Naongea na wewe Serikali

Masalu Jacob

JF-Expert Member
Jul 26, 2017
948
1,092
Habari Tanzania.

Napenda kuongea na Serikali kuhusu tatizo la ajira nchini. Serikali na wadau wachache wamekuwa wakihimiza sana vijana wajiajiri baada ya kuhitimu vyuo vikuu nk. (Hawa ndio haswa wahanga wa tatizo hili kwa asilimia kubwa kutokana na mfumo husika wa elimu yetu).

1. Hivi Serikali mnakumbuka wazo na lengo lililopelekea kuanzishwa kwa taasisi ya VETA hapa nchini? Au pengine hamjui?

2. Hivi Serikali mnajua wazo na lengo mahususi la kuanzishwa mitihani ya darasa la nne, darasa la saba, kidato cha pili, kidato cha nne na kidato cha sita hapa nchini? Au mnadhani ni utaratibu umejikuta upo katika elimu yetu baada ya kuukopa mahali?

3. Hivi Serikali mnajua wazo na lengo la kuanzishwa vyuo vya kati na vyuo vikuu katika taifa la Tanzania? Au mnadhani ni fashion baada ya kuona baadhi ya viongozi waliokuwepo madarakani enzi hizo watoto wao kutokukidhi matakwa na kukosa sifa katika mfumo husika ndio tatizo lilipoanzia? Sijui kama mnajua haya mambo lakini?

4. Sijui mnakumbuka tatizo lililojitokeza kuhusu mahakama za mwanzo na wilaya kuhusu chuo cha Sheria Lushoto Tanga na janga la wahitimu wa shahada ya Sheria hapa nchini? Sijui kipindi cha awamu ya Nne kurudi nyuma mlipojadili bungeni hivi hamkuona hili tatizo kwa fani nyingine? Ubaya wote mlikuwepo.

5. Je, mlishafanya tafiti kuhusu uhitaji wa elimu ya shahada na shahada ya uzamivu kama zina umuhimu hapa Afrika sio Tanzania tu au tunaona fashion kuitwa wasomi nk?

NB:

Nawaomba sana mtafute taarifa na maarifa ya miaka ya nyuma tangu nchi inapata Uhuru viongozi waliopita walifanya nini mazuri mtakuwa na mwanzo mzuri wa kujifunza. Agalo la kale ni kinga kwa agano jipya.

Serikali yoyote hapa duniani ni kama mfano wa siku tu maana jinsi ilivyo leo inakuja na kesho inaenda zake. Siku iliyo nzuri ya kuikumbuka ni ile iliyokupa alama nzuri sana maishani mwako.
 
Ajira kesho kutwa zitamwaga na watumishi posho itaongezwa na madaraja watopandishwa .
Hii ni njia mojawapo ya kufanya akubalike wakati wakuomba kura
 
Ajira kesho kutwa zitamwaga na watumishi posho itaongezwa na madaraja watopandishwa .
Hii ni njia mojawapo ya kufanya akubalike wakati wakuomba kura
Hiyo sio njia nzuri brother. Tanzania hakuna tatizo la ajira kabisa. Taasisi zote nchini wanauhaba wa watumishi zaidi ya 53+% alafu bado wanaongea kinafki eti nafasi ni chache vijana wajiajiri na huku mambo hayaendi katika maofisi yao na mafanikio ni hafifu sana kutokana na uwezo mdogo uliopo wa watumishi katika taasisi.

Sio vizuri haitapendeza kuishi kisiasa hapa nchini ipo siku wao ndio watalia vijana wakianza kuwa wanasiasa maslai. Tutatengeneza tatizo kubwa sana la ustaafu wa hiyari kwa vijana wadogo ambao tutakuwa tumeingia gharama kuwahudumia.
 
Hiyo sio njia nzuri brother. Tanzania hakuna tatizo la ajira kabisa. Taasisi zote nchini wanauhaba wa watumishi zaidi ya 53+% alafu bado wanaongea kinafki eti nafasi ni chache vijana wajiajiri na huku mambo hayaendi katika maofisi yao na mafanikio ni hafifu sana kutokana na uwezo mdogo uliopo wa watumishi katika taasisi.

Sio vizuri haitapendeza kuishi kisiasa hapa nchini ipo siku wao ndio watalia vijana wakianza kuwa wanasiasa maslai. Tutatengeneza tatizo kubwa sana la ustaafu wa hiyari kwa vijana wadogo ambao tutakuwa tumeingia gharama kuwahudumia.
Katika hili mimi ningependa ubadilishwe mfumo wa ajira tanzania,mtu anapokuambia ujiajiri na hali yeye mwenyewe kaajiriwa na ana karibia miaka 30 kwenye ajira .kwa nini hao wazee walio tumikia taifa kwa zaidi ya miaka ishirini mawizarani wasiondoke na kuwaachia vijana fursa? Mana wao tayari wana mitaji na wameshajenga na wanafamilia tayari na uchumi wao lazima utakuwa stable.

Hoja yangu hapa ni kwa hao waajiriwa walio kaa kwenye ajira zaidi ya miaka kumi na tano na kuendelea,uwepo utaratibu wa kuachiana nafasi za kazi hasa pale unapokuwa umetumika kwa mda wa miaka kumi na mitano+ ,hii iko wazi kwamba unaweza kujiajiri kama wanavyotuimbia hiyo ngojera ya sisi vijana kujiajiri.kama umetumika serikalini kwa miaka 20 inatosha kuwaachia vijana na wewe ukajiajiri mana tayari mtaji unao na umeshapevuka kiakiri zaidi na sisi tutumie mgongo wa kuajiriwa mana sifa na utaalamu tunao kama hao waliopo kwenye ajira.

Nilimsiki kijana anaongea akiwa na bahasha yake ya kaki mkononi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpango uliopo kwa sasa ni huo ajira zitaambatanishwa na siasa kidogo
Hiyo sio njia nzuri brother. Tanzania hakuna tatizo la ajira kabisa. Taasisi zote nchini wanauhaba wa watumishi zaidi ya 53+% alafu bado wanaongea kinafki eti nafasi ni chache vijana wajiajiri na huku mambo hayaendi katika maofisi yao na mafanikio ni hafifu sana kutokana na uwezo mdogo uliopo wa watumishi katika taasisi.

Sio vizuri haitapendeza kuishi kisiasa hapa nchini ipo siku wao ndio watalia vijana wakianza kuwa wanasiasa maslai. Tutatengeneza tatizo kubwa sana la ustaafu wa hiyari kwa vijana wadogo ambao tutakuwa tumeingia gharama kuwahudumia.
 
Back
Top Bottom