Napenda sana mwanamke akilia

ALU255

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
2,089
Reaction score
2,126
sijui kama nina tatizo au vipi lakini sio siri yani nikimuona mwanamke analia huwa nafarijika sana huwa napatwa na huzuni usoni ila nahisi raha sana moyoni na huwa naenda kumbembeleza kama nipo nae karibu hapo ndo raha inaongezeka moyoni,jana nilipita mitaa flani nikamkuta mdada analia yuko pekeyake anasubiri daladala nikaona si vibaya nikamsogelea pale alipo nikamkuta anatokwa machozi hataki kusema tatizo ni nini basi nikambembeleza pale hadi raha yani kumbembeleza mwanamke hadi akanyamaza then nikamuuliza tatizo nini akasema mapenzi nikasema shit.!!
hadi leo sijajua tatizo langu akilia mtoto sipendi akilia mwanaume sipendi ila akilia mwanamke napenda sana nim'bembeleze
 
Wewe utakuwa enzi zako za utoto ulikuwa ukipigwa nambavu wa mtaani
kwenu unakimbilia kwa dada zako waka kuubembeleze badala ya kukomaa
na kutunisha msuli wako kwa vidume wenzio, sasa umeathirika sana
kisaikolojia mpaka sasa. na ndio maana una penda kupangusana machozi
na watoto wa kike tu...
 
Jamani huyu jamaa ni yeye interest zake na anapenda nn?, hata tusimshangae hapa tukiulizana tunapenda kitu gani mbona tutashangaana sana humu ndani??....

Hivi hamna mtu humu anaependa kumbembeleza msichana akilia, unamshika nywele zake then analalia kifuani kwako acheni hizo habary wadau

lakini akilia mtoto mbele yangu hata awe msichana mbona atajuta kukaa mbele yangu piga makofi

tukiulizana humu ndani wadau wote tunapenda nn mbona huyo jamaa anaafadhali

Am done...
 
una psychosocial problems
 

haha ha ha nimecheka sana
 

tatizo lako la kwanza ni kuwa hujaoa..
ukioa baada ya miezi miwili utakuja mwenyewe kuutoa huu uzi.
 
Mwanaume anayejua kubembeleza mzuri sana.Utakuta limtu limekosea limekuumizs hadi umelia hata kubembeleza halijui shit limekazana tu nisamehe mpenzi wangu bila vitendo ha!ha!ha.Kubembelezwa raha ati
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…