusema usitukanw mamba hujavuka mto bado safari 2020
 
Weweee.. unazani mkimtoa ndio kazi imeishia hapo? KUMBUKA RAIS ANWEZA AKATANGAZA HARI YA HATARI AKAA IKULU MIAKA KAZAA NA HAO WASITAAFU WAKO WAKAPIGWA BANI HATARI. Acha kucheza na Amiri jeshi mkuu
Hata ccm wako hapo kwa sababu ya Majeshi yetu. Acha ushamba kabisaa
Ndugu zamani Miaka ya 70 nilipokua mdogo nilikupa na mawazo Kama yako Ila baadae nikagundua kuwa CCM ni Dude kubwa kuliko ukubwa wenyewe
Mwalimu aliisuka CCM kwa namna ya pekee hakuna mkubwa kuliko CCM hapa Tanzania waulize wapinzani 2015 pamoja na vulugu zote lakini mwishowe wakawa Kimya na nchi inasonga Mbele
 
1.0 NAPE NI NANI KATIKA SIASA ZA MAGUFULI
Hapo awali Rais Magufuli alimteua Ndugu Nappe Nauye kuwa waziri wa habari ifahamike Kuwa Nappe Nauye alikua ni Mwenezi wa Chama Cha CCM kabla ya kupata wadhifa huo wa uwaziri ambao baadae ulitoweka baada ya kutaka kuingilia mgogoro Kati ya Mkuu wa Mkoa wa dar es salaam Paul Makonda na kituo Cha habari Cha clouds.

Baada ya Nappe kuondolewa katika nafasi ya uwaziri kulikuwa na maneno maneno kutoka kwa Wadau mbalimbali wa siasa nchini wengine wakisema alipewa uwaziri baada ya Rais kushinikizwa na wakongwe ndani ya chama, wengine wakisema halikua chaguo la Rais, wengine wakisema amefanya makosa kukosana na mwana wa mfalme (Makonda) wengine wakisema alionekana kwenda kinyuma au kupingana na Rais kwa baadhi ya vitu kitu ambacho kilipelekea Rais kumuondoa kwa haraka

Tukiangalia haiba ya Nappe ni mtu mwenye kujiamini, anamaono na anasimamia anacho kiamini hili limetokea hata akiwa UVCCM amewahi kukwaruzana na ndugu Lowassa na hatimae alimshinda simaanishi Kuwa Nnguvu ya Nappe ndio ilimshinda Lowassa bali mtandao ambao Nappe alikuwemo kama spika ndani yake kwa bahati mbaya na marazote Nappe amekuwa akitumika dhidi ya kile kinachoonekana kutokubalika na JK na kundi lake tujikumbushe kidogo kampeni ya Vua Gamba

Nappe amewahi kufanya makosa kadhaa hasa alipotumika kufanya njama kuzima bunge live baada ya miezi kadhaa akiwa waziri aligundua kuwa mpango Ule haukua kwa maslahi mapana ya nchi bali kuijengea nguvu taasisi ya Urais na Rais mwenyewe tofauti na kile kilicho aminishwa na waziri Mkuu Majaliwa kuwa wananchi wafanye Kazi.

2.0. SASA TURUDI KINACHOENDELEA HIVI SASA
2.1. Kumekuwa na Hoja ama vihoja vya kumfanya Rais wa Sasa kuwa Kama Mungu mtu yaani untouchable na genge linalonufaika na mfumo wa utawala wa Sasa likiongozwa na RC Makonda na genge lake yaani Musiba, Jerry Mulo, Lemutuz ma RC ma DC nawengine

2.2 Kumekuwa na kile kinachoitwa CCM MPYA ambao wameeneza propaganda kuwa CCM ya awamu zilizopita hazikufanya lolote hivyo kuwadhalilisha waziwazi wale waliotangulia

2.3. Kumekuwa na mpango au mkakati wa kuongeza muda wa Urais na Ubunge harakati hizi zimekuwa zikiibuliwa na kuzimwa tumemuona Nkamia na wabunge wengine wakitumika Kama Spika katika mpango huu

2.4. Kumekuwa na tetesi kuwa mpango wa kuongeza muda wa Urais unaratibiwa na rais wa Rwanda ndugu Paul Kagame ambae alikua hasimu wa Rais kikwete alipokuwa Madarakani

2 5. Kumekuwa na hatua za kununua wapinzani ama kuwapa Ubunge ama vyeo kwa maslahi ya kufanikisha njama hii na kuongeza ungwaji mkono ndani ya CCM

2.6. Kumekuwa na HOFU juu ya usalama wa Rais hasa katika mkakati wa kutekeleza adhma hii ya kuongeza muda wa urais ambapo pamoja na juhudi zinazifanyika inatakiwa njia ya kuwadhoofisha wakuu waliotangulia hasa JK, Mkapa na Kinana hawa ambao wanaonekana wanaweza kuzuia njama hii.

2.7. Kumekuwa na wasiwasi kuwa Rais anaaminiwi tena na wakuu waliotangulia hasa ukizingatia Mambo yanayoendelea nchini katika Uchumi, kutekana, matukio ya mauaji na makatazo ya kisiasa hivyo kutengeneza kitu kinaitwa kundi la Benard Membe ndani ya CCM linaloendeshwa kwa ufanisi mkubwa na kijana Nappe Nauye mwana mikakati

3.0 KUIBUKA GHAFLA KWA WASTAAFU/WAZEE
Sasabasi tukiangalia kilichotekea baada ya Musiba kuanzisha makelele dhidi ya waliokuwa makatibu wakuu CCM yaani Kanali Mstaafu Kinana na Luteni Makamba tunaona reaction ya moja kwa moja kwa balaza la wazee wa CCM ambapo barua yao imeonesha kuna kitu watuhumiwa yaani Musiba na Mtu mwenye Kinga (hapa wanamaanisha Rais) wanatuhumiwa kuwachafua kwa malengo fulani ya kisiasa (hawakutaja ni malengo gani hayo ya kisiasa! Labda niyale niliyotaja hasa ya kuongeza muda wa kipindi cha Urais) utaona kuna mpango wa kutokubalika ama kutoelewana Kati ya viongozi wa Sasa na wale waliotangulia.

Ingawa viongozi waandamizi kama JK na Mkapa wako kimya inaonesha kuwa wanajua kinachoendelea hivyo wako Kimya kimkakati akina Kinana na Makamba wameachiwa waanzishe zogo

Pia inaonesha kuwa kuna jitihada za kuwalinda vijana waliokulia katika CCM ambao hawakubaliana na kupanga njama ya kuongeza muda wa Urais Kama akina Nappe, January, Mwigulu, nk. ambao inaonesha wanaweza kukatwa majina na mwenyekiti wao Rais Magufuli hivyo kukimbilia kulia kwa wazee wastaafu Kama Jakaya na Kinana

4.0 KWANINI MAGUFULI ANAPASWA KUMUHESHIMU NAPPE
Ingawa Nappe ni mdogo ameonekana akiaminiwa Sana na wastaafu yaani wanamwamini pasi na shaka yoyote kwaio anachokiratibu Nappe kwa lugha nyingine sio Nappe bali katumwa na wastaafu au wazee wa CCM kutokana na matishio ambapo kwa sasa ni dhahiri kuwa Mwenyekiti Magufuli atalikata jina la Nappe katika majina ya wagombea Ubunge ndani ya chama imepelekea wazee wanao mwamini Nappe kuingilia Kati na kutaka kuhatarisha hata nafasi ya Mwenyekiti Magufuli hapa nikusema ukicheza na mtoto wa Simba unakuwa mnamchezea Simba mwenyewe

Kutokana na sababu kuu ya kutaka kubaki Madarakani baada ya muda wake kuisha kunapelekea kuhatarisha ustawi na taharuki kwa tabaka la Vijana walio kulia na kuishi CCM ambao baadhi Yao wanandoto za kuwa maraisi na viongozi wakubwa siku za usoni Kama January Makamba Ridhiwani Kikwete, Mwigulu Nchemba Nappe nawengine hivyo kusababisha wazee kutaka kumuondoa Magufuli kwa sababu wanaona baada ya wao kupoteza NGUVU kabisa hawataweza kumdhibiti Nappe amepewa kazi ya ukachero katika hoja hii.

5. NAFASI YA MKAPA NA JK KATIKA WARAKA WA KINANA NA MAKAMBA

Kutokana na ukaribu wa hawa watu Kuna uwezekano mkubwa wakamkata Jina Magufuli uchaguzi ujao na kumpitisha Benard Membe sababu kuu ni njama za Magufuli kung'ang'ania madaraka, njama ya kuhatarisha usalama wao ambapo hawana uhakika kuwa wako salama kwa sasa pia kutokana na kuona vizazi vyao vinaishia kuwa watumishi badala ya tabaka tawala hivyo hawatakubali kumpa muda zaidi hata kwa dawa.
Tukumbuke kuwa licha ya Mzee Mwinyi kutokutajwa Kama mtu mwenye maamuzi katika CCM ni dhahiri hawezi kupingana na hoja za MKAPA (napenda kumwita mtaalamu) ambapo nyuma yake atakuwepo Pius Masekwa AKA Roho Ngumu, Warioba, Salim endapo wakitaka kumuondoa Magufuli Madarakani Ni Jambo la Dk 2 tuu
Pia JK ambapo nyumayake atakuwepo Kinana (master planner), Makamba Yusuph (king'amuzi) Karume, mzee Pinda (mafia) na Dr. Shein kwa aina io ya wajumbe Magufuli atambue kuwa pamoja ya kuwa yeye ni amiri jeshi Mkuu Kuna wakuu wake ambao wakinusa harufu ya kuhatarisha usalama wa nchi wanaweza kumla kichwa yaani akakatwa jina Kama anavopanga kuwakata akina Nappe na watu wanao mpinga ndani ya CCM

6.0. MAGUFULI AFANYE NINI
1. Aachane na mpango wa kutaka kubaki Madarakani au kuongeza muda wa Urais kama inavyodaiwa na wazee wajiridhishe pasi na Shaka kuwa hakuna mpango huo
2. Awadhibiti wanaharakati wake akina Musiba na Makonda ambao wamekuwa wakitoa maneno ya hovyo kwa viongozi waliopita na waliopo Madarakani
3. Aachane na mpango wake wa kutaka kumuondoa Nappe na Vijana wengine wa JK ndani ya CCM ni dhahili JK na Kinana hawawezi kukubali hili litokee
4. Amtafutie Kazi Benard Membe ili awenae karibu Kama njia ya kumdhibiti
5. Arekebishe uchumi na akomeshe matukio ya kutekana

7.0. ASIPOFUATA USHAURI HUU NINI KITATOKEA
1. Magufuli ataendelea na kile kinachoitwa kuongeza muda wa Uraisi hapa ndio jina la Benard Membe litakapokuwa linaangaliwa kwa jicho la karibu na wazee ambapo anaeweza kukatwa na baadae kupewa Membe imewahi tokea kwa Jumbe alivyo ikosea CCM aliitwa na Kisha akaambia amestaafu Urais hiyo ndio CCM ndio maana ya ule wimbo CCM inawenyewe
2. Magufuli anaweza kukatwa jina endapo akiwakata akina Nappe sababu baba zao hawezi kukubali wakupe Kazi Kisha uwafukuze kazi wanae
3. Magufuli asipodhibiti akina Musiba ataendelea kuimarisha uhasama na wazee wa CCM ambapo kwa ya oa vijana watataka kuendelea kuwadhalilisha ama kwa kurekodi maongezi, picha za ngono nk.. sababu ndio tabia yao hivyo itapelekea uhasama kushamiri na kufika 2020 jina Magufuli halitarud mtaani
Tujikumbushe ile koras wanqimba "CCM Inawenyewe"
Napenda kuwasilisha
Kwenye mapendekezo yako ya nini Magufuli afanye namba 4 na 5, akilifanta na asipolifanya haponi yaani kifupi akisimama nchale akikaa nchale.

Mbinu pekee aliyobaki nayo ni hiyo ya kutuma vijana wake wa Tissccm kuteka, kuua, kutesa na kupoteza, ukumbuke mbinu hii ilikuwa ni last resort, kwa siasa tu Chadema ilikuwa imeshamlaza chini kumbuka uchaguzi wa 2015 na chaguzi zingine za marudio 2016 na 2017.

So far so now Magufuli has no any good option.
 
Aiseeee
Tuwe wawazi tu kwamba yaani CCM imkate jina Rais aliyeko madarakani ambaye kwa wakati huo Jaji Mkuu, Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, IGP, Mkuu wa Majeshi, Mkurugenzi TISS...wote wa ariport kwake.

Na kumbuka kipindi hicho cha hiyo mikutano jamaa ana power zote... mnaweza mkaingia mkutanoni kwa mbwembwe kisha mkatokea mlango wa kuingilia segelea kwa muda.. .haijalishi uwe mstaafu ama lah
 
CCM niijuavyo Mimi haijawahi kukosa mgombea hasa katika nafasi ya uraia walikuwepo watu safi akina Jaji Ramadhani Augustine lakini walipendekeza Magufuli ntachukua nchi sababu kuu ni ule utii alioonesha kwa wazee wa chama wakati akiwa waziri tofauti na Lowassa Kama unakumbuka mwenyekiti wakati wa JK Alikua Nani 2010 wakati JK anatafuta kipindi Cha pili don't play with CCM


Kumbuka JPM ndiye Rais. CCM hawana kitu bila ya Rais inikumbeti na vyombo vya Dola. Ni mwendawazimu anaye fikiri atachezea sharubu za Rais wa nchi kama Tanzania. Yaani hata hao Marais Wastaafu wanajua huu ukweli mchungu kuumeza.
 
Mkuu ccm inawenyewe, mfumo wa ccm iliundwa kimahususi sana, unawezaa ukawa amiri jeshi Mkuu lakini ukashindwa nguvu na majabali wa chama.....hao wazee ambao ni wastaafu wananguvu kubwaaa sana ndani ya mfumo wa chama na serikali na hii yote nyerere aliona mbali kwambaa hata ukiwa raisi kuwepo na watu wa kukudhibiti ndani ya mfumo wa chama na nje.
Nje ya mfumo wa chama. Nani atathubutu kumdhibiti Magufuli ?
 
Ndugu zamani Miaka ya 70 nilipokua mdogo nilikupa na mawazo Kama yako Ila baadae nikagundua kuwa CCM ni Dude kubwa kuliko ukubwa wenyewe
Mwalimu aliisuka CCM kwa namna ya pekee hakuna mkubwa kuliko CCM hapa Tanzania waulize wapinzani 2015 pamoja na vulugu zote lakini mwishowe wakawa Kimya na nchi inasonga Mbele
Kumbuka 2015 ccm mulikuwa hamsemi chagua ccm. Mulisema chagua Magufuli mchapakazi.
Acheni masihara nyie watu. Kila kitu na zama zake. CCM inaelekea mwisho.
 
Ndugu zamani Miaka ya 70 nilipokua mdogo nilikupa na mawazo Kama yako Ila baadae nikagundua kuwa CCM ni Dude kubwa kuliko ukubwa wenyewe
Mwalimu aliisuka CCM kwa namna ya pekee hakuna mkubwa kuliko CCM hapa Tanzania waulize wapinzani 2015 pamoja na vulugu zote lakini mwishowe wakawa Kimya na nchi inasonga Mbele


Wewe hujui kuwa hata Nyerere mwenyewe ilifika wakati akawa hana namna nyengine zaidi ya kujisubmitt kwa inikumbeti mkt na Rais!!! Ingawaje alifurukuta kiasi kwa Mzee Ruksa baadaye akapatiwa mwarobani wake.
 
Hujui nchi hii wewe . Nakushauri usianze kuandika wakati ushakuwa biased
1.0 NAPE NI NANI KATIKA SIASA ZA MAGUFULI
Hapo awali Rais Magufuli alimteua Ndugu Nappe Nauye kuwa waziri wa habari ifahamike Kuwa Nappe Nauye alikua ni Mwenezi wa Chama Cha CCM kabla ya kupata wadhifa huo wa uwaziri ambao baadae ulitoweka baada ya kutaka kuingilia mgogoro Kati ya Mkuu wa Mkoa wa dar es salaam Paul Makonda na kituo Cha habari Cha clouds.

Baada ya Nappe kuondolewa katika nafasi ya uwaziri kulikuwa na maneno maneno kutoka kwa Wadau mbalimbali wa siasa nchini wengine wakisema alipewa uwaziri baada ya Rais kushinikizwa na wakongwe ndani ya chama, wengine wakisema halikua chaguo la Rais, wengine wakisema amefanya makosa kukosana na mwana wa mfalme (Makonda) wengine wakisema alionekana kwenda kinyuma au kupingana na Rais kwa baadhi ya vitu kitu ambacho kilipelekea Rais kumuondoa kwa haraka

Tukiangalia haiba ya Nappe ni mtu mwenye kujiamini, anamaono na anasimamia anacho kiamini hili limetokea hata akiwa UVCCM amewahi kukwaruzana na ndugu Lowassa na hatimae alimshinda simaanishi Kuwa Nnguvu ya Nappe ndio ilimshinda Lowassa bali mtandao ambao Nappe alikuwemo kama spika ndani yake kwa bahati mbaya na marazote Nappe amekuwa akitumika dhidi ya kile kinachoonekana kutokubalika na JK na kundi lake tujikumbushe kidogo kampeni ya Vua Gamba

Nappe amewahi kufanya makosa kadhaa hasa alipotumika kufanya njama kuzima bunge live baada ya miezi kadhaa akiwa waziri aligundua kuwa mpango Ule haukua kwa maslahi mapana ya nchi bali kuijengea nguvu taasisi ya Urais na Rais mwenyewe tofauti na kile kilicho aminishwa na waziri Mkuu Majaliwa kuwa wananchi wafanye Kazi.

2.0. SASA TURUDI KINACHOENDELEA HIVI SASA
2.1. Kumekuwa na Hoja ama vihoja vya kumfanya Rais wa Sasa kuwa Kama Mungu mtu yaani untouchable na genge linalonufaika na mfumo wa utawala wa Sasa likiongozwa na RC Makonda na genge lake yaani Musiba, Jerry Mulo, Lemutuz ma RC ma DC nawengine

2.2 Kumekuwa na kile kinachoitwa CCM MPYA ambao wameeneza propaganda kuwa CCM ya awamu zilizopita hazikufanya lolote hivyo kuwadhalilisha waziwazi wale waliotangulia

2.3. Kumekuwa na mpango au mkakati wa kuongeza muda wa Urais na Ubunge harakati hizi zimekuwa zikiibuliwa na kuzimwa tumemuona Nkamia na wabunge wengine wakitumika Kama Spika katika mpango huu

2.4. Kumekuwa na tetesi kuwa mpango wa kuongeza muda wa Urais unaratibiwa na rais wa Rwanda ndugu Paul Kagame ambae alikua hasimu wa Rais kikwete alipokuwa Madarakani

2 5. Kumekuwa na hatua za kununua wapinzani ama kuwapa Ubunge ama vyeo kwa maslahi ya kufanikisha njama hii na kuongeza ungwaji mkono ndani ya CCM

2.6. Kumekuwa na HOFU juu ya usalama wa Rais hasa katika mkakati wa kutekeleza adhma hii ya kuongeza muda wa urais ambapo pamoja na juhudi zinazifanyika inatakiwa njia ya kuwadhoofisha wakuu waliotangulia hasa JK, Mkapa na Kinana hawa ambao wanaonekana wanaweza kuzuia njama hii.

2.7. Kumekuwa na wasiwasi kuwa Rais anaaminiwi tena na wakuu waliotangulia hasa ukizingatia Mambo yanayoendelea nchini katika Uchumi, kutekana, matukio ya mauaji na makatazo ya kisiasa hivyo kutengeneza kitu kinaitwa kundi la Benard Membe ndani ya CCM linaloendeshwa kwa ufanisi mkubwa na kijana Nappe Nauye mwana mikakati

3.0 KUIBUKA GHAFLA KWA WASTAAFU/WAZEE
Sasabasi tukiangalia kilichotekea baada ya Musiba kuanzisha makelele dhidi ya waliokuwa makatibu wakuu CCM yaani Kanali Mstaafu Kinana na Luteni Makamba tunaona reaction ya moja kwa moja kwa balaza la wazee wa CCM ambapo barua yao imeonesha kuna kitu watuhumiwa yaani Musiba na Mtu mwenye Kinga (hapa wanamaanisha Rais) wanatuhumiwa kuwachafua kwa malengo fulani ya kisiasa (hawakutaja ni malengo gani hayo ya kisiasa! Labda niyale niliyotaja hasa ya kuongeza muda wa kipindi cha Urais) utaona kuna mpango wa kutokubalika ama kutoelewana Kati ya viongozi wa Sasa na wale waliotangulia.

Ingawa viongozi waandamizi kama JK na Mkapa wako kimya inaonesha kuwa wanajua kinachoendelea hivyo wako Kimya kimkakati akina Kinana na Makamba wameachiwa waanzishe zogo

Pia inaonesha kuwa kuna jitihada za kuwalinda vijana waliokulia katika CCM ambao hawakubaliana na kupanga njama ya kuongeza muda wa Urais Kama akina Nappe, January, Mwigulu, nk. ambao inaonesha wanaweza kukatwa majina na mwenyekiti wao Rais Magufuli hivyo kukimbilia kulia kwa wazee wastaafu Kama Jakaya na Kinana

4.0 KWANINI MAGUFULI ANAPASWA KUMUHESHIMU NAPPE
Ingawa Nappe ni mdogo ameonekana akiaminiwa Sana na wastaafu yaani wanamwamini pasi na shaka yoyote kwaio anachokiratibu Nappe kwa lugha nyingine sio Nappe bali katumwa na wastaafu au wazee wa CCM kutokana na matishio ambapo kwa sasa ni dhahiri kuwa Mwenyekiti Magufuli atalikata jina la Nappe katika majina ya wagombea Ubunge ndani ya chama imepelekea wazee wanao mwamini Nappe kuingilia Kati na kutaka kuhatarisha hata nafasi ya Mwenyekiti Magufuli hapa nikusema ukicheza na mtoto wa Simba unakuwa mnamchezea Simba mwenyewe

Kutokana na sababu kuu ya kutaka kubaki Madarakani baada ya muda wake kuisha kunapelekea kuhatarisha ustawi na taharuki kwa tabaka la Vijana walio kulia na kuishi CCM ambao baadhi Yao wanandoto za kuwa maraisi na viongozi wakubwa siku za usoni Kama January Makamba Ridhiwani Kikwete, Mwigulu Nchemba Nappe nawengine hivyo kusababisha wazee kutaka kumuondoa Magufuli kwa sababu wanaona baada ya wao kupoteza NGUVU kabisa hawataweza kumdhibiti Nappe amepewa kazi ya ukachero katika hoja hii.

5. NAFASI YA MKAPA NA JK KATIKA WARAKA WA KINANA NA MAKAMBA

Kutokana na ukaribu wa hawa watu Kuna uwezekano mkubwa wakamkata Jina Magufuli uchaguzi ujao na kumpitisha Benard Membe sababu kuu ni njama za Magufuli kung'ang'ania madaraka, njama ya kuhatarisha usalama wao ambapo hawana uhakika kuwa wako salama kwa sasa pia kutokana na kuona vizazi vyao vinaishia kuwa watumishi badala ya tabaka tawala hivyo hawatakubali kumpa muda zaidi hata kwa dawa.
Tukumbuke kuwa licha ya Mzee Mwinyi kutokutajwa Kama mtu mwenye maamuzi katika CCM ni dhahiri hawezi kupingana na hoja za MKAPA (napenda kumwita mtaalamu) ambapo nyuma yake atakuwepo Pius Masekwa AKA Roho Ngumu, Warioba, Salim endapo wakitaka kumuondoa Magufuli Madarakani Ni Jambo la Dk 2 tuu
Pia JK ambapo nyumayake atakuwepo Kinana (master planner), Makamba Yusuph (king'amuzi) Karume, mzee Pinda (mafia) na Dr. Shein kwa aina io ya wajumbe Magufuli atambue kuwa pamoja ya kuwa yeye ni amiri jeshi Mkuu Kuna wakuu wake ambao wakinusa harufu ya kuhatarisha usalama wa nchi wanaweza kumla kichwa yaani akakatwa jina Kama anavopanga kuwakata akina Nappe na watu wanao mpinga ndani ya CCM

6.0. MAGUFULI AFANYE NINI
1. Aachane na mpango wa kutaka kubaki Madarakani au kuongeza muda wa Urais kama inavyodaiwa na wazee wajiridhishe pasi na Shaka kuwa hakuna mpango huo
2. Awadhibiti wanaharakati wake akina Musiba na Makonda ambao wamekuwa wakitoa maneno ya hovyo kwa viongozi waliopita na waliopo Madarakani
3. Aachane na mpango wake wa kutaka kumuondoa Nappe na Vijana wengine wa JK ndani ya CCM ni dhahili JK na Kinana hawawezi kukubali hili litokee
4. Amtafutie Kazi Benard Membe ili awenae karibu Kama njia ya kumdhibiti
5. Arekebishe uchumi na akomeshe matukio ya kutekana

7.0. ASIPOFUATA USHAURI HUU NINI KITATOKEA
1. Magufuli ataendelea na kile kinachoitwa kuongeza muda wa Uraisi hapa ndio jina la Benard Membe litakapokuwa linaangaliwa kwa jicho la karibu na wazee ambapo anaeweza kukatwa na baadae kupewa Membe imewahi tokea kwa Jumbe alivyo ikosea CCM aliitwa na Kisha akaambia amestaafu Urais hiyo ndio CCM ndio maana ya ule wimbo CCM inawenyewe
2. Magufuli anaweza kukatwa jina endapo akiwakata akina Nappe sababu baba zao hawezi kukubali wakupe Kazi Kisha uwafukuze kazi wanae
3. Magufuli asipodhibiti akina Musiba ataendelea kuimarisha uhasama na wazee wa CCM ambapo kwa ya oa vijana watataka kuendelea kuwadhalilisha ama kwa kurekodi maongezi, picha za ngono nk.. sababu ndio tabia yao hivyo itapelekea uhasama kushamiri na kufika 2020 jina Magufuli halitarud mtaani
Tujikumbushe ile koras wanqimba "CCM Inawenyewe"
Napenda kuwasilisha
 
Mwenyekiti wa CCM taifa = mmiliki wa Chama
Kuna wakati Magufuli ni mgombea kama wagombea wengine Sasa wenye chama wanajua wafanye nini kwa tabia za wazee wa CCM huwakimya Hadi mudawao ufike yaani unaweza kuwanyanyasa lakini wanakusubiri zamu yao ifike
Pia wako smart wanaweza kutumia demikrasia kukutoa Tena tukiwa Live media zote zinaona kitu ambacho kitasababisha endapo Rais atatumia Nguvu Basi atapoteza waungwaji mkono
CCM sio mwenyekiti wa chama hata Kikwete alimtaka Membe mwisho wenye CCM wakampa Magufuli
 
Tuwe wawazi tu kwamba yaani CCM imkate jina Rais aliyeko madarakani ambaye kwa wakati huo Jaji Mkuu, Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, IGP, Mkuu wa Majeshi, Mkurugenzi TISS...wote wa ariport kwake.

Na kumbuka kipindi hicho cha hiyo mikutano jamaa ana power zote... mnaweza mkaingia mkutanoni kwa mbwembwe kisha mkatokea mlango wa kuingilia segelea kwa muda.. .haijalishi uwe mstaafu ama lah

Nonsense
 
Back
Top Bottom