Nape mbona hukusema busara itumike kwa Maxence Melo?

Goliath mfalamagoha

JF-Expert Member
Aug 3, 2012
602
2,505
Mheshimiwa Nape, nimekusikiliza jana, nimekuelewa sana..., unataka busara ipi hiyo itumike katika kuwashughulikia hawa "wanaodaiwa kuhusika na biashara haramu ya dawa za kulevya"!? Leo Nape unataka utaratibu wa kisheria uzingatiwe.., umesahau mengi kwa haraka sana..,

sawa.., sasa unataka busara ipi itumike kupambana na hawa wasanii 'walioko chini yako' (wewe ni waziri wa sanaa) wanaojihusisha na biashara hii haramu!? Wakati ule (wewe) na wenzako kule Dodoma mnaungana kutunyima sisi raia wa Kawaida haki yetu ya kuwatazama wabunge wetu (wawakilishi) haki ya kutazama bunge Mubashara, kwanini haukutumia busara hiyo kusililiza kelele za watanzania wale!? (uliongozwa na busara ipi kuweka bunge gizani, licha ya watanzania wengi kusema hapana!?)

Leo unapata wapi nguvu za kusema kwamba "Brand ya wasanii wale inachafuliwa"!? Kwanini usione kwamba "Brand ya bunge inakufa kwa kuliweka bunge gizani"!? Hebu bwana Nape, acha bwana Marconder aendelee na sanaa zake (apate kiki) wakati huo wewe ukifanikisha mpango wa kurejesha bunge "mubashara" kwa watanzania..,

Swali rahisi sana kwako wewe bwana Nape, "unaweza kukumbuka, ni lini wewe umewahi kutoa tuhuma kwa namna inayolinda brand za watu?" umesahau wakati ule unarekebu Lowassa, umesahau vita yako na Dr Slaa.., leo unataka "busara itumike"..,

zile porojo zenu za "watanzania wafanye kazi" mara "kurusha matangazo ni gharama" zimepitwa na wakati (waswahili wanaita, uongo na ulaghai laini), ukishindwa hili, basi acha (Marconder) awashughulikie hawa (casts) wake katika filamu yake hiyo.., hauna "usafi" huo wa kusema "haki ifuatwe" wakati wewe ulitunyima haki yetu ya msingi ya kupata habari bwana Nape!

Pia.., kama issue ni busara na kushauri mamlaka na watawala kufuata sheria na taratibu.., wewe Nape, ungeomba, Busara pia katika ukamataji wa Magurudumu ya pikipiki zipitazo katika barabara za mwendokasi.., au kwa sababu wameguswa marafiki zako, sasa unaanza kuumia.., wauza unga wapewe utetezi, wale Bodaboda nani mtetezi wao kule "sentro"!?

NB; ingawa mimi mwenyewe, kwenye (maigizo) yenu haya, sina imani na yoyote kati yenu (wewe au Marconder), naona sasa mmeanza kuingiliana kwenye mistari yenu, piga miluziiiiii.., "mbwa" apotee njia, matokeo kidato cha 4, pale MZIZIMA vipiiii?
 
Kwa Melo nahisi alijisahau.Huenda sasa ameanza kuelewa nini maana ya Haki sawa kwa Wote.
 
Ni vizuri viongozi waanzishe tabia ya kuwakosoa wenzao au mwenendo wa Serikali wakiwa madarakani kama alivyofanya Nape badala ya kusubiri wakistaafu au kuhamia vyama vya Upinzani.
 
nape anatetea kitu hapo, maana yeye hiyo busara anayotaka itumike kimsingi hajawahi kuitumia, amkumbushe mkuu wa mkoa kuna kabinti kalikamatwa na mzigo mkubwa SA uwanja wa Oliver Tambo na kenyewe kakamatwe.
 
Nikikumbuka issue ya Max na ukimya wa Nape ndio ninaapo mdharau
 
Mheshimiwa Nape, nimekusikiliza jana, nimekuelewa sana..., unataka busara ipi hiyo itumike katika kuwashughulikia hawa "wanaodaiwa kuhusika na biashara haramu ya dawa za kulevya"!? Leo Nape unataka utaratibu wa kisheria uzingatiwe.., umesahau mengi kwa haraka sana..,

sawa.., sasa unataka busara ipi itumike kupambana na hawa wasanii 'walioko chini yako' (wewe ni waziri wa sanaa) wanaojihusisha na biashara hii haramu!? Wakati ule (wewe) na wenzako kule Dodoma mnaungana kutunyima sisi raia wa Kawaida haki yetu ya kuwatazama wabunge wetu (wawakilishi) haki ya kutazama bunge Mubashara, kwanini haukutumia busara hiyo kusililiza kelele za watanzania wale!? (uliongozwa na busara ipi kuweka bunge gizani, licha ya watanzania wengi kusema hapana!?)

Leo unapata wapi nguvu za kusema kwamba "Brand ya wasanii wale inachafuliwa"!? Kwanini usione kwamba "Brand ya bunge inakufa kwa kuliweka bunge gizani"!? Hebu bwana Nape, acha bwana Marconder aendelee na sanaa zake (apate kiki) wakati huo wewe ukifanikisha mpango wa kurejesha bunge "mubashara" kwa watanzania..,

Swali rahisi sana kwako wewe bwana Nape, "unaweza kukumbuka, ni lini wewe umewahi kutoa tuhuma kwa namna inayolinda brand za watu?" umesahau wakati ule unarekebu Lowassa, umesahau vita yako na Dr Slaa.., leo unataka "busara itumike"..,

zile porojo zenu za "watanzania wafanye kazi" mara "kurusha matangazo ni gharama" zimepitwa na wakati (waswahili wanaita, uongo na ulaghai laini), ukishindwa hili, basi acha (Marconder) awashughulikie hawa (casts) wake katika filamu yake hiyo.., hauna "usafi" huo wa kusema "haki ifuatwe" wakati wewe ulitunyima haki yetu ya msingi ya kupata habari bwana Nape!

Pia.., kama issue ni busara na kushauri mamlaka na watawala kufuata sheria na taratibu.., wewe Nape, ungeomba, Busara pia katika ukamataji wa Magurudumu ya pikipiki zipitazo katika barabara za mwendokasi.., au kwa sababu wameguswa marafiki zako, sasa unaanza kuumia.., wauza unga wapewe utetezi, wale Bodaboda nani mtetezi wao kule "sentro"!?

NB; ingawa mimi mwenyewe, kwenye (maigizo) yenu haya, sina imani na yoyote kati yenu (wewe au Marconder), naona sasa mmeanza kuingiliana kwenye mistari yenu, piga miluziiiiii.., "mbwa" apotee njia, matokeo kidato cha 4, pale MZIZIMA vipiiii?

Kati ya yao ambao anasema busara zitumike walishawahi kunaswa nchi za nje bahati nzuri/mbaya walinasuliwa na sasa tuna Rais ambaye hana masihara Dr Magufuli! Mungu katujalia na tumuombee sana awe na afya njema hasa kwa kipindi chake cha uongozi mpaka 2025, wanasiasa wengi watakimbua nchi/kazi just wait and see.
 
Amesahau alivyo waita wenzake mawaziri mizigo leo wanakula sahani moja.
 
Sasa kama anakula mzigo kwanini sheria zisifuate mkondo wake...?


Abiria analinda mzigo wake hapo
 
Nakumbuka jamaa alienda kuzindua app ya wema labda ana maslah fulan kwa spenga
 
Kumbuka unamuongelea aliyekua msemaji wa chama tawala na baadhi ya watuhumiwa walikua kwenye kampeni.

Hapo ndio utajua sheria zetu haziko sawa, zina macho zinaangalia ni nani ana hatia na nani hana hatia kutokana na alivyofungamana na chama tawala.
 
Umuhimu wa kufuata sheria na taratibu uonekana pale unapoguswa; yumkini alidhani kuwa hatokuja kuguswa na fagio la mwendo kasi lisilozingatia taratibu walizojiwekea wenyewe
 
Back
Top Bottom