Kuzuia chakula kwenda nje sio sahihi badala yake wenzetu wanapokuwa na njaa ndo fursa ya sisi kuzalisha kwa wingi ili kutosheleza soko. Watu wengi hasa wanaoishi vijijini wanashindwa kuzalisha mazao ya chakula kwa sababu hayana bei nzuri wakati garama pembejeo zinapanda kila siku,lakini kama tutafungua mipaka yetu chakula kitakuwa na bei nzuri na wakulima watazalisha kwa wingi kwakuwa itakua kilimo biashara badala ya sasa kilimo chakula.