Napataje NIDA kwa haraka?

Napataje NIDA kwa haraka?

mbongombishi

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2014
Posts
593
Reaction score
309
Habarini wanajukwaa.
Nina ndugu yangu anarudi Tz Jumatano (tarehe 06/07/2022). Atakuwepo Tz kwa siku 10 tu.
Huyu ndugu ana uhitaji mkubwa wa Kitambulisho cha Taifa.
Naomba mnijuze mchakato wa yeye kuufanya pindi afikapo.
Akhsanteni.
 
Akiwa na vielelezo visivyo na shaka anaweza pata ila kwa kuchonga na ofisir wa NIDA ili taarifa zake ziuploadiwe fasta fasta
 
Inawezekana hata ndani ya siku 4 …ikifika zamu yake ya kupiga picha kabla ya kufanya hivo awaeleze shida yake..wanautaratibu wa kuwasaidia wenye utahitaji wa haraka
Mimi nilifanya hivo na nilifanikiwa
N.B: hii ni kwa namba tu kwa Kitambulisho sijajua
 
Nenda 7 7 maonyesho,Tafuta banda la Nida.
Ukilipata umekwisha.
Unachotakiwa kufanya,Piga picha za passport size,nenda serikali za mtaa wakupe barua ya utambulisho,kisha nenda stationary waambie wakupe form ya nida(,Kama hana,ana download kwny Website husika.)
Ukiipata hiyo jaza taarfa zako kwa usahihi ...kwny hiyo form.
Kisha nenda 7 7 maonyesho.
Utafute hilo banda watashughulika na hitaji lako.
Usiniulize swali maana mm mwenyewe nimeambiwa tu,ila aliyenambia yy alipata.
Hakua nacho tangu mchakato umeanza na amesumbuka sana lkn awamu hii kapata.
 
Inawezekana hata ndani ya siku 4 …ikifika zamu yake ya kupiga picha kabla ya kufanya hivo awaeleze shida yake..wanautaratibu wa kuwasaidia wenye utahitaji wa haraka
Mimi nilifanya hivo na nilifanikiwa
N.B: hii ni kwa namba tu kwa Kitambulisho sijajua
Vitambulisho unatengenezewa ukiwa na namba ya NIDA ni Elfu ishirini Tu Buguruni rozana hapa
 
Vipi ushafanikiwa mkuu?? kuna mtumishi mwenzetu ana changamoto ya majina katika NIDA yake
 
Wakuu mwenye kuelewa, mimi walikosea spelling ya jina langu nifanyeje? Taratibu za kufuata ni zipi?
 
Back
Top Bottom