Nape: CCM itashinda tu uchaguzi mkuu ujao hata kwa goli la mkono

EmmaGMangwela

Senior Member
May 11, 2015
139
53
Habari Jf..

Nape Nnauye Juzi akiwa Mkoani Kanda ya Ziwa aliwaambia CCM Ushindi ni Lazima hata kwa Goli la Mkono ili mradi tu Referee apulize Kipenga.

"Goli ni Goli tu Hata Kama ni la Kuotea"

Hapa Swali la Kujiuliza Je Referee wa Mechi ya CCM na UKAWA atatuvusha Salama?, Kwa Maana Team zote Zimejipanga Vilivyo na Washahabiki Safari hii Naona Hawanunuliki na Hawataki hata Jezi za BURE.

UKAWA Kazi Kwenu Sasa,Wananchi Hawatawasaidia Kulalamika na Kulialia Baada ya Mechi Kuisha Kwa Bao la Mkono wa Mungu.
 
Hizi kauli za Nape ni mbaya sana , mbaya zaidi kwenye Chama chake hakuna anayemkanusha. Zitakuja kuleta machafuko.

Kwa kauli hizi hata kama upinzani utashindwa Oktoba . Hata kama watashindwa kihalali sidhani kama watakubali.

Aina hii ya viongozi kama Nape sijui huwa wanafikiria nini.

Nafikiri Nape ni katibu mwenezi wa hovyo kuwahi kutokea kwenye CCM.
 
Hiyo kauli anairudia mara kwa mara, tume ya uchaguzi nayo imekaa kimya.
 
Nawashauri UKAWA hiyo kauli waitunze ipasvyo ili wakati wa kusubiri matokeo rafu ya aina yeyote ikichezwa likumbukwe hili NENO!!
 
Hivi tume ya Uchaguzi inakaaje kimya kwa kauli za uvunjifu wa sheria wa dhahiri kama hizi?
 
Kama kweli amesema hivyo ccm wamekwisha kuingiwa na hofu kwani wameona wanaojiandikisha kupiga kura wengi ni vijana waliopigika na wanaotaka mabadiliko. Hivyo tume ikichakachua kura au ikichelewesha kutangaza matokeo PATACHIMBIKA!
 
Mlitaka aseme vipi ilihali yeye yupo katika upande wa propaganda...mnajua kauli za kuleta machafuko zaidi ya" nchi hatatawalika"
 
upinzani wanatakiwa kwenye kampeni zao wakumbushie hili neno ili nguvu ya UMA walinde kura zao hakuna kulala ck hiyo :na huyo Nape akiendelea na hizo kaulu ajiandae kuwa mteja wa Bensouda .
 
Kwa sheria za football ukitumia mkono ni faulo inaweza sababisha penati au free kick na uliyetumia mkono unaweza pata kadi ya njano au kadi nyekundu. Labda refa apendelee upande mmoja
 
Nape ni kiongozi wa hovyo kuwahi kutokea Tanzania...

Anafanya siasa za kijima sana..

Sijui elimu aliyo nayo imemsaidiaje?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…