Vikao halali vya chama au taasisi yoyote haviendeshwi kwa kuzingatia majungu au hisia bali kwa kufuata kanuni na sheria rasmi zinazojulikana!
Kama kuna mwenye uthibitisho kwamba Ridhiwani amefanya kosa lolote la kijinai au kimaadili apeleke pingamizi kwenye chama akiwa na ushahidi rasmi, vinginevyo itakuwa kama kelele za chura ambazo hazimzuii tembo kunywa maji.
Hata hivyo, pamoja na kwamba ni haki yake ya msingi na kikatiba kugombea uongozi, siyo vema sana kwa uongozi kulimbikizwa kwa baadhi tu ya familia, koo au kikundi fulani. Tunataka kuwepo social mobility kwenye jamii yetu yenye masikini wengi, watu wa lower class wapande middle na wa middle waende upper and vice versa. Hii inawezekana tu kama familia za juu hazitajilimbikizia hatamu za uongozi na mali.
Ni muhimu tujue kwamba hili siyo tatizo la Ridhiwani au baba yake Mh. J. Kikwete, Rais wa JMT, bali tatizo la mfumo mzima na halitamalizwa kutoa tuhuma zisizo na uthibitisho au majungu!