Habari wana jukwaa.
Ni matarajio yangu kuwa mnaendelea vyema.
Leo katika kufuatilia kwangu kile kinachoendelea kwenye harakati za kuwapata wabunge na madiwani ndani ya chama tawala, nimefurahishwa na baadhi ya wananchi wa baadhi ya maeneo hapa kwa jinsi wanavyoonesha 'reaction' kwa waliokuwa wawakilishi wao na wanataka kuendelea kuwawakilisha!
Hawa hawa waliokuwa wanawaita wananchi wao "Kenge", eti wanataka waendelee kuaminiwa na wananchi ili wakishapata tena waendeleze matusi yao kwa raia. Hapana. Hili halikubaliki kabisa. Ndiyo maana wananchi wa baadhi ya sehemu binafsi wamenifurahisha sana.
Viongozi wote wanapaswa kufahamu kwamba nguvu yao inatoka kwa hao wanaowaita Kenge. Hili linapaswa kueleweka vizuri kabisa kuanzia ngazi ya chini kabisa ya mjumbe wa mtaa hadi kwa Rais.
Unafiki wa kuwapenda "kenge" wakati wa kutafuta kura zao, hatutaki.
Tunamtaka kiongozi kama Hayati JPM ambaye kamwe hakuweza kuacha kusikiliza wanyonge (kenge) kwenye mikutano yake.
Hatutaki kiongozi ambaye hakutaka kuwasikiliza wanyonge wakati wa kipindi chake cha urithi (ushahidi upo).
Hatutaki viongozi wenye kaliba ya "mama wa kambo".
Wananchi wa Butiama mmenifurahisha sana.
Hili naomba lisiishie Butiama tu, liende pote palipokuwa na viongozi wa hovyo waliowaona wananchi wao kama "Kenge" tu.
Sasa wakati wa kenge kuonesha umuhimu wao, umefika.
NOTE:
Mh. Balozi Polepole, shikilia hapo hapo, tuko pamoja na wewe.
Mungu ibariki Tanzania
Ni matarajio yangu kuwa mnaendelea vyema.
Leo katika kufuatilia kwangu kile kinachoendelea kwenye harakati za kuwapata wabunge na madiwani ndani ya chama tawala, nimefurahishwa na baadhi ya wananchi wa baadhi ya maeneo hapa kwa jinsi wanavyoonesha 'reaction' kwa waliokuwa wawakilishi wao na wanataka kuendelea kuwawakilisha!
Hawa hawa waliokuwa wanawaita wananchi wao "Kenge", eti wanataka waendelee kuaminiwa na wananchi ili wakishapata tena waendeleze matusi yao kwa raia. Hapana. Hili halikubaliki kabisa. Ndiyo maana wananchi wa baadhi ya sehemu binafsi wamenifurahisha sana.
Viongozi wote wanapaswa kufahamu kwamba nguvu yao inatoka kwa hao wanaowaita Kenge. Hili linapaswa kueleweka vizuri kabisa kuanzia ngazi ya chini kabisa ya mjumbe wa mtaa hadi kwa Rais.
Unafiki wa kuwapenda "kenge" wakati wa kutafuta kura zao, hatutaki.
Tunamtaka kiongozi kama Hayati JPM ambaye kamwe hakuweza kuacha kusikiliza wanyonge (kenge) kwenye mikutano yake.
Hatutaki kiongozi ambaye hakutaka kuwasikiliza wanyonge wakati wa kipindi chake cha urithi (ushahidi upo).
Hatutaki viongozi wenye kaliba ya "mama wa kambo".
Wananchi wa Butiama mmenifurahisha sana.
Hili naomba lisiishie Butiama tu, liende pote palipokuwa na viongozi wa hovyo waliowaona wananchi wao kama "Kenge" tu.
Sasa wakati wa kenge kuonesha umuhimu wao, umefika.
NOTE:
Mh. Balozi Polepole, shikilia hapo hapo, tuko pamoja na wewe.
Mungu ibariki Tanzania